Habari wanaJF, Kwanza kabisa tukubaliane kwa Nchi yetu imekuwa shida sana kupata Takwimu za afya ,ni ngumu kujua watu wangapi wanazaliwa kwa siku , wanaofariki kwa siku , ni wastani wa watu wangapi wanapata ujauzito kwa Siku .
Hivyo kwa Uzoefu wangu nitakuja na Takwimu ambazo zitareflect kidogo hali halisi ya Afya katika nchi yetu .
Tanzania kwa sasa inakadiliwa kuwa na watu Milioni 60 ,wengi wao wakiwa wanawake hivyo tuchukue ni Milioni 32 .Ambapo kati ya hawa wanawake ambao wako katika umri wa Kuzaa yaani miaka 15-49 ni asilimia 20-25, hivyo tutachua ni milioni 8 .
Tunapozungumzia suala la BIMA kwa watu wote tunamaanisha kila mtanzania awe na uwezo wa kupata matibabu sahihi na wakati sahihi bila kuwa pesa taslimu mfukoni -malipo baada ya Matumizi .
Hali ilivyo sasa ni kwamba watanzania kama asilimia 15 tu wana bima za afya ,lakini kwa wagonjwa wanaofika hospitali nyingi asilimia 85 ni watumiaji wa Bima mbali mbali ,Asimilia 15 ni wanaolipa .
Hivyo kuna watu wengi huishia maduka ya Madawa na tiba asilia .
Kwa wastani Mtu mmoja hutumia shilingi Elfu 40-45 akienda kupata matibabu hospitali yenye hadhi ya Mkoa kwa Mara moja Gharama kati ya asilimia 20-25 ni pesa ya kumuona daktari nyingine ni dawa ,vipimo na gharama za upasuaji, hivyo kama kila mwezi watakwenda watanzania hospitalini kutibiwa na wengiwe wakafanyiwa upasuaji watu milioni 15 kati ya hizo 60 ni kwamba tutalazima kuwa na 15M x 40000 ambazo kwa haraka ni sawa na Bilioni 600 pesa ambazo ni Nyingi Sana .
Lakini hata kama tutatoa pesa za kuwaona Madaktari zikitolewa kwa wastani mgonjwa mmoja atagharamia elfu 30 mpaka 40 ambayo bado itakuwa ni zaidi ya bilioni 450 kwa mwezi kama watu milioni 15 watatibiwa .
Hivyo basi hili suala la Bima ya Afya kwa watu wote sio la kukurupukia inabidi kujipanga sana .
Kwa Utangulizi Huo napendekeza tuanze wamama Wajawazito wote ,yaani toka Mama akitambulika kuwa Mjamzito tu mpaka huduma za Kujifungua ziwe Bure .
Kwa kifupi uwekwe utaaratibu kliniki kina mama wanapewa kadi ambayo itaruhusu yeye kutibiwa popote pale mpaka ajifungue .
Tuanze na kundi hili sababu :-
1. Linamgusa moja kwa moja mama mwenyewe ,Baba na mtoto wote kwa Ujumla,hivyo kwa kumsaidia unasaidia unasaidia Jamii kwa Ujumla .
2. Ni wahanga wakubwa wa matatizo yatokanayo na Uzazi ukiachana na Mwanaume na mtoto
3.Kwa Idadi sio kubwa hivyo itakuwa rahisi kupata hizo pesa .
Tutapataje Pesa hizo ,Hapa tuachane Misaada ya watu wa Marekani hivyo kuna vyanzo viwili vikuu .
1. Ni mapato ya serikali kupitia Bajeti
2. Ni mapato ya serikali kupitia Tozo itakayo shughulika na Matibabu ya kina mama wajawazito Tu
Mfano :-Tuna laini za simu za mkononi zaidi ya millioni 50 ,Voda na Airtel wana jumla ya milioni 29 huku Tigo na Zantel 20 milioni na mitandao iliyobaki mitatu ina kamilisha .
Watanzania ni waelewa sana tukipata katika laini hizo 25 milioni tu zikawa active na wakaweza lipia 1000-1500 kwa Mwezi tutatengeneza bilioni 25 mpaka 37.5 bilioni ambazo kwa kina mama wajawazito tu zitawatosha kuokoa maisha yao .
