Kwa mwendo huu, Bima ya Afya kwa wote itakwama

johnmashilatu

JF-Expert Member
Sep 16, 2010
718
703
Habari wana Bodi,

Ninachokishuhudia katika mwenendo wa watendaji pamoja na hali ya sasa ya mfuko wa Bima yà Afya, inakatishà tamaa yà kwanini mfuko huu unawafanyia hivi wateja wake?

Kabla sijaendelea naomba niweke jambo moja sawa.. watumishi wa umma Tanzania tambueni kuwa ninyi sio Miungu watu ni watumishi wao mmpo hapo na hali mliyonayo inatokana na sisi kuwagharamikia ninyi. Hivyo basi haiingii akilini kuwaona waajiri wako" hamnazo".

Malengo ya kupitishwa kwa sheria ya Bima ya Afya kwa wote kwa hakika yanaweza yasifikiwe kutokana na taratibu na au watumishi wasiofaa wa Mfuko wa Bima ya Afya.

Mifano yangu itajikita katika Hospitali ya Bugando. Hapa kwenye jengo la Bima wahudumu wake nafikiri wasiokuwa na taaluma ya Afya, waliwataka ndugu warudi nyumbani kumleta mgonjwa ambaye yuko kwenye hali isiyoridhisha na kuhitaji usafiri wa tax ili wamuone kabla ya kumuona daktari ambaye kwa siku hiyo alikuwa anakwenda kuwasomea ndugu majibu ya vipimo alivyochukua.

Mfano mwingine unanihusu mimi. Mgonjwa wangu mwenye bima inayoitwa ya vifurushi alifanyiwa upasuaji hospitalini hapo. Kurudi kwa ajili ya klinik, kwa daktari aliyemfanyia upasuaji na kumpangia siku ya kurudi, tunaambiwa na wàsimamizi wa mfuko kuwa, haiwezekani mpaka muanzie hospitali ya chini iwapatie rufaa ya kwenda Bugando.

Mimi sio tabibu lakini jambo hili haliingii akilini. Siamini kwamba mgonjwa aliyepata matibabu hospitali kubwa anastahili kurudi nyuma ili apewe rufaa na hospitali ya chini kurudi hospitali kubwa.

Kimbembe ni kupata hiyo rufaa, haina tofauti na kuingia na kukutwa ukiwa na mnyama pori! Hospitali ya chini kwa hapa karibu ni Sekou Toure, hawa wako radhi wakuandikie uende Muhimbili lakini sio Bugando.

Mbilinge hizi na nyingine nyingi za watumishi na taratibu zisizofaa za bima ya Afya, zimenipelekea Juzi 23/11 kulipia gharama za matibabu licha ya kuwa mwanachama wa Timiza Afya.

Kwa msingi huu, uliojengwa na taratibu zisizofaa za mfuko wa Bima ya Afya, nina pata mashaka kama haiwezi kuwa kikwazo kwa Bima mpya.

Kwa sasa kuna mambo machache ya kufanya ili kuhakikisha taratibu hizi zina koma.

1. Katiba ya JMT inapiga marufuku vitendo vya ubaguzi wa aina yoyote. Tunakusudia kuiomba mahakama kutoa tafsiri ya kitendo cha watumishi wa umma kuruhusiwa kutibiwa popote ilhali watanzania wengine ambao kimsingi wanachangia zaidi kuliko hao wa umma, wakizuiliwa.

2. Kuishauri hospitali ya Bugando kuwa Bima ya Afya ni muwezeshaji wa huduma hivyo hawezi na hana mamlaka ya kuqapangia taratibu za kutoa huduma.

3. Mashirika na taasisi zisizokuwa za kiserikali, msiangalie tu kuhamashisha watu wajiunge na mifuko hii, angalieni pia utendaji wake.
 
