Dokta...nafuu umekuja mwenyewe. Unaweza kutuambia kwa maoni yako, ni kitu kimewafanya mshindwe kutoka kidedea Busanda? Na kuna marekebisho yoyote mfanyayo katika kampeni kutokana na haya matokeo?
Mtoto,
Thanks. Kwa maoni yangu kuna mambo kadhaa yaliyotufanya tushindwe. Facts ziko clear kwa sababu ni cases ambazo zimeripotiwa na polisi lakini kwa vile Polisi wamekuwa partisan hakuna hatua iliyochukuliwa.
1) Pamoja na kuwa ni kweli kuwa mtandao wa Chadema siyo mpana hadi kwenye vijiji kama ilivyo kwa CCM, mtandao sio muhimu sana kwa uchaguzi kwani Watanzania wengi wanaonyesha dhahiri kuwa "wamechoka" na wako hoi. Hivyo wanahitaji mabadiliko japo hawajui mabadiliko hayo yaje vipi, na wengi kutokana na level ya elimu yao, wanashindwa kuoanisha uhusiano kati ya kura yao na maendeleo. Hili ni tatizo la msingi kabisa, na siku 28 za Kampeni hazitoshi kabisa kupeleka elimu hii kila mahali( ukizingatia kwa mfano Bussanda inayo vijiji 75).
2) System yote ya Serikali, kuanzia Mkuu wa Wilaya, Tarafa, Kata hadi mtendaji wa Kijiji wanafanyia kazi chama Tawala, na hasa kwa kuwatumia Watendaji wa Vijiji na wa Kata (WEO na VEO) ambao kimsingi wanatumia sana vitisho. Kwa maeneo mengi hawa bado ni "Miungu watu" na wanaogopwa sana. Hawa ndio waliotumika kushusha bendera zetu, ndio waliotumika kupasua mabango yetu, na kusimamia zoezi la kuandikisha namba za Shahada na hatimaye kuzinunua.
Tunao ushahidi kamili na kesi kadhaa zilipelekwa polisi lakini hakuna kilichoendelea. Hata kesi mmoja ingelisimamishwa mahakamani wengine wangeliogopa kufanya hivyo. Lakini kwa vile ni syndicate, hakuna hatua iliyochukuliwa, hata waliokamatwa waliachiwa wakati yeyote aliyedhaniwa wa upande wetu alikamatwa na kukaa ndani, hata kwa flimsy charges kwa mfano Waitara Mwikwabe alikamatwa na tuhuma zilizoandikishwani kusemekana kutamka " Busanda ni zaidi ya Tarime" ambayo ni slogans za kawaida kisiasa. Lakini amelala lock up siku 5 na kesi yake iko mahakamani wakati aliyekamatwa kununua shahada ya kupigia kura waliachiwa na hadi leo hakuna mwelekeo kuwa watafikishwa mahakamani.
Afisa wetu Basil Lema na Sabula walivamiwa kwenye Guest house saa 6 Usiku, mlango kuvunjwa na makada wa CCM wakiongozwa na Mtendaji wa Kijiji na Diwani ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Geita. Maofisa wetu walipigwa sana na Basil alichomwa kisu, kwenye eneo la nyumba ya Diwani huyo ambako walipelekwa kwa kuongozwa na Mtendaji wa Kijiji. Walifungwa pingu ( hata polisi hawaelewei wakereketwa wa CCM walipata wapi Pingu), na hatimaye kuwafunga pia kamba mikono na miguu, mateso ya ajabu. Waliwaita polisi, lakini cha ajabu polisi walipofika walikamatwa wao (waliovamiwa) na polisi hawakutaka kusikia chochote mpaka tulipoingilia sisi kwa nguvu kubwa. Hadi leo wahusika hawakukamatwa na kupelekwa mahakamani. Ni dhahiri kuwa kuna jambo hapa.
3) Zoezi la kuandika namba za shahada na hatimaye kuzinunua imechangia kwa kiwango kikubwa katika kupunguza idadi ya wapiga kura hadi chini ya 40%.Utafiti wetu wa kina unaonyesha kuwa kwanza wanaandika namba za shahada kwa kupita nyumba hadi nyumba, kwa kutumia gear kubwa ya watendaji na maofisa VEO na WEO ikiandamana na vitisho. Baada ya kuwaandikisha wote huchambua wale ambao hawatawapigia kura, na hapo huanza kununua shahada, na kwa wanaoghairi hutumia mabavu, mathalan kata ya Nyakagomba alitumika mratibu wa Elimu kutoa vitisho vya kila aina ikiwa ni pamoja na kuwatishia kuwanyang'anya leseni za biashara, kunyang'anywa nyumba za biashara zilizopangishwa na kadhalika. Hivyo wengi wa watu wanaoondolewa katika upigaji wa kura ni wale ambao wana uhakika hawataipigia kura CCM kwa mujibu wa utambuzi wa viongozi na mtandao wao.
4) Rushwa kubwa iliyokuwa inatembea mchana kweupe, na hasa rushwa ya kitu kama Chumvi na "chupi", na matumizi ya fedha taslimu ambayo imeanzishwa safari hii, ni sababu kubwa sana vijijini kutokana na wananchi wengi wa vijijini kujali mahitaji ya "leo" badala ya mahitaji mapana (macro) yatokanayo na mchakato wa uchaguzi. Mathalan kijiji cha Nyachiluluma, tuliwakamata na kutoa taarifa polisi lakini polisi wakakataa kata kata kuwa " wanamaelekezo kuwa hawana ruksa ya kumkamata yeyote wakati wa uchaguzi mpaka maelekezo yatoke ngazi ya juu. OCD alipojulishwa naye akang"angania kuwa hiyo ni kazi ya PCB na PCB nayo haikuwa tayari. Katoro alikamatwa Mratibu wa Elimu aliyekuwa anagawa fedha wakati kura zinaendelea kupigwa na Returning Officer alipoulizwa alisema ni kosa kufanya hivyo. Polisi bado wakakataa kumkamata hadi tulipoamua kutumia nguvu na kumkamata kwa kutumia vijana wetu wenyewe. Wananchi nao walitaka kumpiga na katika hatua hiyo polisi waliingilia kumnusuru na kumpakia kwenye gari lao na kumchukua. Wakati polisi walipokataa kumkamata, alifika hapo Bwana Kiravu, Mkurugenzi wa Uchaguzi (T) akitaka akabadhiwe yeye, kwa kujua kuwa yeye hana mamlaka hayo alikataliwa. Lakini yeye ndiye aliyeenda kumtoa polisi. Mwenye kuelewa atajua hapo nako kuna nini? Hakuna kesi iliyoendelea. Mawaziri wamekutwa wakishiriki katika kugawa hizo rushwa.
5) Tunaushahidi wa dhahiri, tangu Airport Dar, hadi walipotua Geita, watuhumiwa wa Ufisadi ndio waliopeleka fedha Geita ili zitumike Busanda. Katika hali hii ni dhahiri vita haikuwa kati ya Vyama na CCM bali ufisadi na vyama kwa kutumia nguvu ya dola.
Ni kweli kuwa kazi ya kuandikisha namba za Shahada Biharamulo ilifanyika hata kabla ya kifo cha Kabuya. Ndiyo kusema kulikuwa na mawasiliano kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi na CCM kwa vile wakati huo, rufaa ya Kabuye ilikuwa haijaamuliwa. Lakini CCM waliisha kufahamu kuwa uchaguzi utafanyika. Tunao ushahidi wa hilo pia. Ni dhahiri Tume ya Uchaguzi (T) inafanya kazi ya CCM badala ya kuwa chombo huru kinachojitegemea kama inavyotaka ieleweke kila mara.
Kuna mengine mengi ambayo sikuyasema hapa yatajitokeza wakati tutakapotoa taarifa yetu kamili ya mchakato mzima wa Uchaguzi wa Busanda. Hatua kadhaa zimeisha kuchukuliwa na nisingelipenda kuelezea hatua hizi kwani ni mikakati ya ndani ambayo kwa hatua hii si vizuri kuitangaza hadharani. Niwajulishe tu wapenzi wetu kuwa kwa Biharamulo tumezingatia changamoto hizo zote, na tunajipanga kwa uangalifu zaidi ikiwa ni pamoja na kuzipigia kelele sana hujuma hizo za wenzetu kwenye ngazi zote.
Tusaidiane kwa wapenzi wetu wote, na ushauri wenu unakaribishwa sana.