sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Mwan a Fa na Ay waliwahi kuwashtaki Tigo kutumia nyimbo zao kwenye miito ya kupiga simu, Tigo waliwalipa bilioni 2.15 lakini kiuhalisia huenda walibaki na bilioni 1.5 (kila moja milioni 750), Huenda walimlipa mwanasheria wao Albert Msando milioni 150 na wazee wazito wakapiga mchinjo wa milioni 500.
Kwa kiasi hicho Mwana Fa itakuwa aliamua kuchota walau 200 zake kuingia kwenye siasa na kweli aliingia kwa kishindo kwenye kipindi cha uchaguzi, Pesa hizo zinaweza kutosha kufanyia kampeni, kuwapooza wajumbe na kupata backup ya anachama, kumbuka nje ya upinzani hata ndani ya ccm kuna upinzani.
Kwa upande wa AY wengi tulikuwa na shauku ya kujua uwekezaji ataofanya maana hata yeye anajiita mzee wa commercial na kashafanya biashara kadhaa ikiwemo kumiliki kipindi maarufu cha Mkasi, kampuni ya unity entertainment, n.k.