Bundi analia juu ya mpapai wangu

Bundi analia juu ya mpapai wangu

Huku napoishi, wanakuja ndege wa kila aina, wanalia kwa sauti za kila aina, mpaka bundi, mie naona ufahari tu, maana mpaka wakutembelee ina maana boma lako lina maua, miti, vivuli na utulivu na amani...
Achana naye, mpotezee tu, achana na dhana potofu, kwanza mrekeodi kabisa ili uturingishie 🙂🙂🙂
 
Hebu ngoja nitaweka ufafanuzi juu ya huyu kiumbe
 
Jamani uoga ni asili ya binadamu. Utafiti unaonesha kila binadamu ambaye hajafa ni muoga.

Hapa kwangu yamenikuta, Kuna bundi kavamia, yupo juu ya mpapai analia kwa sauti kama vile anatumia kipaza sauti. Nimemuuliza jirani yangu kwa simu kama hampigii kelele ikiwezekana akamfukuze lakini hajanijibu, nahisi anaogopa. Nimejaribu kuwasiliana na mwenyekiti wa serikali ya mtaa amesema nipambane na hali yangu.

Kuna mwanajeshi anakaa mtaa wa pili kanishauri nimpotezee ikiwezekana niweke head phone ili nisimsikie. Naombeni ushauri
Anatafuta chakula huyo , na chakula kikuu cha bundi ni panya. Aidha wewe au jirani yako mnafuga panya. Endesheni operation tokomeza panya mkuu!
 
Kwa hiyo una maana jirani yangu atakufa. Maana mpapai upo karibu zaidi na nyumba yake japo ni wa kwangu.
Ahahaaaa...

Unajitahidi kuhamisha goli....jiulize tu. Mwenye mamlaka na huo mpapai ndy anaehusika na huyo ujumbe wa bundi....
 
Ukiwa na imani na haya mambo, lazima ujiumize mwenyewe. Huyo hana tofauti na kunguru au njiwa, ni kwamba Mungu kamuumba awe bize usiku.
Jamani uoga ni asili ya binadamu. Utafiti unaonesha kila binadamu ambaye hajafa ni muoga.

Hapa kwangu yamenikuta, Kuna bundi kavamia, yupo juu ya mpapai analia kwa sauti kama vile anatumia kipaza sauti. Nimemuuliza jirani yangu kwa simu kama hampigii kelele ikiwezekana akamfukuze lakini hajanijibu, nahisi anaogopa. Nimejaribu kuwasiliana na mwenyekiti wa serikali ya mtaa amesema nipambane na hali yangu.

Kuna mwanajeshi anakaa mtaa wa pili kanishauri nimpotezee ikiwezekana niweke head phone ili nisimsikie. Naombeni ushauri
 
Usiogope bundi.Kipindi fulani nilikuwa kama wewe.Nikisikia bundi tu amani inatoweka.Hii ilitokana na malezi/mapokeo kwamba bundi akilia anaashiria bahati mbaya/mkosi/kifo.Siku moja nikasikia radioni nadhani ilikuwa RFA,katika kipindi cha Je, wajua?Kwamba huko Misri bundi akilia anaashiria bahati njema.Kuanzia hapo nikajua kuwa mlio wa bundi unatafsiriwa tofauti kulingana na mila na desturi za jamii husika.So, relax.After all,bundi ni ndege tu kama ndege wengine.Lazima alie.
Sema tu biologically yeye yuko tofauti na ndege hawa wa kawaida ambao wako active mchana.Yeye yuko active usiku(nocturnal)
 
Jamani uoga ni asili ya binadamu. Utafiti unaonesha kila binadamu ambaye hajafa ni muoga.

Hapa kwangu yamenikuta, Kuna bundi kavamia, yupo juu ya mpapai analia kwa sauti kama vile anatumia kipaza sauti. Nimemuuliza jirani yangu kwa simu kama hampigii kelele ikiwezekana akamfukuze lakini hajanijibu, nahisi anaogopa. Nimejaribu kuwasiliana na mwenyekiti wa serikali ya mtaa amesema nipambane na hali yangu.

Kuna mwanajeshi anakaa mtaa wa pili kanishauri nimpotezee ikiwezekana niweke head phone ili nisimsikie. Naombeni ushauri
Ana njaa huyo wee umetoa papai zote wee unafikiri atakula nini kaamua kukulilia
 
Huyo ni ndege kama ndege wengine acha uoga
 
Jamani uoga ni asili ya binadamu. Utafiti unaonesha kila binadamu ambaye hajafa ni muoga.

Hapa kwangu yamenikuta, Kuna bundi kavamia, yupo juu ya mpapai analia kwa sauti kama vile anatumia kipaza sauti. Nimemuuliza jirani yangu kwa simu kama hampigii kelele ikiwezekana akamfukuze lakini hajanijibu, nahisi anaogopa. Nimejaribu kuwasiliana na mwenyekiti wa serikali ya mtaa amesema nipambane na hali yangu.

Kuna mwanajeshi anakaa mtaa wa pili kanishauri nimpotezee ikiwezekana niweke head phone ili nisimsikie. Naombeni ushauri
Kemea!
 
Jamani uoga ni asili ya binadamu. Utafiti unaonesha kila binadamu ambaye hajafa ni muoga.

Hapa kwangu yamenikuta, Kuna bundi kavamia, yupo juu ya mpapai analia kwa sauti kama vile anatumia kipaza sauti. Nimemuuliza jirani yangu kwa simu kama hampigii kelele ikiwezekana akamfukuze lakini hajanijibu, nahisi anaogopa. Nimejaribu kuwasiliana na mwenyekiti wa serikali ya mtaa amesema nipambane na hali yangu.

Kuna mwanajeshi anakaa mtaa wa pili kanishauri nimpotezee ikiwezekana niweke head phone ili nisimsikie. Naombeni ushauri

KUMBE ni BUNDI.. ngoja nikuulize swali.. UNAIJUA kazi ya MANATI??
 
Wengine wanamtumia bundi kama ndege wa kumfuga ndani kama vile njiwa au kasuku...

Hana tatizo hana madhara... kua na amani...

Wakumuogopa ni binadamu kama huyo aliyekuambia pambana na hali yako...


Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom