CCK yaingia Arusha kwa kishindo

Like father like son sijui kama watakuwa na tofauti na wenzao ccm ktk ukandamizaji na wizi
 
Baada ya kukamilisha safu ya uongozi wa mkoa wa Arusha,CCK inatangaza rasmi kuwa tunaingia katika uchaguzi mdogo wa Arumeru kwa ajili ya kuchukua jimbo.

Hawa wanatakiwa kujipanga kwanza! sidhani kama kwa muda huu wana uwezo wa kushiriki uchaguzi wenye ushindani mkali kama huo wa Arumeru! ni vizuri wajenge chama kwanza kuliko kukimbilia kupata aibu ya kushindwa vibaya!!, watakosa wanachama baada ya kushindwa vibaya!!!
 
Hebu tuwe wakweli,kwa jinsi na muda ccm iliokaa madarakani imejijengea mtandao mkubwa saana katika kila kona ya nchi hii.
Kwa hiyo wale wanaonufaika na ccm kwa maslahi binafsi ni wengi mno na wanatosha kuunda chama cha kisiasa ambacho moja ya mikakati yao inakuwa ikiwahakikishia kutokaa mbali na pale kijiweni ili kulinda maslahi yao,na hapo ndio tunapoona mambo ya chama cha ki..sadi.
Ili yasiwakute yale ya kufikishwa mahakamani ndani ya machela

Hayo ni mawazo yako tu ambayo una uhuru wa kikatiba. Unazungumziaje taarifa zilizoenea kwamba iwapo CCM isingesimamisha kundi la wagombea fulani fulani uchaguzi wa Urais mwaka 2005, basi wagombea wale wangetimkia Chadema na platform hiyo ilishawekwa? Ebu tuwe wa kweli kwa hili, kama jinsi ulivyotaka tuwe wakweli kuhusu hoja yako.
 
Like father like son sijui kama watakuwa na tofauti na wenzao ccm ktk ukandamizaji na wizi

Isnt Mtei among the sons of CCM? Mtei alikuwa mwanachama wa TANU na baadae CCM, na aliondoka kwenda washington kufanya kazi na IMF, baada ya kukata tamaa na sera za Azimio lake la Arusha. Mtei na IMF ni chanda na pete. Tangia kuanguka kwa azimio la arusha, tunacho implement Tanzania ni IMF alternative to Development. Je, imemsaidia nini mtanzania baada ya kufa kwa ujamaa? Ni Mtei ndiye aliyeshirikiana na IMF kutuletea soko huria lillo holela ambalo ndio limezaa mijizi ndani ya CCM, na kumfanya mtanzania kuwa maskini kuliko hata enzi za Azimio la Arusha. Ni muhimu tuambiane ukweli sasa kwani hii tabia ya kuona vyama vingine vya upinzani ndio malaika wa nchi hii, huku vingine vikitukanwa haiwezi kuvumiliwa kwani haijengi demokrasia bali inaua demokrasia.
 
WALIPATA KUNENA HAYA: Nasser na utegemezi; "Yeyote yule ambaye hana uwezo wa kujitegemea mwenyewe, hawezi kuwa na sifa ya kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi yake mwenyewe".
Ni Mpendazoe yupi unayemsema? Mwacheni yuko shamba analima! Dhana ya kukihusisha CCK na baadhi ya watu ambao hawako kwenye chama hiki ife mara moja! Ni mawazo ya kipuuzi kama haya kila siku yanawaingiza Watanzania kwenye shida. Tunaendelea na tunasonga mbele, endelea kukejeli sisi tunajenga chama kipya. Kwa taarifa tu, baada ya kukamilisha uteuzi wa viongozi mkoa wa Arusha, Mkoa wa Dodoma nako kazi imekamilika tunaendelea mkoani Mtwara underground wewe piga domo lakini umeifanyia nini nchi yako?

he kumbe hamchagui? Mnapachikana vyeo.tobaaaa,wapi demokrasia?
 
Bwana mkubwa hawa watu kama kiongozi wao ni huyo Akitanda Constantine namfahamu sana na ni mtu makini sana labda kama kwa hizi siku chache kabadilika , nampenda ni kijana mpambanaji na mwadilifu sana, mgogoro wangu na wao uko kwa huko nyuma tulipotoka CCj tulikuwa na viongozi wa kitaifa matapeli ila yeye wakati huo alikuwa katibu mwenezi, alifanya kazi nzuri sana ila kuna uzembe mkubwa ulikuwepo awali, kama atakuwa na safu nzuri ya uongozi naamini baadaye chama chake baada ya Chadema kitafuatia. maana ccm,tlp,tadea,nccr,udp cuf aka KAFU na majina mengine yafananayo na hayo tutavisahau soon. ilmradi tu wasiwe ccmB. au wakawa wametumwa kuharibu, ila kama wako serious nina imani na Akitanda baada ya kukuta yupo. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Akitanda ni mtu makini sana iwapo ataungana na wapambanaji wenzake akina Willbrod Slaa,Mbowe,Lema ,Mdee,Mnyika,Kabwe, Ndessa na wengine kama hao ambao hupatikana Chadema.:welcome:

Binafsi, mimi simfahamu mwenyekiti wa CCK, wala viongozi wake wengine, lakini nafahamu kilichotokea katika usajili wa CCJ. Ile ilikuwa ni hujuma ambayo Chama tawala kilitaka CCJ ionekane ni wababaishaji. Na inaonyesha kwamba hiyo project ya kuwachafua CCJ imefanikiwa kwani kwa kauli za wengi humu, CCK inaonekana kama walikuwa ni wahuni tu. Mimi ni mwana ccm lakini penye kuhitaji ukweli, lazima ukweli uwekwe wazi. Siasa na njama za kuua vyama vingine havitatusaidia sisi CCM, sana sana vitakimaliza CCM. Vinginevyo waelewa juu ya uchafu uliojitokeza wakati wa usajili wa CCJ wapo wengi. CCM inahitaji mpinzani wa kweli, Chadema wanajitahidi lakini hawajatimia ki-itikadi. Wana umaarufu wa muda mfupi tu - siasa za personalities na kelele za ufisadi. Hivi viwili vikiisha, Chadema haipo, kama ilivyokuwa kwa NCCR Mageuzi na personalities zake kubwa (Prince bagenda, Mabere Marando, Masumbuko Lamwai, Kaborou, Mrema) na kelele zake nyingi kuhusu ufisadi chini ya serikali ya Mwinyi 1995. NCCR haipo juu tena, na pengine kwa sababu Chadema wamewekeza kwenye yaleyale kama ya NCCR - wana majina makubwa - Slaa, Mnyika n.k. Inaonekama kwamba wanaona mambo haya yangewasaidia chama kupata umaarufu wa upesi kwa formula la NCCR 1995, hivyo, kuibuka kwa vyama vipya kama CCK kunawaogopesha, na ndio maana mashabiki wake wanakimbilia matusi, majungu na kashfa. Chadema, acheni majungu, wekezeni kwenye itikadi. Msomeni Mwanakijiji pia katika gazeti la leo la Tanzania Daima Lipo Online - ana makala nzuri sana inayosema: Kuikumbatia CCM Ni Hatari. Makala hii inawahusu sana Chadema.
 
CCK ni chama kidogo, hakina jina wala uwezo wa fedha ulivyo kwa vyama vingine. Hauna watu wakubwa na kimeanzishwa na vijana waliokatishwa tamaa wakati wa kuanza CCJ. Wale waliotaka madaraka walionekana wakatoka na kukimbia when the going was getting tough; lakini wachache waliodharauliwa, kudhalilishwa na kupuuzwa ambao kwa kila kipimo walitakiwa wawe wamekata tamaa walijikongonja wakaganga majeraha yao na wakaamua kubadili mkakati kabisa! Kinyume cha matarajio ya wengi wakafanikiwa - tena kimya kimya kabisa - kuzunguka nchi nzima na kupata wanachama na hatimaye kupata usajili wa muda na baadaye Msajili - baada ya kufanya uhakiki - akaona wametimiza matakwa yote na akawapatia usajili wa kudumu.

Sasa, ni kweli hiki chama inaonekana hakitakiwi kuwepo na wapo ambao kwa kweli wangependa kisiwepo. Nakumbuka vita ile kubwa kabisa ya kuelekea 2010!! Ninachosema ni hivi - kama kuna chama cha siasa ambacho kinaamini kuwa kina uhodhi wa fikra na mioyo ya Watanzania kinajidanganya. Chama chochote cha siasa kinachotaka kuwaongoza Watanzania ni lazima kiwe tayari kutambua kuwa kinaitwa kutumika siyo kutumiwa. CCK kwangu mimi ni kama mtoto asiyetakiwa; hakuutakiwa na wazazi wake, hakutakiwa na jamii yake, na akabakia mitaani. Wengi walimtupa na kusema "hawezi na hafai" na kuwa ni "mvuta bangi". Lakini yeye mwenyewe alijitambua ni nani.

