Baada ya kukamilisha safu ya uongozi wa mkoa wa Arusha,CCK inatangaza rasmi kuwa tunaingia katika uchaguzi mdogo wa Arumeru kwa ajili ya kuchukua jimbo.
Hebu tuwe wakweli,kwa jinsi na muda ccm iliokaa madarakani imejijengea mtandao mkubwa saana katika kila kona ya nchi hii.
Kwa hiyo wale wanaonufaika na ccm kwa maslahi binafsi ni wengi mno na wanatosha kuunda chama cha kisiasa ambacho moja ya mikakati yao inakuwa ikiwahakikishia kutokaa mbali na pale kijiweni ili kulinda maslahi yao,na hapo ndio tunapoona mambo ya chama cha ki..sadi.
Ili yasiwakute yale ya kufikishwa mahakamani ndani ya machela
Like father like son sijui kama watakuwa na tofauti na wenzao ccm ktk ukandamizaji na wizi
WALIPATA KUNENA HAYA: Nasser na utegemezi; "Yeyote yule ambaye hana uwezo wa kujitegemea mwenyewe, hawezi kuwa na sifa ya kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi yake mwenyewe".
Ni Mpendazoe yupi unayemsema? Mwacheni yuko shamba analima! Dhana ya kukihusisha CCK na baadhi ya watu ambao hawako kwenye chama hiki ife mara moja! Ni mawazo ya kipuuzi kama haya kila siku yanawaingiza Watanzania kwenye shida. Tunaendelea na tunasonga mbele, endelea kukejeli sisi tunajenga chama kipya. Kwa taarifa tu, baada ya kukamilisha uteuzi wa viongozi mkoa wa Arusha, Mkoa wa Dodoma nako kazi imekamilika tunaendelea mkoani Mtwara underground wewe piga domo lakini umeifanyia nini nchi yako?
Bwana mkubwa hawa watu kama kiongozi wao ni huyo Akitanda Constantine namfahamu sana na ni mtu makini sana labda kama kwa hizi siku chache kabadilika , nampenda ni kijana mpambanaji na mwadilifu sana, mgogoro wangu na wao uko kwa huko nyuma tulipotoka CCj tulikuwa na viongozi wa kitaifa matapeli ila yeye wakati huo alikuwa katibu mwenezi, alifanya kazi nzuri sana ila kuna uzembe mkubwa ulikuwepo awali, kama atakuwa na safu nzuri ya uongozi naamini baadaye chama chake baada ya Chadema kitafuatia. maana ccm,tlp,tadea,nccr,udp cuf aka KAFU na majina mengine yafananayo na hayo tutavisahau soon. ilmradi tu wasiwe ccmB. au wakawa wametumwa kuharibu, ila kama wako serious nina imani na Akitanda baada ya kukuta yupo. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Akitanda ni mtu makini sana iwapo ataungana na wapambanaji wenzake akina Willbrod Slaa,Mbowe,Lema ,Mdee,Mnyika,Kabwe, Ndessa na wengine kama hao ambao hupatikana Chadema.:welcome:
Tunakuja na mbinu mpya za siasa za kisasa, wanafiki mpaka wakimbie, hatuwezi kuendelea kuona nchi yetu kwa miaka mingi ikichezewa, tuache ushabiki tukalikomboe taifa
Mkuu wangu navyokusoma tayari nakuelewa huna tofauti kabisa ni kama viongozi waliopo ama waliopita ambao wanafikiria chama ni NGO au shirika. Na hata iwe hivyo, huwezi kuingia mahala kichwa kichwa kabla hujaweza kujitangaza na kupata support ya wananchi. Niulize mimi kama naweza kukupa kura yangu? jibu likakua hapana na sababu ni kwamba sielewi lolote kuhusiana na CCK zaidi ya katiba na sera zenu. Mkuu wangu unahitaji kuzaa WANACHAMA kwanza kabla ya mjumbe bungeni..
Hayo ya kupambana na rushwa,posho na kadhalika unayasema wewe hapa JF na hizi ni ahadi hewa tulozisikia kwa viongozi wote wakati wakigombea ubunge na tatizo ni kwamba haijafanywa sheria kwa chama kutekeleza sera zao kama walivyoainisha. Inatakiwa kwanza mtueleze kwa nini CCK ni tofauti na vyama vingine, kwa nini tuwaamini viongozi wenu maana usije nambie Lowassa au Rostam ndiye muasisi wa chama na mjumbe wa CC. Nini hasa madhumuni ya kuanzishwa kwa chama hiki na kwa kupigania haki za kina nani? maana neno wananchi wanyonge pekee haitoshi.. kuna vyama vya haki za binadamu na havigombei ubunge. Tumewaona wafanyabiashara wakubwa wakisema wanapigania haki ya wanyonge, kisiasa mkuu wangu hakuna kitu kama hiki.. Kina CHE, Castro na wengine wametoka ktk jamii za wanyonge na wanaelewa shida za wanyonge, hizi habari za matajiri kufungua vyama mkuu wangu ni biashara tu maana kama kweli wewe tajiri na unataka kusaidia wanyonge basi fungua hata NGO na kugombea Ubunge..Kusema kweli mnatuchezea tu akili zetu..
