CCK yaingia Arusha kwa kishindo

tumeichoka CDM,issue ya katiba ndo ilonifanya nikate tamaa na hawa wafanyabiashara wa siasa wa CDM,kwenda ikulu wakahongwa na kurudi bungeni kupitisha madudu yale waloyapinga mwanzo???? nini hii?? afadhali CCK ije arusha

Think loud antie!umetoka lini jela?unakumbuka jina la hii nchi?hebu tuambie kipi walichopinga na wakakipitisha?haya nenda na usiongee uharo tena!!
 
CCK kama cha cha siasa wana haki ya kuweka mgombea Arumeru, wangekaa meza moja na Chadema waweke mgombea mmoja, kila mmoja akiingia kivyake watagawa kura na hatimaye CCM wanashinda.
an ordinary Ritz??there.is must be something wrong with my eyes!Ritz?
 
Baada ya kukamilisha safu ya uongozi wa mkoa wa Arusha,CCK inatangaza rasmi kuwa tunaingia katika uchaguzi mdogo wa Arumeru kwa ajili ya kuchukua jimbo.
SASA HAPA KISHINDO KIKO WAPI?
Tunaomba urudishe maswali haya kwa walokutuma.
*Ni lini wamefanya ziara ya kujitambulisha jimboni humo kama chama kipya cha siasa{vingine vyote vinafahamika jimboni tayari na vilikwisha shiriki chaguzi kadhaa jimboni humo}
*Kama lengo ni kuleta siasa safi kwa nini msionyeshe mfano kwa kutokimbilia madaraka kwa uchaguzi msiojiandaa,
*Wenzetu ruzuku mmepata wapi mapema namna hiyo ili kuweza endesha kampeni?
Tutaonana baadae,,,,,,,
 
Daaaah! CCK mbona mnaingia msikitini na mguu wa kushoto?..
Kwa mwananchi piga kura nisingetegemea kabisa kukiona chama hiki ktk kushiriki jambo lolote la uchaguzi mdogo isipokuwa kujiandaa ktk kukitangaza na kukiuza chama kwa wananchi.
Kitendo cha kuingia uchaguzi mara tu baada ya kusajiliwa inaonyesha wazi kwamba uongozi wa chama hiki haukujipanga kisiasa kuwakiisha wananchi bali ushabiki wa kuafuta ruzuku za serikali. Kwa maana hii wameingia msikitini na mguu wa kushoto, ibada zao zote zitakuwa batil na mtakuja nambia!...
 
Baada ya kukamilisha safu ya uongozi wa mkoa wa Arusha,CCK inatangaza rasmi kuwa tunaingia katika uchaguzi mdogo wa Arumeru kwa ajili ya kuchukua jimbo.

Ingieni kwa adabu la sivyo mtarudi kwenu! Hii ni Arusha kwa Mhesh Godbless Jonathan Lema! Njoni mkiwa wachafu mtarudi mkiwa safi na mmekwatuliwa fresh! Nastikitika tu kuwambia kua tayar tushafanya uchaguzi wa Mbunge, nae ni Mhesh Nassari, CDM ishamptisha, na raia wote washasema NDIYO apite!. Karibun m2salimie af mrudi kwenu!
Karibun sanaa!!
 
Hongereni CCK kukamilisha usajili. Wekeni mgombea Arumeru bila kujali siasa uchwara za watu wasiojua siasa wanaodhani kuwa vyama vyao tu ndio vyenye haki ya kuweka wagombea. Wanashindwa kuelewa kuwa CCK inakatiba yake na malengo yake. Wala haikuomba usajili ili isindikize chama fulani. Kazeni buti watanzania wengi hawajui siasa, wamekariri vyama fulani kwa maslahi fulani ama ukanda au udini. Ninaomba msaidie kutupa elimu ya uraia.
 
Daaaah! CCK mbona mnaingia msikitini na mguu wa kushoto?..
Kwa mwananchi piga kura nisingetegemea kabisa kukiona chama hiki ktk kushiriki jambo lolote la uchaguzi mdogo isipokuwa kujiandaa ktk kukitangaza na kukiuza chama kwa wananchi.
Kitendo cha kuingia uchaguzi mara tu baada ya kusajiliwa inaonyesha wazi kwamba uongozi wa chama hiki haukujipanga kisiasa kuwakiisha wananchi bali ushabiki wa kuafuta ruzuku za serikali. Kwa maana hii wameingia msikitini na mguu wa kushoto, ibada zao zote zitakuwa batil na mtakuja nambia!...

Ndiyo maana NEC wametuletea waraka juu ya ratiba ya uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru pamoja na kata nyingine nane za udiwani, tunakwenda kushiriki ili tusimamie maslahi ya jamii na si ruzuku, hatuiwazi hiyo brooo, tutaipinga na kuipinga! Ruzuku ndiyo chanzo cha vyama kubweteka! coome on!
 
Kazi ya kuendelea kukieneza chama inafanywa kwa kasi kubwa siyo lazima tuweke kwenye vichwa vya magazeti! Kikosi kazi kimesambaa kila kona ya nchi kujenga chama tena watu wanajitolea muda na mali zao! Weye unayesubiri ruzuku ndo uende kwenye uchaguzi endelea kusubiri!
 
Iike mahala watu tubadilike, hakuna chama chenye milki na jimbo la Arumeru, mojawapo ya njia ya kueneza chama ni kujitokeza kwenye fursa kama hizi za uchaguzi ili kunadi malengo na mwelekeo wa chama kwa Watanzania! Acheni woga tutapiga kazi Arumeru na tutawaduwaza
 
Hongereni CCK kukamilisha usajili. Wekeni mgombea Arumeru bila kujali siasa uchwara za watu wasiojua siasa wanaodhani kuwa vyama vyao tu ndio vyenye haki ya kuweka wagombea. Wanashindwa kuelewa kuwa CCK inakatiba yake na malengo yake. Wala haikuomba usajili ili isindikize chama fulani. Kazeni buti watanzania wengi hawajui siasa, wamekariri vyama fulani kwa maslahi fulani ama ukanda au udini. Ninaomba msaidie kutupa elimu ya uraia.

Safi Kamanda wangu, msijali mambo makubwa yanakuja! Kuanzia tarehe 1 Machi tunaanza mikutano ya hadhara kwenye kila mkoa Tanzania, bila kusahau Arumeru, macho na mioyo yetu tunaielekeza huko mpaka kieleweke!
 
Ndiyo maana NEC wametuletea waraka juu ya ratiba ya uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru pamoja na kata nyingine nane za udiwani, tunakwenda kushiriki ili tusimamie maslahi ya jamii na si ruzuku, hatuiwazi hiyo brooo, tutaipinga na kuipinga! Ruzuku ndiyo chanzo cha vyama kubweteka! coome on!
Mkuu wangu navyokusoma tayari nakuelewa huna tofauti kabisa ni kama viongozi waliopo ama waliopita ambao wanafikiria chama ni NGO au shirika. Na hata iwe hivyo, huwezi kuingia mahala kichwa kichwa kabla hujaweza kujitangaza na kupata support ya wananchi. Niulize mimi kama naweza kukupa kura yangu? jibu likakua hapana na sababu ni kwamba sielewi lolote kuhusiana na CCK zaidi ya katiba na sera zenu. Mkuu wangu unahitaji kuzaa WANACHAMA kwanza kabla ya mjumbe bungeni..

Hayo ya kupambana na rushwa,posho na kadhalika unayasema wewe hapa JF na hizi ni ahadi hewa tulozisikia kwa viongozi wote wakati wakigombea ubunge na tatizo ni kwamba haijafanywa sheria kwa chama kutekeleza sera zao kama walivyoainisha. Inatakiwa kwanza mtueleze kwa nini CCK ni tofauti na vyama vingine, kwa nini tuwaamini viongozi wenu maana usije nambie Lowassa au Rostam ndiye muasisi wa chama na mjumbe wa CC. Nini hasa madhumuni ya kuanzishwa kwa chama hiki na kwa kupigania haki za kina nani? maana neno wananchi wanyonge pekee haitoshi.. kuna vyama vya haki za binadamu na havigombei ubunge. Tumewaona wafanyabiashara wakubwa wakisema wanapigania haki ya wanyonge, kisiasa mkuu wangu hakuna kitu kama hiki.. Kina CHE, Castro na wengine wametoka ktk jamii za wanyonge na wanaelewa shida za wanyonge, hizi habari za matajiri kufungua vyama mkuu wangu ni biashara tu maana kama kweli wewe tajiri na unataka kusaidia wanyonge basi fungua hata NGO na kugombea Ubunge..Kusema kweli mnatuchezea tu akili zetu..

