Ushindi ni ushindi tuu, 'The Winner Takes it All, the looser standing small' ni wimbo wa ABBA.
Lazima tuipongeze CCM kwa ushindi wa kishindo.
Nimehudhuria kampeni na kushuhudia upigaji kura. aminini msiamini, CCM imeshinda sio kwasababu inapendwa sana, bali CCM imeshinda kwa sababu vijijini bado wamelala!, mimi ni Msukuma niliyezaliwa, kukulia na kusomea mjini. Kitendo na kurudi vijijini na kushuhudia jinsi low literacy level ilivyo kubwa, kimenistua, kimenisikitisha na kunihuzunisha!. Asilimia kubwa ya ndugu zangu hawajui kusoma wala kuandika! na hizo kura imebidi wapigiwe!.
Hii high ignorance level ya Watanzania, CCM wameitumia to their advantage. Siwatukani ndugu zangu Wasukumu, ila nimethibitisha CCM inaendelea kupendwa Kanda ya Ziwa kwa sababu za ujinga tuu!, sisi Wasukuma, sio watu wa fujo ila sio siri Wasukuma wa vijijini, wamelala mno!.
Inahitajika civic education ya ukweli kuwaelimisha mamilioni ya Watanzania wanaoichagua CCM bila kujua wanachagua nini au waendelee kuchagua CCM kwa sababu, au waipige chini CCM kwa sababu!. Pia kuna akina sisi tunaoichagua CCM kwa sababu so far, bado hakuna mbadala muafaka!. Baada ya kuhudhuria kampeni za Chadema jana pale Katoro, nikasema kama CCM itashinda, basi wanaKatoro ni vichaa au wamelogwa!.
Chadema imethibitisha inaweza kuwa chama mbadala, Watanzania waliolala wanazidi kuamka na wale wajinga wanazidi kuelimika. Naamini uchaguzi wa 2010 will never be the same, japo bado sioni anguko kuu la CCM, but as the going gets tough, the tough will get going, hivyo mabadiliko yanakuja.
Kwa wenzetu ilio mbali na Geita, Geita isikieni hivyo hivyo tuu mnavyoisikia!, Geita ndio wilaya yenye utajiri mkubwa wa dhahabu kuliko wilaya zote!. Kwa kifupi ndio wilaya tajiri zaidi Tanzania mzima kuliko wilaya nyingine zozote kwa utajiri wa madini ya dhahabu!, lakini watu wake ni masikini wakutupwa!.
Geita ina nyumba nyingi za udogo na nyasi kuliko nyumba za bati!. Watoto wa Geita, wanasura za kutilisha huruma!, Wakinamama wa Geita wasura za kukatisha tamaa, wakinababa wa Geita wana sura za mashaka, dada poa Geita ni buku!, buku mbili!, ukitoa dala unang'ang'aniwa! mdada anataka kuhamia, ile unagusa tuu, kwisha hata hujasema!, kama ni kwenu mtu unaweza kulia!.
Hiyo ndiyo Geita iliyozungukwa na mgodi mkubwa wa Geita Gold Mine, (wenyewe wanauita JIJIEMU kwa kukazia maneno Kisukuma!, upande mwingine kuna mgodi wa Bulyanhulu, upande mwingine kuna mgodi wa Buzwagi, upande mwingine mgodi wa Kahama Gold Mine, kitongoji cha Nyarugusu ndiko wanakohemea dhahabu wale wachimbani wadogo ambao kiukweli hali zao ni destitute!, yaani Geita ni dhahabu na dhahabu na dhahabu kila upande!, hivi kuna sababu kweli ya Geita kuzama kwenye lindi la Umasikini?. Yote hayo Wasukuma hawayajui, hawayaoni, wameambiwa hiyo dhahabu ni ya wazungu, na sasa inachimbwa kwa kazi nzuri iliyofanywa na CCM kuleta wawekezaji!, hivyo CCM is just so good na ndio maana bado mnawachagua kuyaendeleza mazuri haya kisa Wasukuma ni masikini by nature!, ila ni masikini jeuri, umasikini ni jadi yetu, utajiri hatuujui and you can never miss something you have never had!.
Wasukuma bado wamelala, wakiamka, walioamka watalala 2010!.
Naomba nikatishie hapa nisije ishia kulia bure...
Kidumu Chama Cha Mapinduzi ....