Karibu wana JF tujadili suala nyeti la Afya kwa Wote .
Hivyo kwa Uzoefu wangu nitakuja na Takwimu ambazo zitareflect kidogo hali halisi ya Afya katika nchi yetu .
Tanzania kwa sasa inakadiliwa kuwa na watu Milioni 60 ,wengi wao wakiwa wanawake hivyo tuchukue ni Milioni 32 .Ambapo kati ya hawa wanawake ambao wako katika umri wa Kuzaa yaani miaka 15-49 ni asilimia 20-25, hivyo tutachua ni milioni 8 .
Tunapozungumzia suala la BIMA kwa watu wote tunamaanisha kila mtanzania awe na uwezo wa kupata matibabu sahihi na wakati sahihi bila kuwa pesa taslimu mfukoni -malipo baada ya Matumizi .
Hali ilivyo sasa ni kwamba watanzania kama asilimia 15 tu wana bima za afya ,lakini kwa wagonjwa wanaofika hospitali nyingi asilimia 85 ni watumiaji wa Bima mbali mbali ,Asimilia 15 ni wanaolipa .
Hivyo kuna watu wengi huishia maduka ya Madawa na tiba asilia .
Kwa wastani Mtu mmoja hutumia shilingi Elfu 40-45 akienda kupata matibabu hospitali yenye hadhi ya Mkoa kwa Mara moja Gharama kati ya asilimia 20-25 ni pesa ya kumuona daktari nyingine ni dawa ,vipimo na gharama za upasuaji, hivyo kama kila mwezi watakwenda watanzania hospitalini kutibiwa na wengiwe wakafanyiwa upasuaji watu milioni 15 kati ya hizo 60 ni kwamba tutalazima kuwa na 15M x 40000 ambazo kwa haraka ni sawa na Bilioni 600 pesa ambazo ni Nyingi Sana .
Lakini hata kama tutatoa pesa za kuwaona Madaktari zikitolewa kwa wastani mgonjwa mmoja atagharamia elfu 30 mpaka 40 ambayo bado itakuwa ni zaidi ya bilioni 450 kwa mwezi kama watu milioni 15 watatibiwa .
Hivyo basi hili suala la Bima ya Afya kwa watu wote sio la kukurupukia inabidi kujipanga sana .
Kwa Utangulizi Huo napendekeza tuanze wamama Wajawazito wote ,yaani toka Mama akitambulika kuwa Mjamzito tu mpaka huduma za Kujifungua ziwe Bure .
Kwa kifupi uwekwe utaaratibu kliniki kina mama wanapewa kadi ambayo itaruhusu yeye kutibiwa popote pale mpaka ajifungue .
Tuanze na kundi hili sababu :-
1. Linamgusa moja kwa moja mama mwenyewe ,Baba na mtoto wote kwa Ujumla,hivyo kwa kumsaidia unasaidia unasaidia Jamii kwa Ujumla .
2. Ni wahanga wakubwa wa matatizo yatokanayo na Uzazi ukiachana na Mwanaume na mtoto
3.Kwa Idadi sio kubwa hivyo itakuwa rahisi kupata hizo pesa .
Tutapataje Pesa hizo ,Hapa tuachane Misaada ya watu wa Marekani hivyo kuna vyanzo viwili vikuu .
1. Ni mapato ya serikali kupitia Bajeti
2. Ni mapato ya serikali kupitia Tozo itakayo shughulika na Matibabu ya kina mama wajawazito Tu
Mfano :-Tuna laini za simu za mkononi zaidi ya millioni 50 ,Voda na Airtel wana jumla ya milioni 29 huku Tigo na Zantel 20 milioni na mitandao iliyobaki mitatu ina kamilisha .
Watanzania ni waelewa sana tukipata katika laini hizo 25 milioni tu zikawa active na wakaweza lipia 1000-1500 kwa Mwezi tutatengeneza bilioni 25 mpaka 37.5 bilioni ambazo kwa kina mama wajawazito tu zitawatosha kuokoa maisha yao .
Karibu wana JF tujadili suala nyeti la Afya kwa Wote .