Hakuna sababu yoyote ya kuibeza, kuiogopa au kujaribu kuivuruga CCK. Na wala tusiogope kutoa ushauri mzuri ili wajijenge ndio sehemu ya demokrasia yenyewe. Tusiogope kuwa labda CCK watachukua nafasi "yetu" badala yake tuwasikilize na kuona hoja yao ni ipi na kama ni ya msingi tuangalie ni jingi gani tunaweza kuitriangulate.
 
Tanzania ina matatizo ya kimfumo,mna maoni na mapendekezo gani ya tatizo hili?
 
Mkuu wangu navyokusoma tayari nakuelewa huna tofauti kabisa ni kama viongozi waliopo ama waliopita ambao wanafikiria chama ni NGO au shirika. Na hata iwe hivyo, huwezi kuingia mahala kichwa kichwa kabla hujaweza kujitangaza na kupata support ya wananchi. Niulize mimi kama naweza kukupa kura yangu? jibu likakua hapana na sababu ni kwamba sielewi lolote kuhusiana na CCK zaidi ya katiba na sera zenu. Mkuu wangu unahitaji kuzaa WANACHAMA kwanza kabla ya mjumbe bungeni..

Hayo ya kupambana na rushwa,posho na kadhalika unayasema wewe hapa JF na hizi ni ahadi hewa tulozisikia kwa viongozi wote wakati wakigombea ubunge na tatizo ni kwamba haijafanywa sheria kwa chama kutekeleza sera zao kama walivyoainisha. Inatakiwa kwanza mtueleze kwa nini CCK ni tofauti na vyama vingine, kwa nini tuwaamini viongozi wenu maana usije nambie Lowassa au Rostam ndiye muasisi wa chama na mjumbe wa CC. Nini hasa madhumuni ya kuanzishwa kwa chama hiki na kwa kupigania haki za kina nani? maana neno wananchi wanyonge pekee haitoshi.. kuna vyama vya haki za binadamu na havigombei ubunge. Tumewaona wafanyabiashara wakubwa wakisema wanapigania haki ya wanyonge, kisiasa mkuu wangu hakuna kitu kama hiki.. Kina CHE, Castro na wengine wametoka ktk jamii za wanyonge na wanaelewa shida za wanyonge, hizi habari za matajiri kufungua vyama mkuu wangu ni biashara tu maana kama kweli wewe tajiri na unataka kusaidia wanyonge basi fungua hata NGO na kugombea Ubunge..Kusema kweli mnatuchezea tu akili zetu..

Kibaya kuliko yote mnaingia kwa kujificha ficha sielewi mnachoogopa. Mimi nataka kujua nani amekuja na wazo hili la CCK kisha tumpime kama yeye na waasisi wengine wote ni wapiganaji..Na amini maneno yangu hamuwezi kujiingiza ktk uchaguzi haraka kiasi hiki mkidhania kwamba ni uhshuda wa kuwaonyesha wananchi mnataka kuleta mabadiliko kupitia sanduku la kura, sanduku ambalo ni sehemu ya ufisadi uleule..Hapa nilipo mimi, binafsi yangu nashindwa hata kuelewa kwa nini Chadema na CUF vinaendelea kushiriki ktk chaguzi ambazo wanafahamu fika kwamba haki haitatumika au wananchi wenyewe wamepuuza hata kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa sababu wanajua haki yao ya kuchagua haitapokelewa..

Na kwa kila mnavyozidi kukumbatia mfumo mbovu kama huu ndivyo CCM inavyozidi kushinda kwa sababu wananchi wasiopiga kura wengi ni wale wasioipenda CCM maana CCM ina mpango wa kukusanya watu wake kwa lazima kupitia wajumbe wa nyumba 10 na kadhalika. Kwa mwana CCM kutopiga kura unachukuliwa kama msaliti hivyo kila mwananchama wa CCM kwa kadi au mapenzi husisitizwa hupiga kura kwa kupewa Khanga au Tshirt na mshiko kidogo wakati nyie mnategemea uzalendo wa WATU waliokwisha poteza Uzalendo kutokana na mfumo wa Msituni (Darwin). Sisi waislaam tuna hadithi ya Mtume inayosema Fukara yaani maskini wa mali ni sawa na Kafir..Umaskini ni mbaya na adui mkubwa wa maskini wenyewe, huyu ni mbaya kama fisi ambaye anaweza kula mwanaye au hata matumbo yake mwenyewe akisha jeruhiwa..

Usije sema nawakatisha tamaa lakini mtakuja nambia siku ya siku maana sisi wengine tumejaliwa kuyaona msoyaona, nisome vizuri..

