Hawa wabunge wa CCM Mkuu wanadhani Watanzania ni vichaa kama wao, watu wanasikiliza wanachambua mbivu na mbichi!!!! Wabunge wa CCM wanashabikia bajeti ya kuwauwa watu wao wanachekelea na kutukana watetezi wa wanyonge, wangoje hukumu yao iko karibu wasidhani 2015 ni mbali saana!!!!! Huyo Mwigulu ni wa kufuatwa kwao Ilamba tuone kama atapona safari hii!!!!Nimesikiliza Bunge la budget kweli lugha zinazotumika mwisho wake naona nchi yetu inaelekea kubaya sana kwa mtu aliyesikiliza bunge na leo jioni utakubaliana na mimi kabisa kuwa maadili ndani ya waheshimiwa wa bunge imeisha na hawajui kama wananchi tunawasikiliza na sii hivyo tu hata nchi za nje wanasikiliza nini kinaendela ndani ya bunge letu. Swali kweli tutafika?
Heading ya thread imenistua kidogo, nilidhani kachafua hali ya hewa kweli.Aisee kumbe Mwigulu Nchemba hana akili kabisa. Anahitaji kupelekwa Mirembe CCM inakufa anaamua kutupa matope Bungeni kutukana upinzani waigizaji na vichaa na eti wana pepo mtaka vyeo.
Hasira zake nafikiri ni failure kule arumeru. Anataka kurudia yale ya Lusinde arumeru ama kweli CCM imekwisha. Ametupa bajeti ya Upinzani na kuiita rubbish
Huyo Mwigulu Mchemba, Mhe Komba ndio wenye akili kutetea badget kandamizi???? Badala kutukana kwa nini wasieleze hiyo mikopo wanayochukua wataifanyia nini, wanataka Watanzania tuwe watumwa wa mikopo kama Greece kwenye UROZONE???? Je kwa nini wasieleze matumizi ya serikali sijui safari, semina, posho vyote hivyo vinamsaidia vipi Mtanzania anayelalia mlo mmoja????Mwigulu na Lissu wanatia aibu sana.
Huyu Mhe Mwigulu majibu ya ARUMERU hayakumuiingia akilini, hajakaa kutafakali nini kilitokea, hao ndio wabunge wa CCM Mkuu!!!! Watu wameishafunguka na hasa linapokuja swala la maslahi yao, wanakandamizwa na mabajeti kandamizi wananyamaza ila majibu watayatoa kwenye sanduku la kura!!!!!Kuthibitisha ni jinsi gani hiki chama cha mafisadi kinazidi kufa, Wabunge wake wanadhani Watz na wale wale wa zama hizo!!!!
Wewe hujamuelwa Muheshimiwa hapo alikuwa anaelekeza jinsi budget ya serikali ilivyo tofauti ya upinzani usipotoshe umma wewe.