Kibaya kuliko yote mnaingia kwa kujificha ficha sielewi mnachoogopa. Mimi nataka kujua nani amekuja na wazo hili la CCK kisha tumpime kama yeye na waasisi wengine wote ni wapiganaji..Na amini maneno yangu hamuwezi kujiingiza ktk uchaguzi haraka kiasi hiki mkidhania kwamba ni uhshuda wa kuwaonyesha wananchi mnataka kuleta mabadiliko kupitia sanduku la kura, sanduku ambalo ni sehemu ya ufisadi uleule..Hapa nilipo mimi, binafsi yangu nashindwa hata kuelewa kwa nini Chadema na CUF vinaendelea kushiriki ktk chaguzi ambazo wanafahamu fika kwamba haki haitatumika au wananchi wenyewe wamepuuza hata kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa sababu wanajua haki yao ya kuchagua haitapokelewa..
Na kwa kila mnavyozidi kukumbatia mfumo mbovu kama huu ndivyo CCM inavyozidi kushinda kwa sababu wananchi wasiopiga kura wengi ni wale wasioipenda CCM maana CCM ina mpango wa kukusanya watu wake kwa lazima kupitia wajumbe wa nyumba 10 na kadhalika. Kwa mwana CCM kutopiga kura unachukuliwa kama msaliti hivyo kila mwananchama wa CCM kwa kadi au mapenzi husisitizwa hupiga kura kwa kupewa Khanga au Tshirt na mshiko kidogo wakati nyie mnategemea uzalendo wa WATU waliokwisha poteza Uzalendo kutokana na mfumo wa Msituni (Darwin). Sisi waislaam tuna hadithi ya Mtume inayosema Fukara yaani maskini wa mali ni sawa na Kafir..Umaskini ni mbaya na adui mkubwa wa maskini wenyewe, huyu ni mbaya kama fisi ambaye anaweza kula mwanaye au hata matumbo yake mwenyewe akisha jeruhiwa..
Usije sema nawakatisha tamaa lakini mtakuja nambia siku ya siku maana sisi wengine tumejaliwa kuyaona msoyaona, nisome vizuri..
Je tuwatofautishe vipi na chama kama tadea, TLP na nk yaaki mna lipi jipya....
Umetokea msikiti gani weye?
Mkuu wangu nadhani wewe unatazam picha hii ukiwa ndani ya chama chako na kufanya mzaha ktk swala ambalo linatumaliza Watanzania wengi. Hizi habari za CCM sio mama yangu naweza kuachana nayo ni hadithi za Buricheka maana walioweza kuondoka wameondoka, lakini kama bado umo ndani basi una maslahi yako maana hakuna sifa yoyote ambayo inaweza kumwekla mwanaharakati ndani ya CCM.. Utanisamehe mkuu wangu ktk hilo..Nadhani kuna hoja nzuri sana hapa ila zinahitaji ufafanuzi zaidi. Lakini muhimu zaidi haujatoa mapendekezo nini kifanyike kurekebisha mapungufu hayo. Je, unapo himiza umuhimu wa haki kwa wananchi, katika kipindi hiki cha maandalizi ya kupata katiba mpya yenye kutoa na kulinda haki hizo, vyama vya siasa vifanye nini, vikache uchaguzi ndogo kama za Arumeru na kujikita zaidi katika kujiandaa kutafuta haki chini ya katiba mpya? Sijakupata vizuri katika hili, ingawa nadhani naelewa unaelekea wapi. Kwa mtazamo wako, je vyama vya upinzani vifanye nini kati ya kipindi hiki na katiba mpya 2014/15?
Kuhusu CCK kushiriki uchaguzi wa Arumeru hata kama ni wageni katika siasa, ni muhimu tutambue kwamba, mbali ya CCK kuwa na haki sasa na CCM, Chadema, CUF, NCCR etc in that context kwa mujibu wa sheria chini ya msajili wa vyama vya siasa na tume ya uchaguzi, any publicity, no matter how bad, is good publicity.
MKuu wangu hata mimi sina mapenzi hayo isipokuwa nategemea kuona kitu cha Uhakika na sii ubabaishaji ule ule. Nahcojenga hapa ni kuwatakia kheri na kuwaelekeza mwanzo mzuri maana nilifanya hivi hivi wakati wa Chadema kinajipanga.. walinichukia vile vile wakidhani nawabeza..@mkandara
Embu Tuache wananchi tupate burudani na mawazo mapya na CCK..
Unajua Chadema tumeshaanza kuchoka na wengine hata mtufanyeje hatuwaamini tena chadema??
Mkuu wangu nadhani wewe unatazam picha hii ukiwa ndani ya chama chako na kufanya mzaha ktk swala ambalo linatumaliza Watanzania wengi. Hizi habari za CCM sio mama yangu naweza kuachana nayo ni hadithi za Buricheka maana walioweza kuondoka wameondoka, lakini kama bado umo ndani basi una maslahi yako maana hakuna sifa yoyote ambayo inaweza kumwekla mwanaharakati ndani ya CCM.. Utanisamehe mkuu wangu ktk hilo..
