Bungeni: Mwigulu Nchemba achafua hali ya hewa!

Bungeni: Mwigulu Nchemba achafua hali ya hewa!

Kuna kitu CCM imemeza(epa-kagoda,radar,kuuza nyumba za viongozi,ubadhirifu wa rasilimali,impunity etc)hakishuki tumboni wala hakiwezi kutapikwa. Kukabwa huko ndiko kunakomfanya Mwigulu aropoke,nadhani hajaropoka kwa sababu ya hiyo bajeti ya upinzani tu,kuna sumu na makandokando mengi yamemjaa mwilini na akilini kama yalivyowajaa viongozi wengi wa CCM,ndio maana baada ya kusema alishangiliwa sana na kupongezwa na wenzake na hata mwenyekiti alipeta upande ule mwingine ulipotaka mwongozo. Hapo ndipo CCM inapokosea ikidhani kuwa hayo yanayoendelea bungeni sisi wananchi wa kawaida hatuyaoni. Kuna mambo CCM wamekosea,wayasahihishe na wala hawatahitaji kutokwa na misuli ya shingo na mapovu kama alivyofanya Mwigulu leo pale bungeni
 
Kuna utofauti mkubwa sana kati ya "season" na "time"
alafu hepukana na story za kusimuliwa.
 
Kuna utofauti mkubwa sana kati ya "season" na "time"
alafu hepukana na story za kusimuliwa. Au kama hujasimuliwa basi uongeze umakini...! Husije kuwa kama mbunge wa mbinga magharibi.
 
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!
Jamani eti Bungeni kuna wasomi!*

Nimemuangalia kiumbe aitwaye Mwigulu akibwabwaja. Pia nimemsikia Tundu akitumia neno 'silly.' Neno hili silly hutumika sana nchi za magharibi wakati wa uchaguzi kwamba ni silly moment. yeye kaamua kusema wakati wa bajeti ni silly time.

Ubaya mkubwa wa Lisu ilikuwa kuanza kushambulia moja kwa moja CCM badala ya kuishambulia bajeti ya hovyo iliyo bungeni ili angalau apate kuungwa mkono na baadhi ya wana CCM. Wapo wengi tu wasiyopenda ujinga kama huo ulioletwa bungeni.

Tatizo la Mwigulu naona hajapata exposure ya kutosha dunia hii. Hana mifano ya kweli, alichonacho ni theories za mambo aliyoyasoma darasani. Anadhani yanamsaidia kujadili bajeti bila fahamu kwamba shida ya mwanakijiji siyo supply-demand curve.

Hili ni tatizo linaloongezeka kwa watu wengi wenye viji-digrii vyao pale bungeni. wanajisahau na kuanza swaggers za taaluma zao wakidhani ndo umaarufu. Kwa mtu kama Mwigulu naona hakuzoea kushangiliwa maana aliposhangiliwa ndo kabisaaa! akaongeza manjonjo kama mcheza mdundiko. Nikimuangalia hana jipya zaidi ya theories za vitabuni na internet. Amejiita senior economist wa bank kuu. Mimi mara moja nika google jina lake kama limewahi kuchangia uelewa wowote wa uchumi dunia hii. Wapi! nimejisemea mwenyewe, rubbish Mwigulu

Ndo maana sasa wakaingia na akina Komba kwa kudhani kushangiliwa ndo kufanya vizuri.*

Mwigulu,*Komba, et al., nawaomba waache kusubiri kushangiliwa. Hakuwapi lolote katika jamii. Kuna watu bungeni wana taaluma ambazo wakizitumia hakuna hata atakayewaelewa.

MchunguZI, Ukiangalia mabunge ya nchi zilizoendelea wakati wa debate wanafanya exactly alichofanya Lissu. Jaribu kufuatilia Westiminster, Dodoma ni chini ya cha mtoto. Ila ninachoona hapa bado wabunge wengi hawajawa na 'ngozi ngumu' kisiasa, wanalialia kama watoto wadogo.

Kwa mfano kitendo cha Lukuvi kusimama na kusema Lissu anatumia lugha za kuudhi ni utoto mtupu, Lissu is using his skills of hammering down the opposite side, yeye Lukuvi anasema kaudhika? Yaani alitegemea Lissu amchezee mdundiko ili afurahi or what?

