Short tale..
Alisoma shule za seminari kuanzia kidato cha 1 mpk cha 4. Akapata mfadhili wa kumsomesha kidato cha 5&6. Akafaulu vizuri. Akapata scholarship nchi za nje. Akaweza kupata bsc. na masters. Alikua kijana mwenye haiba nzuri, mwerevu, mpole na mcha Mungu. Kiongozi flani (kwa sasa he is late) akaunyaka wasifu wake. Akamrudisha nchini na kumpa kitengo katika balozi za nchi zilizoko kusini.
Alivyoingia pale, wahafidhina wakamuona ni tishio. Aliendelea kumcha Mungu. Behind the scene kuna njama zikasukwa. Akapewa kesi ya human trafficking. Mpk kuja kuprove sio kweli, miaka imepita shwaa. Hakuweza kupata ajira tena. His character was assasinated. Akarudi mbwinde kuishi. Akaamua kulima zake mahindi madongoni. His career slapped him hard.
10 years later:
Paroko mmoja katika shirika la white fathers anatembelea mbwinde. Akasikia story yake. Ashukuriwe Mungu kuna mchongo wa maana na huyu victim ni fit candidate. Akatafutwa, fanyiwa counselling, pigishwa interview, akafaulu. Sasa aanze kujiandaa kwenda kureport nchi za mbali....guess what.......
Akapata ajali ya bodaboda, akiwa na passport yake mkononi. He is no more!!😞😞
Kuna msemo unasema keep your friends close and your enemies closer. Naona hapa ulibackfire kinoma....
MUNGU atutetee katika sehemu zetu za kujipatia kipato. Kuna vita sana ktk kuupata mkate wa kila siku..
Neema ya Kristo ikae nawe...