Mkuu, mbaguzi ni mbaguzi tu. Wale makaburu hatukuwqpinga kwa rangi zao ni vitendo.
Bima ya Afya inankumbusha pia waiingereza walivyowafanyia wachina baada ya kuuteka mji wa Peiking. Waliweka mabango yaliyosomeka " Wachina na Mbwa hawaruhusiwi kuingia"
 
NHIF inaendeshwa kibaguzi. Sisi ambao si waajiriwa tunakataliwa huduma nyingi hata tukilipa kifurushi cha TIMIZA ambacho ndicho cha juu. Isitoshe tunalipa mwaka mzima mwanzoni kabla ya huduma kuanza.
Watumishi wa umma wanakatwa asilimia ya mshahara kila mwezi, kadri mshahara unavyoongezeka na makato yanaongezeka na haijalishi hata kama huna wategemezi........nyie hivyo vifurushi mnajiunga mkiwa mmeweka idadi kamili ya wategemezi.

Kwa hiyo kusema kwamba nyie mnachangia kuliko watumishi wa umma siyo kweli na kutaka kujenga hoja yako kwa kujilinganisha na watumishi wa umma unakuwa umeingia chaka maana wanazo incentives zao ambazo ukitaka kuzipata unatakiwa ujiunge nao.

Miaka nenda rudi wamepata changamoto ya mishahara isiyokidhi na kutolipwa stahiki mbalimbali, hasa walimu hapo hapo unataka uwasagie kunguni kwamba hawastahili kutibiwa popote wakati kila siku mnaponda kwamba walimu wana hali ngumu, mara kuajiriwa ni utumwa.​
 
1. Katiba ya JMT inapiga marufuku vitendo vya ubaguzi wa aina yoyote. Tunakusudia kuiomba mahakama kutoa tafsiri ya kitendo cha watumishi wa umma kuruhusiwa kutibiwa popote ilhali watanzania wengine ambao kimsingi wanachangia zaidi kuliko hao wa umma, wakizuiliwa
Pia iombe hiyo hiyo mahakama itoe tafsiri ya kitendo cha watumishi wa umma kuwekewa dhamana na serikali ili wapewe mikopo benki huku watanzania wengine wakijitafutia wenyewe dhamana zao ili uende nao sawa bin sawia😂😂
 
Watumishi wa umma wanakatwa asilimia ya mshahara kila mwezi, kadri mshahara unavyoongezeka na makato yanaongezeka na haijalishi hata kama huna wategemezi........nyie hivyo vifurushi mnajiunga mkiwa mmeweka idadi kamili ya wategemezi.

Kwa hiyo kusema kwamba nyie mnachangia kuliko watumishi wa umma siyo kweli na kutaka kujenga hoja yako kwa kujilinganisha na watumishi wa umma unakuwa umeingia chaka maana wanazo incentives zao ambazo ukitaka kuzipata unatakiwa ujiunge nao.

Miaka nenda rudi wamepata changamoto ya mishahara isiyokidhi na kutolipwa stahiki mbalimbali, hasa walimu hapo hapo unataka uwasagie kunguni kwamba hawastahili kutibiwa popote wakati kila siku mnaponda kwamba walimu wana hali ngumu, mara kuajiriwa ni utumwa.​
Mkuu.
Nafikiri issue hapa haipaswi kuwa umechangia kiwango gani. Na nyaraka za kiwango cha kuchangia kwa wasiokuwa watumishi wa umma kipo humu na madaraja yake. Issue ni taratibu zilizowekwa hatuna sababu ya mimi na wewe kutofautiana ilihali mtesi wetu yupo!
 
Habari wana Bodi,

Ninachokishuhudia katika mwenendo wa watendaji pamoja na hali ya sasa ya mfuko wa Bima yà Afya, inakatishà tamaa yà kwanini mfuko huu unawafanyia hivi wateja wake?

Kabla sijaendelea naomba niweke jambo moja sawa.. watumishi wa umma Tanzania tambueni kuwa ninyi sio Miungu watu ni watumishi wao mmpo hapo na hali mliyonayo inatokana na sisi kuwagharamikia ninyi. Hivyo basi haiingii akilini kuwaona waajiri wako" hamnazo".

Malengo ya kupitishwa kwa sheria ya Bima ya Afya kwa wote kwa hakika yanaweza yasifikiwe kutokana na taratibu na au watumishi wasiofaa wa Mfuko wa Bima ya Afya.

