Jamani uoga ni asili ya binadamu. Utafiti unaonesha kila binadamu ambaye hajafa ni muoga.
Hapa kwangu yamenikuta, Kuna bundi kavamia, yupo juu ya mpapai analia kwa sauti kama vile anatumia kipaza sauti. Nimemuuliza jirani yangu kwa simu kama hampigii kelele ikiwezekana akamfukuze lakini hajanijibu, nahisi anaogopa. Nimejaribu kuwasiliana na mwenyekiti wa serikali ya mtaa amesema nipambane na hali yangu.
Kuna mwanajeshi anakaa mtaa wa pili kanishauri nimpotezee ikiwezekana niweke head phone ili nisimsikie. Naombeni ushauri