Soma hapa nadhani umekosea tu ulitaka kusema Ubepari au sio? Lakini maadam unasisitiza kuwa ufisadi umetokana na Uliberali naomba somo hapo kidogo..
Maadam hapo awali nimeshakueleza kwamba uliberali una vitu vikuu vitatu ambavyo ni
Liberalization,
Marketisation na
Privatization, na pia nikaelezea kidogo uhusiano wa vitu hivi na ufisadi, nitajikita zaidi kwenye mifano kadhaa kuboresha hoja yangu kuhusu uhusiano baina ya ulibepari na ufisadi. Kabla sijaenda mbali, ni muhimu niseme kwamba, pamoja na umhimu wa vitu hivi katika Maendeleo ya uchumi, viongozi wetu wamechangia sana kufanya uwepo am ujio wa uliberali kuwa na madhara kuliko faida kwa wananchi walio wengi. Uliberali umekuwa ni chaka kubwa la viongozi wetu kujinufaisha binafsi kwa njia za ten percent na pia kuruhusu mikataba isiyokuwa na maslahi kwa watanzania walio wengi. Viongozi wetu walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuhakikisha uliberali unaleta faida kuliko hasara, hasa kwa kusimamia maslahi ya taifa wakati wa majadiliano/mashauriano mbalimbali na wawekezaji n.k.
Wakati tunapata uhuru (1961), mataifa makubwa yaliyotutawala walituambia kuwa sisi ni maskini kwa sababu tuna
ardhi, rasilimali na nguvu kazi, lakini hatuna
tekinolojia na
mtaji. Hivyo, ili tuendelee, tunahitaji mitaji na tekinolojia kutoka nje, na pia mikopo ili serikali yetu iweze kuendesha shughuli mbalimbali, hasa kilimo. Lakini lengo walitaka tuendelee kuzalish mazao kwa ajili yao. Mwalimu alifuata maagizao haya kwa kuwa hakuwa na jinsi, kwani taifa lilikuwa bado changa na liliwahitaji wakubwa hawa. Lakini baadae (1967), Mwalimu akaona bila ya sisi kujitambua kama taifa, tutabakia kuwa taifa tegemezi. Hivyo akaja na mkakati wa kujenga viwanda, ili visaidiane na kilimo kujenga uchumi. Wakubwa wan je hawakupenda hili. Lakini ilibidi wampe sifa Nyerere kwa kujenga viwanda vingi muhimu, hasa vya ngozi, food processing, nguo, na sekta ya mafuta (TPDC), kwa kutumia zaidi rasilimali za ndani (fedha za walipa kodi), kuliko misaada/mikopo kutoka nje.
Uchumi ulipotetereka miaka ya mwisho ya sabini-mwanzo ya themanini,
Mwalimu alichotaka toka kwa IMF ni bail out ili kuokoa viwanda vytetu na pia kilimo, bail out kama ile ya Ureno, Ugiriki, Marekani, n.k miaka ya sasa. Nyerere alijitahidi sana kujenga hoja kwamba tunachohitaji ni bail out,
lakini Mzee Mtei (mwasisi wa Chadema), ambae aliegemea upande wa IMF, akapingana na hoja hiyo. Badala yake, IMF wakaja na kauli mbiu ile ile ya wakati wa uhuru -
mna ardhi,
rasilimali, na
nguvu kazi lakini
hamna mitaji na tekinolojia, hivyo fungueni uchumi wenu ili mpate mambo haya. Na mbaya zaidi ni kwamba, hata nchi wahisani nao wakaegemea kwa IMF na kuanzia wakati ule mpaka sasa, hawatoi mkopo/misaada wowote bila ya IMF na WorldBank kutoa ruksa. Hivyo, ili kupata misaada ya nje, IMF na WorldBank wakatupa masharti kama vile serikali kuachana na viwanda, na badala yake, kurudi kwenye kilimo cha enzi ya mkoloni.
Uliberali umepelekea viwanda vyetu vingi kufa au kuuzwa, hata vile vilivyokuwa vinatengeneza faida kubwa, vinalipa kodi, vinatoa ajira kwa watanzania – vya nguo, ngozi, oil sector (TPDC), food processing n.k, tena hivi vikawa vya kwanza kuathirika.