Halafu kama wewe mwanachama wa CCM huwezi kuyaona nayozungumza kwa picha ile ile zaidi ya klutumia hiyo katiba ambayo mnaipanga wenyewe bila kumhusisha mwananchi hadi pale mtakapo taka NYIE ahusishwe. Na nazungumza haya yote sii kwa sababu ni Mwana Chadema bali mwanaharakati ambaye naitafuta haki ya wananchi kupitia vyombo hivi, hivyo sitazami hiyo katiba kitu ambacho hakipo leo nielndelee kutegemea labda kesho itakuwa bora zaidi.
Wazee wetu walipopigania Uhuru walikuwa ahadi nyingi tu, wakaahidiwa kupelekwa Ulaya na kupewa elimu, nyumba utadhani shetani alojmjaribu Yesu, lakini haikuweza badilisha nia zao. Wazee wetu waliambiwa tena ya kwamba - Watanzania bado hatupo tayari kuwa Huru na wakoloni walituwekea sera za kila aina kutonyesha wao wana nia nzuri na sisi lakini wazee wetu wakikataa katu na kusema - Tupeni nchini yetu na tutajikongoja vivyo hivyo.. Ndivyo navyoitazama Tanzania ya leo hatuhitaji maamuzi ya CCM hata kidogo bali sisi wananchi ndio wa kuwaambia CCM tunataka nini..
Chadema na CUF hawana sababu kabisa ya kuendelea kugombea chaguzi ndogo kama hizi wakati kuna chaguzi nyingi za nyuma wamepigwa chini, sasa waendelee tu kushiriki wakisubiri katiba?..Na kuna ushahidi gani hiyo katiba itawaletea mwongozo bora ambao utawawezesha wao kushinda. Mkuu wangu kupitia chama chako HAIWEZEKANI kabisa Chadema au chama kingine chochote kushinda kupitia sanduku la kura ikiwa katiba hiyo itaandikwa na wana CCM - HAIWEZEKANI labda kitafutwe chombo cha kimataifa kuifanya kazi hiyo maana najua fika majibu yake. Nasema sioni sababu kabisa ya vyama vya Upinzani kuendelea kugombea uchaguzi mdogo wakati wanatakiwa kuandaa mazingira ya uchaguzi wa 2015..Bora hata hao madktari waliogoma wameonyesha watu waliopania kuipata haki yao wenyewe.
Unapozungumzia CCM na kuharibu vyama vya Upinzani hii ni kawaida yake wala hawana wasiwasi maana waliweza kukivuruga NCCR lakini watu mnafikiria kwamba ni chama hicho kilichokuwa na matatizo.. Wameweza pia kukivuruga CUF na sasa hivi wanaitafuta Chadema hii inajulikana wazi wala haina ubishi kwani ktk mbinu zake mojawapo na kubwa ilotumika sana ni kuvunja nguvu ya chama mbadala cha ushindani. Na kwa bahati mbaya hawa vijana wa CCK mnaowasifia wameingia msikitini na mguu wa shoto. Haraka ya nini uda bado upo sana kufikia 2015, onyesheni uanaharakati wenu kwanza mpate kusifiwa na wananchi.
Na pengine huelewi maana ya Bad publicity is Good Publicy ni kama tunavyomsema Lowassa au Zitto. Ni kaa uweke tangazo baya linalouddhi watu lakini watu huitana kulitazama ili kesho libakie kichwani mwao na pengine hata waende KUNUNUA.. haina maana nje ya hiyo kama wanavyotaka CCK kujtangaza kana kwamba chama ni chao WAO na wao ni kina So and SO, heee! imekuwa bendi ya kizaire?.
Chama ni WANACHAMA unakitangaza chama ili upate wanachama wengi na through them ndipo chama kinajinadi kirahisi kutokana na mvuto huo. Kwenda kugombea Ubunge Arumeru haina kujitangaza bali unaingia ktk mashindano bila wachezaji afadhali hata wangekuwa miguu peku lakini wamekamilika.
Mkuu wangu kwa dalili hii inatuonyesha wazi kwamba CCK haikujiandaa kuchukua NCHI bali inadandia majimbo hapa na pale wapate KULA.. mabadiliko huanza na kuonyesha kivitendo yale unayoyalaani.. Kujenga UANAHARAKATI na kuzivuta mioyo ya watu washiriki nawe ktk vita dhidi ya utawala au vitu unavyopigania hata iwe UFISADI..lakini kuingia uchaguzi huku umebeba bango la Itikadi na sera mkuu wangu hii nisawa kabisa na kujidanganywa wao wenyewe.
Hata hivyo nawatakia kila la kheri ingawaje najua fika wameanza vibaya na pengine ndio utakuwa fundisho kwa vijana wadogo wanakurupukia siasa bila kujianda na vita nje ya sanduku la kura.