Nadhani kuna hoja nzuri sana hapa ila zinahitaji ufafanuzi zaidi. Lakini muhimu zaidi haujatoa mapendekezo nini kifanyike kurekebisha mapungufu hayo. Je, unapo himiza umuhimu wa haki kwa wananchi, katika kipindi hiki cha maandalizi ya kupata katiba mpya yenye kutoa na kulinda haki hizo, vyama vya siasa vifanye nini, vikache uchaguzi ndogo kama za Arumeru na kujikita zaidi katika kujiandaa kutafuta haki chini ya katiba mpya? Sijakupata vizuri katika hili, ingawa nadhani naelewa unaelekea wapi. Kwa mtazamo wako, je vyama vya upinzani vifanye nini kati ya kipindi hiki na katiba mpya 2014/15?

Kuhusu CCK kushiriki uchaguzi wa Arumeru hata kama ni wageni katika siasa, ni muhimu tutambue kwamba, mbali ya CCK kuwa na haki sasa na CCM, Chadema, CUF, NCCR etc in that context kwa mujibu wa sheria chini ya msajili wa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi, any publicity, no matter how bad, is good publicity.
 
Je tuwatofautishe vipi na chama kama tadea, TLP na nk yaaki mna lipi jipya....

Kwanini hamjishughulishi na hao Tadea, TLP kama mnavyojishughulisha na CCK in relation to Chadema? Hivi kuna thread yoyote humu inayojadili Tadea, TLP, Jahazi Asilia na vyama vingine in relation to Chadema au CCM? Kwahiyo kwa kusaidia kujibu swali lako ni kwamba, CCK ni tishio kwa CCM na Chadema, na utofauti huo ndio unaokupa msukumo wa kuja na swali ulilouliza. CCK wametuwekea humu katiba yao na wengi tukachangia mawazo na kubaini utofauti mkubwa uliopo baina ya CCK na vyama vingine. Ukipata muda, jaribu kuisoma katiba hiyo humu JF. Na hakujawahi kutokea chama cha siasa kikatoa draft ya katiba yake kwa wananchi kujadili. Huo ni utofauti mwingine.

Kwa kweli CCK wanatia sana moyo, na kwa maoni yangu, Chadema isipokuwa makini, CCK itakuwa Chama Kikuu Cha Upinzani Tanzania ndani ya miaka saba. Mimi ni mwanachama wa kawaida tu wa CCM, sina mkataba wowote na CCM kwani sina uongozi wowote ndani ya CCM na siweki uzito katika kutafuta uongozi wa aina yoyote ndani ya CCM kwasababu siamini kwamba njia pekee ya kuchangia maendeleo ya nchi yako ni kwa kupitia uongozi ndani ya CCM. Vinginevyo muhimu ni kwamba bado nina amini katika vision ya Nyerere kuhusu future ya nchi yetu. Chama chochote kitacho onyesha kuwa na vision hii, chama hicho kitakuwa na nafasi kubwa sana katika nafsi yangu, na ninaweza kabisa kwenda kukipigia kura yangu kwenye uchaguzi katika eneo husika. Hii ni kwa sababu, pamoja na kwamba Nyerere alikuwa mwana CCM, utaifa ulimtangulia kuliko CCM na ndio maana alidiriki kupambanana majangili ndani ya chama alicho kiasisi mwenyewe kwa maslahi ya watanzania wote, mpaka alipokutana na umauti wake. Isitoshe, Nyerere aliwahi kutamka kwamba: "CCM Sio Mama Yangu, Naweza Kuachana Nayo". Same applies to many leo hii, uwe CCM, Chadema, CCK, CUF, NCCR n.k, vyama vyote hivi sio mama zetu, lakini kuna baadhi ya vyama ambavyo vinamkaribia mama kwa maana ya kuwa na uwezo wa kututetea kwa dhati.
 
Umetokea msikiti gani weye?

Islamophobia ni ugonjwa hatari
sana. Ugonjwa huko siku nyingi
sana ila kwa miaka ya hivi
karibuni umekuwa ukikua kwa
kasi ya ajabu sana. Aliyeathiriwa
na ugonjwa huu huwa anaogopa UISLAM na vitu vyote
vinavyohusiana na UISLAM.
Mfano, mtu anayeumwa
ISLAMOPHOBIA akiona mtu
amevaa kofia ama kanzu ama
hijabu, mtu huyu huwa anaogopa sana na huwa anateseka sana
katika nafsi yake. Au mgonjwa
wa islamophobia akisikia kuwa
waislam wanataka kuanzisha
mahakama ya kazi basi yee
huwa hapendi na maumivu humsonga moyoni mwake.
Wagonjwa wa islamophobia
huwa hawapendi kuona uislam
ukienda mbele ama sharia za
kiislam zikifuatwa.
 