Mifano yangu itajikita katika Hospitali ya Bugando. Hapa kwenye jengo la Bima wahudumu wake nafikiri wasiokuwa na taaluma ya Afya, waliwataka ndugu warudi nyumbani kumleta mgonjwa ambaye yuko kwenye hali isiyoridhisha na kuhitaji usafiri wa tax ili wamuone kabla ya kumuona daktari ambaye kwa siku hiyo alikuwa anakwenda kuwasomea ndugu majibu ya vipimo alivyochukua.

Mfano mwingine unanihusu mimi. Mgonjwa wangu mwenye bima inayoitwa ya vifurushi alifanyiwa upasuaji hospitalini hapo. Kurudi kwa ajili ya klinik, kwa daktari aliyemfanyia upasuaji na kumpangia siku ya kurudi, tunaambiwa na wàsimamizi wa mfuko kuwa, haiwezekani mpaka muanzie hospitali ya chini iwapatie rufaa ya kwenda Bugando.

Mimi sio tabibu lakini jambo hili haliingii akilini. Siamini kwamba mgonjwa aliyepata matibabu hospitali kubwa anastahili kurudi nyuma ili apewe rufaa na hospitali ya chini kurudi hospitali kubwa.

Kimbembe ni kupata hiyo rufaa, haina tofauti na kuingia na kukutwa ukiwa na mnyama pori! Hospitali ya chini kwa hapa karibu ni Sekou Toure, hawa wako radhi wakuandikie uende Muhimbili lakini sio Bugando.

Mbilinge hizi na nyingine nyingi za watumishi na taratibu zisizofaa za bima ya Afya, zimenipelekea Juzi 23/11 kulipia gharama za matibabu licha ya kuwa mwanachama wa Timiza Afya.

Kwa msingi huu, uliojengwa na taratibu zisizofaa za mfuko wa Bima ya Afya, nina pata mashaka kama haiwezi kuwa kikwazo kwa Bima mpya.

Kwa sasa kuna mambo machache ya kufanya ili kuhakikisha taratibu hizi zina koma.

1. Katiba ya JMT inapiga marufuku vitendo vya ubaguzi wa aina yoyote. Tunakusudia kuiomba mahakama kutoa tafsiri ya kitendo cha watumishi wa umma kuruhusiwa kutibiwa popote ilhali watanzania wengine ambao kimsingi wanachangia zaidi kuliko hao wa umma, wakizuiliwa.

2. Kuishauri hospitali ya Bugando kuwa Bima ya Afya ni muwezeshaji wa huduma hivyo hawezi na hana mamlaka ya kuqapangia taratibu za kutoa huduma.

3. Mashirika na taasisi zisizokuwa za kiserikali, msiangalie tu kuhamashisha watu wajiunge na mifuko hii, angalieni pia utendaji w

Habari wana Bodi,

Ninachokishuhudia katika mwenendo wa watendaji pamoja na hali ya sasa ya mfuko wa Bima yà Afya, inakatishà tamaa yà kwanini mfuko huu unawafanyia hivi wateja wake?

Kabla sijaendelea naomba niweke jambo moja sawa.. watumishi wa umma Tanzania tambueni kuwa ninyi sio Miungu watu ni watumishi wao mmpo hapo na hali mliyonayo inatokana na sisi kuwagharamikia ninyi. Hivyo basi haiingii akilini kuwaona waajiri wako" hamnazo".

Malengo ya kupitishwa kwa sheria ya Bima ya Afya kwa wote kwa hakika yanaweza yasifikiwe kutokana na taratibu na au watumishi wasiofaa wa Mfuko wa Bima ya Afya.

Mifano yangu itajikita katika Hospitali ya Bugando. Hapa kwenye jengo la Bima wahudumu wake nafikiri wasiokuwa na taaluma ya Afya, waliwataka ndugu warudi nyumbani kumleta mgonjwa ambaye yuko kwenye hali isiyoridhisha na kuhitaji usafiri wa tax ili wamuone kabla ya kumuona daktari ambaye kwa siku hiyo alikuwa anakwenda kuwasomea ndugu majibu ya vipimo alivyochukua.