Na kuhusu Komba, interestingly, Komba amesema huwa anaangalia debates za mabunge ya nje akataja Uganda na Kenya. Hivi Komba anaelewa kiingereza kweli maana mabunge haya yanaendeshwa kwa kiingereza.

As for Mwigulu, nakubaliana na wewe Mwigulu anafikiri kama yuko kwenye chumba cha mtahani. He makes no sense whatsever na comments zake za ki-first class! Kwa usanii wake wa ki-first class ameweza kupata figure mpya ya percentage ya misaada ya wafadhili kwenye budget yetu - anasema ni asimilia 6! Now put that "silly" theory of his into practice, tunakusanya kiasi gani, tunakopa kiasi na gap inayobaki kweli ni only 6%?
 
Last edited by a moderator:
Kuna utofauti mkubwa sana kati ya "season" na "time"
alafu hepukana na story za kusimuliwa.

Sasa wewe neno season umelitoa wapi? hiyo tofauti unaitaka ya nini?Au unarekebisha jambo gani. huhitaji kuwa intelligent, unachohitaji ni kuwa mwanafunzi mzuri.

Tulia changia, tusaidiane kujenga hoja. Usinyanyuke kama Mwigulu.
 
then kila mbunge anataka asikike na aonekane na apate coverage(kesho gazeti la uhuru na tanzania daima) unadhan yataongelea nini????unadhan HEADING ZITAKUWAJE????
Bunge ndo linatakiwa liwe hivyo. Sidhani kama kuna hata mbunge aliyesinzia. Tusubiri tu kuona hatima yake maana hiyo bajeti ni kwa mishahara yao minono huku tulio wengi tunataabika
 
Sasa wewe neno season umelitoa wapi? hiyo tofauti unaitaka ya nini?Au unarekebisha jambo gani. huhitaji kuwa intelligent, unachohitaji ni kuwa mwanafunzi mzuri.

Tulia changia, tusaidiane kujenga hoja. Usinyanyuke kama Mwigulu.

Naomba msiendelee kulitaja jina la mwigulu. Nemeisha kutapika kiasi cha kutosha. As for Honourable Tindu Lissu speech, i say Alutta continua. Saa ya ukombozi in karibia
 
MchunguZI, Ukiangalia mabunge ya nchi zilizoendelea wakati wa debate wanafanya exactly alichofanya Lissu. Jaribu kufuatilia Westiminster, Dodoma ni chini ya cha mtoto. Ila ninachoona hapa bado wabunge wengi hawajawa na 'ngozi ngumu' kisiasa, wanalialia kama watoto wadogo.

Kwa mfano kitendo cha Lukuvi kusimama na kusema Lissu anatumia lugha za kuudhi ni utoto mtupu, Lissu is using his skills of hammering down the opposite side, yeye Lukuvi anasema kaudhika? Yaani alitegemea Lissu amchezee mdundiko ili afurahi or what?

Na kuhusu Komba, interestingly, Komba amesema huwa anaangalia debates za mabunge ya nje akataja Uganda na Kenya. Hivi Komba anaelewa kiingereza kweli maana mabunge haya yanaendeshwa kwa kiingereza.

As for Mwigulu, nakubaliana na wewe Mwigulu anafikiri kama yuko kwenye chumba cha mtahani. He makes no sense whatsever na comments zake za ki-first class! Kwa usanii wake wa ki-first class ameweza kupata figure mpya ya percentage ya misaada ya wafadhili kwenye budget yetu - anasema ni asimilia 6! Now put that "silly" theory of his into practice, tunakusanya kiasi gani, tunakopa kiasi na gap inayobaki kweli ni only 6%?

Kweli Lisu hakuwa na makosa ktk hali ya kawaida ya bunge la kawaida. amejisahau kwamba wamo akina Komba na Mwigulu. wamo na viti maalumu ambao wao hata kma hawatachangia lolote kwa miaka mitano lakini hupiga mkofi na vigelegele Mwigulu akitupa bajeti ya upinzani.

Tatizo la hapo Dodoma ni uelewa mdogo. Kuna umoja wa chama kiasi kwamba baadhi husikiliza neno CCM ni kupiga makofi, basi!