Nadhani kuna hoja nzuri sana hapa ila zinahitaji ufafanuzi zaidi. Lakini muhimu zaidi haujatoa mapendekezo nini kifanyike kurekebisha mapungufu hayo. Je, unapo himiza umuhimu wa haki kwa wananchi, katika kipindi hiki cha maandalizi ya kupata katiba mpya yenye kutoa na kulinda haki hizo, vyama vya siasa vifanye nini, vikache uchaguzi ndogo kama za Arumeru na kujikita zaidi katika kujiandaa kutafuta haki chini ya katiba mpya? Sijakupata vizuri katika hili, ingawa nadhani naelewa unaelekea wapi. Kwa mtazamo wako, je vyama vya upinzani vifanye nini kati ya kipindi hiki na katiba mpya 2014/15?

Kuhusu CCK kushiriki uchaguzi wa Arumeru hata kama ni wageni katika siasa, ni muhimu tutambue kwamba, mbali ya CCK kuwa na haki sasa na CCM, Chadema, CUF, NCCR etc in that context kwa mujibu wa sheria chini ya msajili wa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi, any publicity, no matter how bad, is good publicity.
Mkuu wangu nadhani wewe unatazam picha hii ukiwa ndani ya chama chako na kufanya mzaha ktk swala ambalo linatumaliza Watanzania wengi. Hizi habari za CCM sio mama yangu naweza kuachana nayo ni hadithi za Buricheka maana walioweza kuondoka wameondoka, lakini kama bado umo ndani basi una maslahi yako maana hakuna sifa yoyote ambayo inaweza kumwekla mwanaharakati ndani ya CCM.. Utanisamehe mkuu wangu ktk hilo..

Halafu kama wewe mwanachama wa CCM huwezi kuyaona nayozungumza kwa picha ile ile zaidi ya klutumia hiyo katiba ambayo mnaipanga wenyewe bila kumhusisha mwananchi hadi pale mtakapo taka NYIE ahusishwe. Na nazungumza haya yote sii kwa sababu ni Mwana Chadema bali mwanaharakati ambaye naitafuta haki ya wananchi kupitia vyombo hivi, hivyo sitazami hiyo katiba kitu ambacho hakipo leo nielndelee kutegemea labda kesho itakuwa bora zaidi.

Wazee wetu walipopigania Uhuru walikuwa ahadi nyingi tu, wakaahidiwa kupelekwa Ulaya na kupewa elimu, nyumba utadhani shetani alojmjaribu Yesu, lakini haikuweza badilisha nia zao. Wazee wetu waliambiwa tena ya kwamba - Watanzania bado hatupo tayari kuwa Huru na wakoloni walituwekea sera za kila aina kutonyesha wao wana nia nzuri na sisi lakini wazee wetu wakikataa katu na kusema - Tupeni nchini yetu na tutajikongoja vivyo hivyo.. Ndivyo navyoitazama Tanzania ya leo hatuhitaji maamuzi ya CCM hata kidogo bali sisi wananchi ndio wa kuwaambia CCM tunataka nini..

Chadema na CUF hawana sababu kabisa ya kuendelea kugombea chaguzi ndogo kama hizi wakati kuna chaguzi nyingi za nyuma wamepigwa chini, sasa waendelee tu kushiriki wakisubiri katiba?..Na kuna ushahidi gani hiyo katiba itawaletea mwongozo bora ambao utawawezesha wao kushinda. Mkuu wangu kupitia chama chako HAIWEZEKANI kabisa Chadema au chama kingine chochote kushinda kupitia sanduku la kura ikiwa katiba hiyo itaandikwa na wana CCM - HAIWEZEKANI labda kitafutwe chombo cha kimataifa kuifanya kazi hiyo maana najua fika majibu yake. Nasema sioni sababu kabisa ya vyama vya Upinzani kuendelea kugombea uchaguzi mdogo wakati wanatakiwa kuandaa mazingira ya uchaguzi wa 2015..Bora hata hao madktari waliogoma wameonyesha watu waliopania kuipata haki yao wenyewe.

Unapozungumzia CCM na kuharibu vyama vya Upinzani hii ni kawaida yake wala hawana wasiwasi maana waliweza kukivuruga NCCR lakini watu mnafikiria kwamba ni chama hicho kilichokuwa na matatizo.. Wameweza pia kukivuruga CUF na sasa hivi wanaitafuta Chadema hii inajulikana wazi wala haina ubishi kwani ktk mbinu zake mojawapo na kubwa ilotumika sana ni kuvunja nguvu ya chama mbadala cha ushindani. Na kwa bahati mbaya hawa vijana wa CCK mnaowasifia wameingia msikitini na mguu wa shoto. Haraka ya nini uda bado upo sana kufikia 2015, onyesheni uanaharakati wenu kwanza mpate kusifiwa na wananchi.

