babukijana
JF-Expert Member
- Jul 21, 2009
- 16,313
- 20,896
Tujiulize nini chanzo na kwanini kagera.
Wakati nikiwa mwangalizi wa Uchaguzi jimboni mwaka 2010, kata za Kashai, Ijuganyondo, Hamugembe, na Buhembe CCM walipita kwa mbinde!
Lakini kumfumuza Ruhangisa ni kujiua zaidi mkoani Kagera maana yeye ni mzee wa kuchaguliwa bila kuwepo!
Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Bw Avelin Mushi amemaliza Press Conf hivi punde na kufafanua kuwa kikao cha Halmasahuri Kuu ya mkoa wa Kagera imemaliza kikao chake hivi punde na kuamua madiwani 8 wa Manispaa ya Bukoba kufukuzwa katika chama na kufutiwa nyadhifa za udiwani kutoka na mgogoro uliokuwa ukiendelea.
teh teh kweli mkuu wanajaribu kutikisa kiberiti kama kina njiti, walifanya hivyo songea pia!CCM wanalifahamu hilo mkuu, na hapa wanazuga tu madiwani wao baadae watawarudisha kupitia vikao vya juu!!!
hiyo rushwa ya million 20 nani awape!?,acha story bhana hakuna hata diwani mmoja hapo wa kukataa million 20, laki laki tu za Kagasheki zimewafanya wamsaliti mayor wao ije kua 20m!!! we unaijua bukoba au unaiskia!wanafukuzwa kwa kukataa kwao ufisadi na rushwa ya million 20 kwa kila mmoja?
ama kweli CCM ni chama cha mafisadi,anaepingana na ufisaidi sio mmoja wao.
nawapongeza madiwani hao kwa ujasiri wao wa kukataa unafiki na uchama
wakaweka maslahi ya nchi mbele na sio ya chama.
uchaguzi lini nashauri hawa hawa waingie chadema kura zote zitawarudia.
shame on you CCM na kizazi chenu
Shida itaendelea kwa ccm tu,wana bukoba wameipokea kauli hii kwa shangwe kuu,siyo kufukuzwa kwa madiwani,bali ni kufukuzwa ccm kagera.Kawaponza Kagasheki hawa. Jamaa alikuwa anawatumia na kuwalipa kwa manufaa yake mwenyewe na wao wakingia mkenge. Haya ndio malipo kwao. Mwenzao ka save. Lakini nashangaa kile kikao kwa nini hakikumchukulia hatua na yeye huku wakijua dhahili kwamba yeye ndiye muasisi na mpigaji wa debe wa jambo hili?
Alafu kafukuzwa mwenyekiti wa wilaya uanachama kisha mnasema mnaviachia vyombo vya juu kuamua? Kuamua nini wakati yeye si mwanachama? Hivi anaweza kuitisha vikao vya wilaya kama kiongozi wa chama?
Too much contradictions?
Fukuza na Kagasheki bila hivyo shida itaendelea kuwepo manispaa ya Bukoba.
Ndugu wanaCCM na wakereketwa wa chama chetu(dola) twawala,kama ilivyo ada katika mkakati wetu wa kuhakikisha kuwa tunaidhibiti CDM kwa kujibu mapigo.Kwaiyo ni furaha yangu mimi kama katibu wa chama tawala kuwatangazia rasmi kwamba siku ya leo tarehe 13/08/2013 chama chetu ngazi ya wilaya tumeamua kuwajibu CDM kwa kuwafukuza madiwani wetu wote nane wa wilaya ya Bukoba kama CDM walivyofanya jijini Arusha mwaka juzi.Ndugu wana CCM uamuzi huu umechukuliwa baada ya kutafakari kwa kina maslahi ya viongozi wetu wa ngazi za juu katika chama ambao wangeathirika kutokana na kusitishwa kwa mikataba hasa ule wa ujenzi wa soko kwani ulikuwa na maslahi manono,ivyo basi huu ni muendelezo wa kushughulikia wale wanachama wetu wote wenye viherehere kama tulivyomshughulikia Rais Jumbe alipochafua hali ya hewa visiwani mwaka 1984.Ndugu wanaCCM na wakereketwa ieleweke kwamba tunapofanya uamuzi huu mgumu hatumkomoi mtu bali tunatetea maslahi ya chama zaidi,rejea mijadala Bungeni ambapo mpaka sasa chama kimeweza kuliteka Bunge,sembuse madiwani??.Mwisho kabisa naomba wana-Bukoba watuelewe kwamba hakuna mtu aliye juu ya maslahi ya chama chetu twawala tukufu.KIGUMU CHAMA CHA MAPINDUZI,ZUDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI.Asanteni kwa kunisikiliza.
Ni mimi wenu mtiifu kwa maslahi ya chama na si taifa.