Ni hoja mbovu kama hizi ndizo nasikia baadhi ya watu wa Chadema wakijiandaa kuzitumia kumaliza chama kingine chochote ambacho kitaonekana tishio kwa safari yao ya kwenda Ikulu 2015. Wenye mikakati hii hawana ufahamu kwamba hoja hii inajenga kuliko kubomoa kwani kuna makundi makubwa tu ya wananchi wasio na tatizo na CCM, bali baadhi ya viongozi. Ndio maana leo hii viongozi walio safi ndani ya CCM wakihamia chadema, watapita kwa kishindo. Kwani hufahamu kwamba Mtei, Bob Makani, Mbowe, Slaa, at one point walikuwa wanachama wa CCM? Tujifunze Kujifunza.