Kibaya kuliko yote mnaingia kwa kujificha ficha sielewi mnachoogopa. Mimi nataka kujua nani amekuja na wazo hili la CCK kisha tumpime kama yeye na waasisi wengine wote ni wapiganaji..Na amini maneno yangu hamuwezi kujiingiza ktk uchaguzi haraka kiasi hiki mkidhania kwamba ni uhshuda wa kuwaonyesha wananchi mnataka kuleta mabadiliko kupitia sanduku la kura, sanduku ambalo ni sehemu ya ufisadi uleule..Hapa nilipo mimi, binafsi yangu nashindwa hata kuelewa kwa nini Chadema na CUF vinaendelea kushiriki ktk chaguzi ambazo wanafahamu fika kwamba haki haitatumika au wananchi wenyewe wamepuuza hata kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa sababu wanajua haki yao ya kuchagua haitapokelewa..

Na kwa kila mnavyozidi kukumbatia mfumo mbovu kama huu ndivyo CCM inavyozidi kushinda kwa sababu wananchi wasiopiga kura wengi ni wale wasioipenda CCM maana CCM ina mpango wa kukusanya watu wake kwa lazima kupitia wajumbe wa nyumba 10 na kadhalika. Kwa mwana CCM kutopiga kura unachukuliwa kama msaliti hivyo kila mwananchama wa CCM kwa kadi au mapenzi husisitizwa hupiga kura kwa kupewa Khanga au Tshirt na mshiko kidogo wakati nyie mnategemea uzalendo wa WATU waliokwisha poteza Uzalendo kutokana na mfumo wa Msituni (Darwin). Sisi waislaam tuna hadithi ya Mtume inayosema Fukara yaani maskini wa mali ni sawa na Kafir..Umaskini ni mbaya na adui mkubwa wa maskini wenyewe, huyu ni mbaya kama fisi ambaye anaweza kula mwanaye au hata matumbo yake mwenyewe akisha jeruhiwa..

Usije sema nawakatisha tamaa lakini mtakuja nambia siku ya siku maana sisi wengine tumejaliwa kuyaona msoyaona, nisome vizuri..
 
nadhani ulikuwa mmoja wao!

Siyo mmoja wao nilikuwa mkubwa wao wee acha tu! yaliyonikuta usiombe, ni mizinga kwa kwenda mbele, kunibomu vijisenti na vocha, kunilalamikia wake zao wanalala nja hivyo nitume pesa Dar wajue watalalia msosi gani! ilimradi tu karaha na maneno mbofumbofu, si unaona niliwaambia wakinishambulia tu naweka mambo yao yote hapa wakanywea?
A%20S%20embarassed.gif
 
nadhani ulikuwa mmoja wao!

Mkubwa mwenzao lakini wa huku mkoani Arusha, nawachukia watu wanaojaribu kina cha maji kwa kidole! watu wanaojiingiza kwenye siasa kwa madhumuni ya tumbo kwanza kabla ya kuangalia maslahi ya Taifa. :A S-confused1:
 
Siyo mmoja wao nilikuwa mkubwa wao wee acha tu! yaliyonikuta usiombe, ni mizinga kwa kwenda mbele, kunibomu vijisenti na vocha, kunilalamikia wake zao wanalala nja hivyo nitume pesa Dar wajue watalalia msosi gani! ilimradi tu karaha na maneno mbofumbofu, si unaona niliwaambia wakinishambulia tu naweka mambo yao yote hapa wakanywea?
A%20S%20embarassed.gif

nadhani ungeweka,maana mie huspend majungu!
 