Mfano mwingine unanihusu mimi. Mgonjwa wangu mwenye bima inayoitwa ya vifurushi alifanyiwa upasuaji hospitalini hapo. Kurudi kwa ajili ya klinik, kwa daktari aliyemfanyia upasuaji na kumpangia siku ya kurudi, tunaambiwa na wàsimamizi wa mfuko kuwa, haiwezekani mpaka muanzie hospitali ya chini iwapatie rufaa ya kwenda Bugando.

Mimi sio tabibu lakini jambo hili haliingii akilini. Siamini kwamba mgonjwa aliyepata matibabu hospitali kubwa anastahili kurudi nyuma ili apewe rufaa na hospitali ya chini kurudi hospitali kubwa.

Kimbembe ni kupata hiyo rufaa, haina tofauti na kuingia na kukutwa ukiwa na mnyama pori! Hospitali ya chini kwa hapa karibu ni Sekou Toure, hawa wako radhi wakuandikie uende Muhimbili lakini sio Bugando.

Mbilinge hizi na nyingine nyingi za watumishi na taratibu zisizofaa za bima ya Afya, zimenipelekea Juzi 23/11 kulipia gharama za matibabu licha ya kuwa mwanachama wa Timiza Afya.

Kwa msingi huu, uliojengwa na taratibu zisizofaa za mfuko wa Bima ya Afya, nina pata mashaka kama haiwezi kuwa kikwazo kwa Bima mpya.

Kwa sasa kuna mambo machache ya kufanya ili kuhakikisha taratibu hizi zina koma.

1. Katiba ya JMT inapiga marufuku vitendo vya ubaguzi wa aina yoyote. Tunakusudia kuiomba mahakama kutoa tafsiri ya kitendo cha watumishi wa umma kuruhusiwa kutibiwa popote ilhali watanzania wengine ambao kimsingi wanachangia zaidi kuliko hao wa umma, wakizuiliwa.

2. Kuishauri hospitali ya Bugando kuwa Bima ya Afya ni muwezeshaji wa huduma hivyo hawezi na hana mamlaka ya kuqapangia taratibu za kutoa huduma.

3. Mashirika na taasisi zisizokuwa za kiserikali, msiangalie tu kuhamashisha watu wajiunge na mifuko hii, angalieni pia utendaji wake.
Kila kitu kina utaratibu wake, ukisoma vizuri maelezo ya vifurushi vya Bima, inakuonesha huduma unazo weza kuzipata kupitia kifurushi ulichochagua, idadi ya vipimo unavyoweza vipata kupitia hkifurushi hicho na vituo vya huduma na wameelekeza kuanzia ngazi ya chini Hadi Hospitali ya Taifa lakini iwe ni kwa rufaa. Na rufaa haiombwi ni taratibu za kawaida za kitabibu kwa jambo
 
Pia iombe hiyo hiyo mahakama itoe tafsiri ya kitendo cha watumishi wa umma kuwekewa dhamana na serikali ili wapewe mikopo benki huku watanzania wengine wakijitafutia wenyewe dhamana zao ili uende nao sawa bin sawia😂😂
Mkuu.
Labda ungekuja na hoja nyjngine, hatuna sababu ya kupingana mimi na wewe.

Hizi hoja za mikopo kwa watumishi zilete kwenye uzi mwingine ili tujadili.
 
Mkuu.
Labda ungekuja na hoja nyjngine, hatuna sababu ya kupingana mimi na wewe.

Hizi hoja za mikopo kwa watumishi zilete kwenye uzi mwingine ili tujadili.
Wewe si unataka mahakama itoe tafsiri kwa nini watumishi wa umma wamependelewa kwenye bima ya afya? maana yake unataka uwe sawa bin sawia na watumishi wa umma kwenye kila kitu, wakilipwa mashahara na wewe ulipwe, wakijengewa nyumba za kuishi na wewe ujengewe nk. nk........vinginevyo ungejenga hoja yako bila kutafuta kujilinganisha nao.​
 
Kila kitu kina utaratibu wake, ukisoma vizuri maelezo ya vifurushi vya Bima, inakuonesha huduma unazo weza kuzipata kupitia kifurushi ulichochagua, idadi ya vipimo unavyoweza vipata kupitia hkifurushi hicho na vituo vya huduma na wameelekeza kuanzia ngazi ya chini Hadi Hospitali ya Taifa lakini iwe ni kwa rufaa. Na rufaa haiombwi ni taratibu za kawaida za kitabibu kwa jambo
Mkuu,
Ni taratibu za kitabibu mgonjwa alyepatiwa matibabu Hospitali ya Kanda kurudishwa Hospitali ya mkoa? Na anayetoa maelekezo haya sio daktari ni mwezeshaji tu wa huduma?
 