Kuna makala moja ya profesa Shivji inaeleza kwa mfano kwamba, mashamba ya mikonge yaliuzwa kwa bei ya chini ya senti hamsini za dollar kwa heka moja katika miaka ya tisini! Leo, hii ni sawa na shillingi 750 za kitanzania kwa heka. Haya yote ni zao la uliberali. Badala ya uliberali kuleta faida kwa taifa, viongozi wameutumia kupata faida zao binafsi kupitia ten percent.
Bado serikali yetu, kupitia Tanzania Investment Centre inazidi kukumbatia ulibepari na masharti yake, ambayo yanachochea ufisadi na wizi wa mali za watanzania. TIC inaruhusu wawekezaji waje kutengeneza faida za haraka, tena kwa dhuluma, huku ubepari katika nchi yetu ukiendelea kuwa juu ya sheria za nchi. Wawekezaji hawa wanalenga zaidi rasilimali na ecology yetu ambayo bado ni ‘virgin', ambayo Nyerere alihimiza iachwe mpaka watanzania wenyewe watakapokuwa tayari kuitumia kwa faida yao wenyewe. Kwa mfano, chini ya ulinzi wa TIC, wawekezaji wanaingia kwenye sekta ya madini na kupewa umiliki wa asilimia mia moja na hawalipi kodi; wanapewa vibali vya kuiba ndege na wanyama wetu; wanapewa vibali vya kukata miti ovyo na kusafirisha magogo kwenda nje. Serikali haiweki mkazo kwa wawekezaji kwenda kuwekeza kwenye sekta muhimu kwa taifa, kama viwanda, ambavyo vingesaidia kutoa ajira kwa vijana na pia kuwapatia wakulima masoko - malighafi kama vile ngozi, mazao ya kilimo, n.k ambayo yangehitajika kwa ajili ya uzalishaji viwandani.
Mwekezaji anapata Baraka za TIC kwenda kupora ardhi kwa ndugu zetu wa kimaasai chini ya uwekezaji wa
‘ranch'. Anaweka ulinzi katika ardhi ile, na kutulia na bunduki zake kusubiria kuua watanzania watakapia eneo lile na mifugo yao, kwani watanzania hawa wanamvurugia shughuli yake ya kusubiria wanyama wetu wa porini wapite katika maeneo yale wakati wa misimu husika, kisha yeye na washirika wake kuwapiga risasi ovyo ovyo tu, kwa ajili ya kuwasafirisha nje kama nyama na ngozi.
Misituni nako, mbali ya kukata magogo na kupelekea nje kwa ridhaa ya serikali chini ya TIC, wawekezaji wanatumia nafasi hiyo pia to exploit bio diversity yetu - wanabeba ‘our exotic plants' na mbegu, halafu wanaenda kuzifanyia genetic engineering na kisha kuziwekea patent. Vizazi vyetu vya baadae vikija hitaji mbegu hizo, inabidi walipie patent, kwa mimea ambayo kwa asili ilikuwa ni mimea yao.
Pia suala la fedha chafu – tunashuhudia jinsi gani TIC inavyotoa vibali kwa makasino yanayoshamiri kila kona ya majiji yetu. Pia tunashuhudia jinsi gani maduka ya kubadilisha fedha za kigeni yanavyoshamiri katika miji yetu kupitia mlango wa kulegeza masharti ya biashara kwenye sekta ya fedha. Shughuli hizi ndio vichaka vikubwa vya ufisadi, ambapo majizi ya mali ya umma na pia wawekezaji majizi ambao hawalipi kodi ndio wanaowapa faida kubwa wamiliki hawa wa hizi kasino, faida ambazo nyingi hutoroshwa nje ya nchi.
Matatizo yote haya ni matokeo wa uliberali ambao umeachiwa na serikali ufanye utakavyo, na uishi juu ya sheria. Ubepari sasa upo juu ya sheria na umechafuliwa na ufiadi, na kupelekea watanzania wengi kuuchukia kwa makosa, kwani mafisadi ndio hujificha humo, huku serikali ikijikita zaidi kusafisha ufisadi badala ya kusafisha ubepari uliochafuliwa na ufisadi. Uliberali ni janga kubwa sana kwa taifa letu kiuchumi na kijamii, na vyama vyote vinavyo unga mkono uliberali ki-itikadi – CCM, Chadema, na CUF, vina wajibu mkubwa sana wa kuwaeleza wananchi kulikoni?