Ndg. Paul Mafie, Mimi ndiye Akitanda, nafahamu wewe ulikuwa Mwenyekiti wa Muda Mkoa wa Arusha, na kwa kweli nakuheshimu kwa maana nafahamu mchango wako mkubwa kwa CCJ ambayo ilifutwa. Hivi wewe huamini kama movement huwa zinarithiwa na kufanikiwa? Why not? Kumbuka Mawazo ya Kimapinduzi siko zote hayafi! Tuko front, tunasonga mbele brother!

Bwana Constantine Akitanda wewe nakufahamu toka mwanzo ni mtu makini sana ila wenzako walikuangusha na hukuangalia tulipoangukia,Kiyabo na wenzake wawajua vizuri na jinsi mlivyoniacha njia panda na mpaka sasa mkaja kimyakimya pasipo kukumbuka michango na maumivu tuliyoyapata tukiwa wote, je haimaanishi kuwa mtakuja kuwasahau wananchi wenu wakishawapitisha kama CUF walivyofanya kwa kuisahau damu ya wapemba baada ya kupata uongozi? ina maana kilichowaua wapemba wale wote na kuwafanya wakimbizi ni Maalim kuwa Makamu wa Rais? mimi ugomvi wangu uko hapo tu. na nakuomba nawe wasikukatishe tamaa kama mimi maana watakuwa wameizima taa muhimu sana, nakushauri ukiona wanakupotezea muda tafuta njia ya kweli. Wewe kama Akitanda nakuheshimu ila!!!! sina cha kusema maana hata mimi nilifikiri hata wewe umeshaacha siasa na kuwa mwanaharakati kama mimi.
 
Safi Kamanda wangu, msijali mambo makubwa yanakuja! Kuanzia tarehe 1 Machi tunaanza mikutano ya hadhara kwenye kila mkoa Tanzania, bila kusahau Arumeru, macho na mioyo yetu tunaielekeza huko mpaka kieleweke!
Mtaji wa chama ni WANACHAMA,huo ubunge ni mavuno baada ya kufanikisha..Hizi ni fikira za kuvuna wakati hujapanda kitu na kama mnafikiria kwenda Arumeru ndiko mtako panda mbegu basi mmekosea sana ni sawa na kupanda mbegu juu ya mwamba.
 
Hv mw/kiti wenu taifa Ni nani? Na inakuwaje mnajitapa kuchukua Arumeru ilhali hata Bendera yenu tu waTZ hawaijui na Kama wapo Ni wachache sana? C ndio NINYI mlotoka ccj? Baada ya kunyimwa usajili mkakimbilia kuanzisha cck? Vp, wenzenu Wana ruzuku NINYI Je? Kampeni mtaendeshaje maana Cku hizi bara bila helkopta hujashinda bado!! MTIHANI, KAZI MNAYO

Bwana mkubwa hawa watu kama kiongozi wao ni huyo Akitanda Constantine namfahamu sana na ni mtu makini sana labda kama kwa hizi siku chache kabadilika , nampenda ni kijana mpambanaji na mwadilifu sana, mgogoro wangu na wao uko kwa huko nyuma tulipotoka CCj tulikuwa na viongozi wa kitaifa matapeli ila yeye wakati huo alikuwa katibu mwenezi, alifanya kazi nzuri sana ila kuna uzembe mkubwa ulikuwepo awali, kama atakuwa na safu nzuri ya uongozi naamini baadaye chama chake baada ya Chadema kitafuatia. maana ccm,tlp,tadea,nccr,udp cuf aka KAFU na majina mengine yafananayo na hayo tutavisahau soon. ilmradi tu wasiwe ccmB. au wakawa wametumwa kuharibu, ila kama wako serious nina imani na Akitanda baada ya kukuta yupo. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Akitanda ni mtu makini sana iwapo ataungana na wapambanaji wenzake akina Willbrod Slaa,Mbowe,Lema ,Mdee,Mnyika,Kabwe, Ndessa na wengine kama hao ambao hupatikana Chadema.:welcome:
 
Back
Top Bottom