Hilo la Lukuvi, you are very right! *Watu kama huyu Lukuvi ktk sinema hupewa nafasi za hovyohovyo. Wanaweza kuwa wanaiba chupi ktk kamba au kutumia mswaki wa mwingine, nk. Lakini nadhani pia kuna tatizo la hiyo kanuni ya maudhi. Iko subjective. Bora hata neno lugha ya matusi, neno lugha ya maudhi haieleweki. Mwingine hata akiambiwa CCM kwake ni maudhi.

Mpaka wa maudhi haueleweki.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Kweli Lisu hakuwa na makosa ktk hali ya kawaida ya bunge la kawaida. amejisahau kwamba wamo akina Komba na Mwigulu. wamo na viti maalumu ambao wao hata kma hawatachangia lolote kwa miaka mitano lakini hupiga mkofi na vigelegele Mwigulu akitupa bajeti ya upinzani.

Tatizo la hapo Dodoma ni uelewa mdogo. Kuna umoja wa chama kiasi kwamba baadhi husikiliza neno CCM ni kupiga makofi, basi!

Hilo la Lukuvi, you are very right! *Watu kama huyu Lukuvi ktk sinema hupewa nafasi za hovyohovyo. Wanaweza kuwa wanaiba chupi ktk kamba au kutumia mswaki wa mwingine, nk. Lakini nadhani pia kuna tatizo la hiyo kanuni ya maudhi. Iko subjective. Bora hata neno lugha ya matusi, neno lugha ya maudhi haieleweki. Mwingine hata akiambiwa CCM kwake ni maudhi.

Mpaka wa maudhi haueleweki.

Hili la maudhi ni mfano wa masalia ya mfumo wa chama kimoja. Hata sasa, CCM inaendeshwa kwa mfumo wa 'zidumu fikra za mwenyekiti'! Na matokeo ya huo mfumo ni uwoga wa ajabu. Sasa hivi mbunge wa CCM akiwa na hoja inayokinzana na serikali anamuomba mtu toka upinzani ili aiseme 'kwa niaba yake'. Utatetea vipi wapiga kura wako kwa mtindo huo wa lift ya kuwasilisha kero?

Ndani ya jengo wanapiga makofi, lakini wakija huku mtaani wanalalamika vibaya sana! Tutafika kweli? Sasa leo Lissu kafunua pazia, haiwezakani miaka nenda miaka rudi wabunge wanapitisha budget lakini wizara nyingi hazipati hela zilizopitishwa? Wizara ya science & Technology mwaka 2011/12 wamepata just 17% ya development budget iliyopitishwa na bunge! Sasa leo wanataka kupitisha budget gani?

Then anatoka mtu kama Mwigulu na kusema OC zinatumika kwenye mambo kama kulipia tume ya katiba mpya, fidia za watu wanaohamishwa! Hivi kweli mtu aliyeenda shule anaweza kusema mambo ya hovyo namna hiyo? Nini maana ya budget kama areas za matumizi zimefunikwa chini ya OC?
 
nimeshindwa kushangaa wakat mwigulu akitoa pumba zake wazir mpya wa madin ambae namjua kwa msimamo alikuwa anapiga makofi kwa style ya umagamba ushabiki usio na tija sidhan kama nimeona sahihi maana huwa namuamin sana muhongo . siamin kumpigia makofi pumba za mwigulu na tena kwa mikon miwil umisaidie kama nimeona vibaya
 
mwigulu tulikuwa nae chuo pale mlimani alikuwa anajiita chief nadhani ni jina alilotoka nalo Mkwawa lakini alikuwa anaonekana dhahiri ni mtu alietoka familia maskini wa kutupa, sa nikiskia hayo makelele yake nakumbuka ule msemo unaosema maskini akipata ...... hulia mbwata.Hiyo mnayoisikia ni mbwataaa
 
eti KIONGOZI WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI KUB amerudisha gari kwa mbwembwe na full media.......ila wakati anachukua lingine kali zaidi pro-chadema media kimyaa?
hoja hujibiwa kwa hoja
 
Huyu jamaa anajiita eti msomi wa uchumi daraja la kwanza. Nasubiri waliosoma naye watamchambua vipi.

Hivi angelikuwa mchumi kama Prof. Lipumba (na yeye mpinzani, SIJUI KASOMEA WAPI?) angelituambiaje?

Nilikuwa nafikiri kwa CCM ni Lusinde tu ndiyo Mropokaji kutoka Mirembe aahhh, Dodoma.

Ila kumbe Singida nayo si mbali sana na Mirembe ahhh Dodoma. Nafikiri hii itaingia kwenye historia.

Tundu Lissu kama Mwana Sheria aliyebobea, amewaTEKENYA kidogo tu akina Mwigulu na huyu jamaa na usomi wake, bila kujua mitego ya Wana Sheria, kauvaa mkenge na kuanza kuropoka kama jamaa yake Lusinde.

Mwigulu, wewe rudi tu BoT na haya mambo ya Siasa, waachie wenyewe maana huyawezi. Huyu jamaa hadi anatia hutuma na kaishia tu kuambiwa afute kauli zake. Mwenzie Tundu Lissu kaweka vitu watu kimya. Kamwaga radhi kwa kuliponda Bunge (pamoja na yeye mwenyewe), CCM, Serikali na viongozi wote kwa ujumla.

How can you brag openly that you are the first class economist in a third world country, and this country has one of the poorest economies in the world.....Daaah!!
 
Am ashamed of the gvmnt, maana me siku zote najiuliza hivi ni kweli wana ssm hawaoni serikali inavyokwenda kuwanyima kura 2015, maana maisha ya watanzania kwa bajeti hii yanazidi kuwa mabaya, kama wafanyakazi wa serikali ndio wanumia zaidi, sitaki kuamini kwamba kweli wabunge wa ssm hawalioni hili. Waombe watanzania waendelee kuruhusu kuibiwa kura ndio watashinda vinginevyo watatafuta pakuishi.
 
Bunge kama letu linapaswa liwe ivi ili serikali isilale,watanzania tumenyonywa vya kutosha,lakni kuna kitu sikielewi kwa wabunge wa ccm,anasema naunga mkono burget mia kwa mia hapo hapo anasema jimbon kwake kuna matatizo kibao serikal haijatatua,kweli uyu ni mzima au mwe..h
 
Mungu ataionjesha muujiza hi chama yenu. John Damien Komba ndo mbunge wa kule alipozaliwa mamangu nasikitika sababu nimepata hasara hata alipozaliwa babaangu ku Lucy nkya.
 
mimi nimeshangaa sisi wananchi tunataka kusikia wabunge zetu watatusaidia vipi katika maisha yetu ya kawaida wao wanaanza kupiga kampeni na kutukanana bungeni...leo hii nyerere angekua hai akaona mambo yanayofanyika bungeni saivi sijui angesemaje
 
tatizo ni kwamba hii serikali ilishazoea miaka yote hii inatayarisha bajeti alafu wabunge wao wa ccm kwa kua walikua wako wengi bungeni walikua wanaipitisha hata kama wapinzani wakiipinga ilikua bado inapita. sasa hivi mambo yamebadilika. wabunge wa chama chao wenyewe wanaipinga hii bajeti ndo maana wanatafutana
 
Ni nini maana ya wabunge CCM kutupigia kelele kwamba hawaungi hoja mkono, Lakini mwisho wa yote budget hiyo hiyo wanayoikataa sasa wataipitisha baadae kwa kelele zao nyingi za Ndiyooooooooooooo????????????????
 
yani komba ametia aibu ya mwaka kwa kujambamaputo yani anasifia bajeti wakati huohuo anaropoka kule jimboni kwake kuna dhiki eti watu wanavua kizamani mara samaki wanafaidiwa sana na wamalawi sisi hatuna uvuvi wa kisasa mara tumesha waneemesha wa kaskazin sasa zamu yetu huyu ni mjinga wa akili madaktari wa milembe waende wakamsedet kwa nguvu kabla ajaanza kuvua nguo. Ameniudhi sana kule nyasa watu hadi mafuta ya taa wanatumia ya malawi viberiti,sukari, serikali yake imelala tu aijitambui.
 
Back
Top Bottom