Kama fisadi ni moja tu ndani ya CCM, kama mikwara yote ya watangazania 42 inasababibishwa na mtu moja tu, kama katika idadi ya wananchama wanaodaiwa kuwa milioni tano (sic!) fisadi na mwizi ni mtu moja tu, kama kwa watangazania wote 42 ni mtu moja tu anayedhani chama ni cha kwake na kama, kama...duh! Heri hiki chama kivunjike vipande vipande kila moja abebe fito zake.
Fikiria mtu moja...EPA yeye, Richmond yeye, Kagoda yeye, Meremeta yeye, mauaji ya tembo yeye, kutoroshwa kwa twiga yeye, Escrow yeye, utawala dhaifu yeye, mauaji ya Albino yeye, ufujaji kwenye halmashauri yeye, madawa ya kulevya yeye, Katiba mbovu yeye, kero za Muungano yeye, ukosefu wa madawa hospitalini yeye, uhaba wa madawati yeye, kufeli katika masomo yeye, polisi kuua watu yeye, TISS kuwang'oa wananchi kucha na meno yeye, wanajeshi kuwapiga raia yeye, kuzurura nje kwa Raisi yeye na, na...
Bavaria, je unakubaliana na
Mzee Mwanakijiji kuwa kama ni kuvunjika ni heri CCM ivunjike haraka taifa lipate nafuu kwa kuondokana na yote niliyoyataja hapo juu?