Na pengine huelewi maana ya Bad publicity is Good Publicy ni kama tunavyomsema Lowassa au Zitto. Ni kaa uweke tangazo baya linalouddhi watu lakini watu huitana kulitazama ili kesho libakie kichwani mwao na pengine hata waende KUNUNUA.. haina maana nje ya hiyo kama wanavyotaka CCK kujtangaza kana kwamba chama ni chao WAO na wao ni kina So and SO, heee! imekuwa bendi ya kizaire?.
Chama ni WANACHAMA unakitangaza chama ili upate wanachama wengi na through them ndipo chama kinajinadi kirahisi kutokana na mvuto huo. Kwenda kugombea Ubunge Arumeru haina kujitangaza bali unaingia ktk mashindano bila wachezaji afadhali hata wangekuwa miguu peku lakini wamekamilika.

Mkuu wangu kwa dalili hii inatuonyesha wazi kwamba CCK haikujiandaa kuchukua NCHI bali inadandia majimbo hapa na pale wapate KULA.. mabadiliko huanza na kuonyesha kivitendo yale unayoyalaani.. Kujenga UANAHARAKATI na kuzivuta mioyo ya watu washiriki nawe ktk vita dhidi ya utawala au vitu unavyopigania hata iwe UFISADI..lakini kuingia uchaguzi huku umebeba bango la Itikadi na sera mkuu wangu hii nisawa kabisa na kujidanganywa wao wenyewe.

Hata hivyo nawatakia kila la kheri ingawaje najua fika wameanza vibaya na pengine ndio utakuwa fundisho kwa vijana wadogo wanakurupukia siasa bila kujianda na vita nje ya sanduku la kura.
 
@mkandara

Embu Tuache wananchi tupate burudani na mawazo mapya na CCK..

Unajua Chadema tumeshaanza kuchoka na wengine hata mtufanyeje hatuwaamini tena chadema??
 
@mkandara

Embu Tuache wananchi tupate burudani na mawazo mapya na CCK..

Unajua Chadema tumeshaanza kuchoka na wengine hata mtufanyeje hatuwaamini tena chadema??
MKuu wangu hata mimi sina mapenzi hayo isipokuwa nategemea kuona kitu cha Uhakika na sii ubabaishaji ule ule. Nahcojenga hapa ni kuwatakia kheri na kuwaelekeza mwanzo mzuri maana nilifanya hivi hivi wakati wa Chadema kinajipanga.. walinichukia vile vile wakidhani nawabeza..
Nipo Chadema kwa sababu bado ninalo tumaini na wala sii kupitia sanduku la kura japokuwa nakatishwa tamaa sana na mawazo ya wanachama wake wengi.
 
Mkuu wangu nadhani wewe unatazam picha hii ukiwa ndani ya chama chako na kufanya mzaha ktk swala ambalo linatumaliza Watanzania wengi. Hizi habari za CCM sio mama yangu naweza kuachana nayo ni hadithi za Buricheka maana walioweza kuondoka wameondoka, lakini kama bado umo ndani basi una maslahi yako maana hakuna sifa yoyote ambayo inaweza kumwekla mwanaharakati ndani ya CCM.. Utanisamehe mkuu wangu ktk hilo..

Halafu kama wewe mwanachama wa CCM huwezi kuyaona nayozungumza kwa picha ile ile zaidi ya klutumia hiyo katiba ambayo mnaipanga wenyewe bila kumhusisha mwananchi hadi pale mtakapo taka NYIE ahusishwe. Na nazungumza haya yote sii kwa sababu ni Mwana Chadema bali mwanaharakati ambaye naitafuta haki ya wananchi kupitia vyombo hivi, hivyo sitazami hiyo katiba kitu ambacho hakipo leo nielndelee kutegemea labda kesho itakuwa bora zaidi.

Wazee wetu walipopigania Uhuru walikuwa ahadi nyingi tu, wakaahidiwa kupelekwa Ulaya na kupewa elimu, nyumba utadhani shetani alojmjaribu Yesu, lakini haikuweza badilisha nia zao. Wazee wetu waliambiwa tena ya kwamba - Watanzania bado hatupo tayari kuwa Huru na wakoloni walituwekea sera za kila aina kutonyesha wao wana nia nzuri na sisi lakini wazee wetu wakikataa katu na kusema - Tupeni nchini yetu na tutajikongoja vivyo hivyo.. Ndivyo navyoitazama Tanzania ya leo hatuhitaji maamuzi ya CCM hata kidogo bali sisi wananchi ndio wa kuwaambia CCM tunataka nini..

