Bila upinzani imara rais angekuwa Membe

Bila upinzani imara rais angekuwa Membe

Mtoa mada umekosea kidogo,kilichosababisha membe asipite ni baada ya Lowassa kukatwa!! Walivyomwaga mboga na wengine wakamwaga ugali! Ndipo magu akaokota dodo kumbuka makundi yaliyokuwepo ndani ya fisiem ndio yaliyosababisha.
 
Magufuli anamgeshimu sana Lowasa kuliko Jk na Mkapa.
 
Upo sawa kabisa, matunda ya Dr Magufuli sio tu ni presure ya upinzani, bali hata madudu na mwelekeo wote ni wa UKAWA tangu siku nyingi na imefika mahali CCM hawana namna kama kawaida yao wameidaka hoja na kutaka tuamini kuwa wao ndio wanatekeleza. Pressure ya UKAWA imemzaa Dr Magufuli mtu niliye amini siku nyingi ndio sahihi ndani ya CCM.

Ila umekosea kidogo, Dr Magufuli alisha teuliwa kabla ya Lowasa kuchukuliwa na UKAWA.
 
CCM Walijipanga ili kupambanana na nguvu ya DR SLAA kupitia kwa muungano wa UKAWA na wala si huyu fisadi mnayemsema.
 
Wakati tukimpongeza rais John P. Magufuli kwa tremendous job anayoifanya, tusisahau kuwapa credit UKAWA kwa kumpendekeza Lowassa kuwa mgombea urais.

Ujio wa Lowassa ndani ya UKAWA ulibadili kabisa mipango yote iliyokuwa imepangwa na watawala (system) ya kumweka mtu wao Membe ambaye angeendeleza 'status quo'.

Kwa hali hiyo kama Membe angekuwa rais haya madudu yanayoibuliwa leo ya vigogo kukwepa kodi yangefunikwa na wala tusingeyajua.

Mungu ana njia nyingi sana za kumsaidia mtu anayeonewa.

Mleta Mada jipange upya, hivi hukumbuki kuwa Membe alikatwa kabla hata ya Lowasa hajaamia Ukawa?
Membe alikatwa mwezi May wakati Lowasa aliamia Ukawa July.
Kwahiyo hakuna lowasa effects kwenye utendaji wa serikali ya sasa
 
Baada ya Lowassa alovyokatwa hasira za team lowasa ndani ccm ikamchagua magufuli

hiyo mnajiliwadha tu eti team Lowasa kumchagua Magufuli. Team Lowasa ilitakiwa ichague mtu dhaifu ili waje wamshinde kwenye kura kirahisi, if any . Ni ujinga kuchagua mtu mwenye reputation kama Magufuli atleast kwa TZ harafu uje ushindane naye na kisha ugomee matokeo.
Hii ya kusema team Lowasa ilimchagua Magufuli ni ujinga.
 
Mkuu unajua hawa wengne n ushabiki tu wa vyama ndo unawasumbua kwasababu Magufuli alipitishwa na Ccm kabla Lowassa hajaenda Ukawa, sasa haya maneno sijui wanayatoa wapi.
Alafu Magufuli alikuwa akizunguka nchi nzima kwa gari wakati wa kampeni hivo alikutana na hizi kelo za wananchi,alipoingia Ikulu ndo huyo anaanza kuzifanyia kazi sasa hili la kusema UKAWA wamemfumbua macho linakujaje?

Tumalize hivi mtoa mada alikosea ku cot ni kwamba baada ya lowasa kukatwa kwenye mchujo wale wafuasi wa lowasa walikuwa wengi sana so kwa hasira ili membe asipite wakampigania magufuli mpaka amepita
 
Ona sasa wana Ukawa wanavyojifariji. Hivi bado tu mna machungu ya EL kukatwa na Nec? NEC ili Jipangeni tu kwa ajili 2020 mumsimamishe kingunge au Sumaye muone tena balaa lake.
 
hiyo mnajiliwadha tu eti team Lowasa kumchagua Magufuli. Team Lowasa ilitakiwa ichague mtu dhaifu ili waje wamshinde kwenye kura kirahisi, if any . Ni ujinga kuchagua mtu mwenye reputation kama Magufuli atleast kwa TZ harafu uje ushindane naye na kisha ugomee matokeo.
Hii ya kusema team Lowasa ilimchagua Magufuli ni ujinga.

Lowasa alijua mpango wa ccm ni kuhakikisha hapiti na inasemekana baada ya lowasa kujua kupita ni vigumu alimshawishi sana magufuli achukuwe form kwa taadhari ili kama kama akikatwa ahakikishe anachukuwa yeye.
 
Wapenzi wa lowassa ndani ya NEC waliamua kuwa chaguo la kikwete (Membe) hawezi penya kwa namna yoyote ile,mpira ukamuangukia JPM!

Kwa formula za ki-Mungu hapo ndo mbaraka wa EL ulichomokea. Waamnio watanielewa. Nishukuru EL kuwamwamini Mungu na watumishi wake.
 
Tumalize hivi mtoa mada alikosea ku cot ni kwamba baada ya lowasa kukatwa kwenye mchujo wale wafuasi wa lowasa walikuwa wengi sana so kwa hasira ili membe asipite wakampigania magufuli mpaka amepita

KWanini wasingempigia kama yule mama Rose ili waje wamshinde kirahisi ?
 
Acha kujitoa ufahamu,Lowasa kaenda ukawa baada ya kukatwa,Hivyo kukatwa kwa membe hakuna relationship na Lowasa kwenda ukawa.Sema hivi wafuasi wa lowasa wa CCM ilibidi wampigie kura Magufuli ili Membe asipenye na walifanya hivyo ili kumkomoa JK
Ndiyo maana yake.
 
Back
Top Bottom