MUSSA ALLAN
JF-Expert Member
- Oct 13, 2013
- 18,925
- 13,280
nec na cc ya ccm inakuhusu nini wewe mchimba chumvi wa chagadema?hao ndo wanampa kiburi mamvi kwani hao ndo NEC au CC
nec na cc ya ccm inakuhusu nini wewe mchimba chumvi wa chagadema?hao ndo wanampa kiburi mamvi kwani hao ndo NEC au CC
Jinga sana wewe, Sijawahi kula hata senti tano ya CCM, ila nasukumwa na mapenzi binafsi kwa chama pamoja na ukweli kuwa CCM ndio chama makini kuliko vyote TANZANIA, licha ya mapungufu madogo madogo yanayojitokeza hapa na pale! Ila CCM haina Mbadala kwa sasa, Wengine ni wasaga sumu tu!
Kamati kuu ya CCM inayotarajiwa kukutana leo jioni jijini Dar es Salaam itatoa ujumbe mzito kwa wasaka urais wa CCM.
Rais Kikwete anayetarajiwa kuongoza kikao hicho, mbali na teuzi mbalimbali zitakazofanyika, pia Kikwete ameonyesha kukerwa na baadhi ya mwenendo ya wasaka urais wa CCM wakiwemo January Makamba, Edward Lowassa na Benard Membe ambapo anatarajiwa kutoa ujumbe mzito kwao.
Kiwete ameonyesha kustushwa na mwenendo wao wa kupiga kampeni waziwazi huku akisema kuwa "kamati kuu haitothubutu kuwapitisha wafanya mazingaombwe"
Cheki miCHADEMA inavyopenda kushadadia vita, hivi vita ni sera yenu? Maana Dr. Slaa aliposhindwa urais na JK mwaka 2010 alisema nchi haitatawalika lakini mwisho wa siku ameaibika kwani nchi inatawalika ipasavyo. Shame on you!
Ikitokea Padre,Dr Slaa kawa Rais wa Tz nitakuwa wa kwanza kuhama Tanzania.
Mandla.
Wapinzani Bado hamjakomaa kisiasa kiasi cha kupewa Nchi, subirini 2055 kama bado mtakuwa hai.
Yericko, hata kama CHADEMA inawaundermine members wengine wote wa UKAWA, huna haja ya kuandika kitu kama hiki hali ukijua wazi hakuna kikao chochote cha UKAWA kilichokaa na kubariki jina la Dr. Slaa. Ni mambo kama haya yanayoleta sintofahamu ndani ya UKAWA...."Urais Tanzania, kuanzia 25/10/2015, iwe mchana au usiku, iwe kiangazi au masika, iwe mawingu au jua kali, Dr Slaa chini ya UKAWA ndie rais wa wote....
UPDATES:
Kwahiyo kwa upeo wako, mtu yeyote anayeshiriki midahalo anafaa kukuongoza wewe na wenzio katika Urais?unamsifia nini sasa? mtu mwenyewe hata ukimuita kwenye mdahalo na january makamba anamtoa jasho hadi la unyayo
Usiniweke kwenye hiyo list ya watanzania wajinga.Watanzania wamesema mwisho wakutawaliwa na mafisadi ni octoba
hakuna kitu nachotamani kama hiki
lowasa akatwe na kamati kuu
baada ya kukatwa ahame ccm na wapambe wake woote
akishahama ccm kiparanganyike
kuanzia hapo tusiwe na chama tawala kibabe tena kama ca ccm
kuanzia hapo chama chochote cha upinzani kichukue nchi na kuanzia hapo tuwe tunabadilisha chama kinachotawala kama kenya
kila chama kikiingia madarakani kiwe macho kwani muda wowote kinaweza pigwa chini.
natamani ccm itoke madarakani
Jirani na mzee wetu wa awamu nne tengeneza historia na kudumisha heshima yako kwa maamuzi sahihi na yatakayoikomboa Tanzania mikononi mwa wanyanganyi. Amen
Naelewa sana kuwa alikuwa sehemu ya serikali iliyoshindwa na hata ya nyuma yake.Labda wewe na ukada wako ndio huelewi kuwa tatizo la nchi hii ni mfumo wa uongozi wa serikali na chama chako kinachoongoza. Nae alikuwa waziri mkuu tu tena awamu hii ya nne angeweza kushauri na sio kubadilisha lolote.Sasa anakuja kama kiongozi wa nchi na atafutilia mbali mfumo huu unaokumbatia wezi na kutoa maamuzi kwa wakati muafaka.Nadhani nimekuongezea uelewa fulani tofauti na unavyonifikiria kuwa mimi ni -----.
Waziri Mkuu ndio kiongozi mkuu wa serikali, Raisi mbwembwe tu.., mambo yote ya kiutendaji siku hadi siku yanaishia kwa PM, Raisi ana-deal na mambo ya kisera tu. Sasa kama PM kaboronga, kashindwa kushauri, hawezi kuja kudai kuwa ana kipya. Kwani hana ushawishi, na hawezi kuongoza, kama unashindwa kumshawishi mtu mmoja awe na sera sahihi, unaweza vipi shauri mamilioni kufuata sera zako?
Kama alishindwa kama Mtendaji mkuu wa serikali kufanya hizi porojo anazodai sasa hivi sidhani kama ana kipya.
Mimi ni chadem lakini Slaa sio presidential material kabisa mara mia asimamishwe makaidi au Dovutwa
Sasa anakuja kama kiongozi wa nchi na atafutilia mbali mfumo huu unaokumbatia wezi na kutoa maamuzi kwa wakati muafaka..
Kwako kubadilisha mfumo wa kuongoza serikali au chama sio mambo ya sera na madaraka yako kwa raisi kama ulivyokiri mwenyewe? Mtendaji mkuu wa serikali anatenda kwa maagizo ya aliye juu yake ambae ni raisi. Hivyo hivyo kwa mtendaji mkuu wa kampuni au shirika anaongoza kwa maagizo ya bodi na anawajibikwa kwao.Kama nitakuwa sahihi waziri mkuu wa sasa alishindwa kumwajibisha hata kumsimamisha tu kazi waziri alietakiwa kuwajibishwa na bunge. Nini kilitokea wote tunakumbuka waziri mkuu aliliahidi bunge kuwa ataongea na raisi aliekuwa ziarani A. kusini na kusikitika kwa kutokuwa na madaraka hayo. Pia wengi watakumbuka Lowassa akiwa wazri mkuu baada ya kugundua mapungufu ya richmond na kuwa hawawezi kuliletea taifa umeme alimpigia simu raisi akiwa nje ya nchi na kumweleza dhamira yake kuufuta mkataba wa serikali na richmond baada ya kubaini hawana utaalam, mtaji na hata ofisi nchini. Alieleza Lowassa mwenyewe kwenye kikao cha chama cha kamati kuu kuwa alijibiwa awaache hadi arudi nchini na aliporudi hakufanya maamuzi yoyote. Hiyo yote inaonyesha pamoja na utendaji wa shufhuli zote za serikali waziri mkuu hana nguvu ya kubadilisha lolote bali aliemteua. Nadhani sasa umeelewa vya kutosha na hutaniquote tena kwa jambo hili hili.