Chadema na CUF hawana sababu kabisa ya kuendelea kugombea chaguzi ndogo kama hizi wakati kuna chaguzi nyingi za nyuma wamepigwa chini, sasa waendelee tu kushiriki wakisubiri katiba?..Na kuna ushahidi gani hiyo katiba itawaletea mwongozo bora ambao utawawezesha wao kushinda. Mkuu wangu kupitia chama chako HAIWEZEKANI kabisa Chadema au chama kingine chochote kushinda kupitia sanduku la kura ikiwa katiba hiyo itaandikwa na wana CCM - HAIWEZEKANI labda kitafutwe chombo cha kimataifa kuifanya kazi hiyo maana najua fika majibu yake. Nasema sioni sababu kabisa ya vyama vya Upinzani kuendelea kugombea uchaguzi mdogo wakati wanatakiwa kuandaa mazingira ya uchaguzi wa 2015..Bora hata hao madktari waliogoma wameonyesha watu waliopania kuipata haki yao wenyewe.

Unapozungumzia CCM na kuharibu vyama vya Upinzani hii ni kawaida yake wala hawana wasiwasi maana waliweza kukivuruga NCCR lakini watu mnafikiria kwamba ni chama hicho kilichokuwa na matatizo.. Wameweza pia kukivuruga CUF na sasa hivi wanaitafuta Chadema hii inajulikana wazi wala haina ubishi kwani ktk mbinu zake mojawapo na kubwa ilotumika sana ni kuvunja nguvu ya chama mbadala cha ushindani. Na kwa bahati mbaya hawa vijana wa CCK mnaowasifia wameingia msikitini na mguu wa shoto. Haraka ya nini uda bado upo sana kufikia 2015, onyesheni uanaharakati wenu kwanza mpate kusifiwa na wananchi.

Na pengine huelewi maana ya Bad publicity is Good Publicy ni kama tunavyomsema Lowassa au Zitto. Ni kaa uweke tangazo baya linalouddhi watu lakini watu huitana kulitazama ili kesho libakie kichwani mwao na pengine hata waende KUNUNUA.. haina maana nje ya hiyo kama wanavyotaka CCK kujtangaza kana kwamba chama ni chao WAO na wao ni kina So and SO, heee! imekuwa bendi ya kizaire?.
Chama ni WANACHAMA unakitangaza chama ili upate wanachama wengi na through them ndipo chama kinajinadi kirahisi kutokana na mvuto huo. Kwenda kugombea Ubunge Arumeru haina kujitangaza bali unaingia ktk mashindano bila wachezaji afadhali hata wangekuwa miguu peku lakini wamekamilika.

Mkuu wangu kwa dalili hii inatuonyesha wazi kwamba CCK haikujiandaa kuchukua NCHI bali inadandia majimbo hapa na pale wapate KULA.. mabadiliko huanza na kuonyesha kivitendo yale unayoyalaani.. Kujenga UANAHARAKATI na kuzivuta mioyo ya watu washiriki nawe ktk vita dhidi ya utawala au vitu unavyopigania hata iwe UFISADI..lakini kuingia uchaguzi huku umebeba bango la Itikadi na sera mkuu wangu hii nisawa kabisa na kujidanganywa wao wenyewe.

Hata hivyo nawatakia kila la kheri ingawaje najua fika wameanza vibaya na pengine ndio utakuwa fundisho kwa vijana wadogo wanakurupukia siasa bila kujianda na vita nje ya sanduku la kura.

Diagnosis imeeleweka, sasa tunapata vipi tiba? Na je, mwanachama yoyote wa CCM, wa mjini na wa kijijini ni wa kulaumiwa kwa matatizo haya? Maana "nyie nyie" zimekuwa nyingi sana katika hoja zako. Je, wanachama wenye matumaini na CCM unawapa nafasi gani? Au ni malofa as long as wanabakia CCM? Usisahau kauli yako sahihi kwamba chama ni watu, sio mtu mmoja mmoja.

Una hoja nyingi za msingi lakini ile ya NCCR kwamba wameharibiwa na CCM sio kweli hata kidogo. NCCR ilimvuta hadi Wassira ambae isingekuwa awamu ya nne kumpitisha JK, wasira angekuwa NCCR mpaka kesho, kama sio kuhamia Chadema na kundi lote kama ilivyo ripotiwa. kwanini? alikuwa anatafuta madaraka. Na hiyo ndio sababu kuu ya wanasiasa wengine wote hata vyama vya siasa - kukamata madaraka, halafu ndio wajipange kutatua matatizo ya nchi. Mambo hayaendi hivyo kwani unaweza kujikuta unaingia ikulu kwa siasa za kubahatisha bahatisha na usikae madarakani kwa zaidi ya miaka mitano.