Watumishi wa umma wanakatwa asilimia ya mshahara kila mwezi, kadri mshahara unavyoongezeka na makato yanaongezeka na haijalishi hata kama huna wategemezi........nyie hivyo vifurushi mnajiunga mkiwa mmeweka idadi kamili ya wategemezi.

Kwa hiyo kusema kwamba nyie mnachangia kuliko watumishi wa umma siyo kweli na kutaka kujenga hoja yako kwa kujilinganisha na watumishi wa umma unakuwa umeingia chaka maana wanazo incentives zao ambazo ukitaka kuzipata unatakiwa ujiunge nao.

Miaka nenda rudi wamepata changamoto ya mishahara isiyokidhi na kutolipwa stahiki mbalimbali, hasa walimu hapo hapo unataka uwasagie kunguni kwamba hawastahili kutibiwa popote wakati kila siku mnaponda kwamba walimu wana hali ngumu, mara kuajiriwa ni utumwa.​
Sitaki kuwasagia kunguni. Wana haki ya kupata wanachopewa. Nalalamika ubaguzi kwenye huduma.
Nimesoma humu basic salary ya daktari anayeanza ni 1,480,000. Malipo yake kwa mwaka ni 888,000. Anaweza kubeba wazazi wake. Tujaaliye hana watoto. Yeye binafsi na wazazi wake mchango wao ni 296,000 kila mmoja.
Nalipa 984,000 kwa ajili yangu peke yangu.
 
Mkuu,
Niliposema tunataka tafsiri ya jambo hili nilikuwa nafahamu pia kwamba ndugu zetu hawa wanapata zaidi yetu katika keki ambauo sote tunachangia lakini bila usawa kwa anayechangia zaidi kupata kidogo ilihali aliyechangia kidogo akinufaika zaidi.
 
Mkuu,
Ni taratibu za kitabibu mgonjwa alyepatiwa matibabu Hospitali ya Kanda kurudishwa Hospitali ya mkoa? Na anayetoa maelekezo haya sio daktari ni mwezeshaji tu wa huduma?
Hapo naweza sema ni suala la uelewa tu mlitofautiana, Kama alikuwa na appointment ya kurudi kwa follow up huwa mwezeshaji hakutakiwa kukuzuia, so si NHIF wenye makosa
 
Bima ya afya Tanzania haiwezekani.
Watu hawana pesa za kulipa kiasi halisi cha bima inabidi bei ipunguzwe na hapo huduma inapungua.
Magonjwa mengi na watu karibu wote ni wagonjwa.
Ufisadi wa kuongeza gharama zinazofanywa na mahospitali wakishirikiana na watumishi wa bima.
 
NHIF wawe wakweli, wamwambie Umi aache siasa kwenye taaluma. Bima ya vifurushi na hata hiyo ya wote itafilisi mfuko. Labda uanzishwe mfuko mpya kwa ajili ya makundi hayo ambao utakuwa anapata ruzuku kutoka serikalini na hautalazimishwa kujiendesha.
 
Hapo naweza sema ni suala la uelewa tu mlitofautiana, Kama alikuwa na appointment ya kurudi kwa follow up huwa mwezeshaji hakutakiwa kukuzuia, so si NHIF wenye makosa
Kitu nilicho baini kwa wanaoitwa watumisihi wa serikali ni mtazamo walionao wa sio kutoa huduma bali kuwa, watwana wa wananchi. Ukitaka kuliona hili leo angalia jirani yako anayejiita mgambo au polisi jamii.

Prof. Kitila anawaita wadhibiti badala ya wawezeshaji.
 
Back
Top Bottom