Kilichoiua NCCR ni haraka haraka, ambayo hata wewe unaizungumzia katika moja ya hoja zako kuu. NCCR waliwekeza kwenda Ikulu na wakaona Mrema ndio kete yao. Sababu unazotoa wewe za kuanguka wa NCCR zipo lakini ni secondary, vinginevyo ni jambo lisilokuwa na ubishi kwamba the primary reason to why NCCR ilianguka ni NCCR yenyewe - waliwekeza kwenye vitu vya muda mfupi kama vile personalities na vuvuzela la ufisadi, bila ya kujijenga ki-itikadi, ndio maana baada ya kushindwa uchaguzi, wakaishiwa hoja. Hili ni tatizo katika chama chako cha Chadema pia kwani hata Slaa miezi michache iliyopita, kwenye TV alitoa tamko la ajabu kidogo pale aliposema kazi yetu kubwa chadema ni kuikosoa serikali, na ikitokea ikajirekebisha, tutaishiwa hoja. Matamshi haya sio ya kutolewa na chama cha siasa, hasa chama kikuu cha upinzani, hizi ni hoja za pressure groups kama akina Mtikilia na wengineo, sio chama kikubwa cha siasa kama Chadema. Ndio maana Chadema pamoja na mafanikio yenu kadhaa, bado inawapa shida watu wengi kuona kwamba Chadema ndio mbadala wa kweli. Ni jambo lililo wazi kwamba hata miongoni ma vijana wasomi, wamegawanyika kuhusu Chadema. Msiendeshe siasa kama za pressure groups, endesheni siasa programmed, vinginevyo mtaishia kuilamu CCM kwa makosa mengine ambayo ni ya kwenu wenyewe.

Nikiwa bado kwenye suala la kuanguka kwa NCCR, haaingii akilini kwamba eti wasomi wote wale, kwa pamoja warubuniwe na wachotwe akili na CCM, how? Haijawahi kutokea wasomi wakubwa wa namna hii, kwa umoja wao, kushindwa na CCM na serikali yake katika mazingira ya siasa, kwani historia ya nchi yetu inatuelezea suala tofauti kabisa na hili.

Again, umetoa diagnosis nzuri lakini sijaona solution zaidi ya ile kwamba "CCM haiwezi angushwa kupitia sanduku la kura, unless waje international observers". Pia bado sioni kwanini CCK wasishiriki katika uchaguzi Arumeru, kwa dhana ile ile ya any publicity is good publicity. Inawezekana kabisa wasishinde lakini ni muhimu wakatumia haki yao chini ya sheria zilizopo, kwenda kujipatia uzoefu katika chaguzi zozote kabla ya mwaka 2015. Binafsi, sioni dhana ya haraka haraka katika hili kwani publicity na kuuza sera ni part ya kujijenga, na chaguzi hizi ndogo ndogo ndio the best platoform kufanikisha lengo hilo. Mimi nadhani hilo ndo lengo lao kuu, kwenda kuuza sera zao kwani matukio ya kampeni za wagombea wa Arumeru yata trickle down the whole nation.

Na je, Mwaka 2010, mtu angewaambia Chadema mna haraka sana msigombee Urais, jipangeni zaidi kwenye majimbo, kwa mtazamo wako hoja hiyo ingekuwa sahih? Kwani 2005, CCM ilishinda urais kwa 82%, na je bila ya kujaribu/kujipima mwaka 2010 mngeweza kweli kubaini nguvu yenu? Msiwaogope CCK, waacheni wafanya vitu vyao kwa jinsi wanavyojisikia wao ili mradi hawavunji sheria na taratibu zilizopo. Una hoja nyingi sana nzuri Mkuu Mkandara ambazo ungezipanga katika mazingira ya kuleta mjadala wa kisera na ki-itikadi kwa kuangalia je, vyama vya CCK, Chadema, CCM, CUF, NCCR, vinawapa watanzania varieties gani na nani yupo tofauti na kivipi n.k, hakika tungejifunza mengi sana. Pia nikuulize mkuu, leo hii ukienda kijijini kwenu na ukapata wasaa wa kuzungumza na vijana ambao hawana ufahamu wowote wa siasa lakini wangependa wachagua chama cha kujiunga au kukipigia kura, ungeitumiaje nafasi hiyo kuiuza Chadema/ungeiuzaje Chadema?
 
Back
Top Bottom