Wakati tukimpongeza rais John P. Magufuli kwa tremendous job anayoifanya, tusisahau kuwapa credit UKAWA kwa kumpendekeza Lowassa kuwa mgombea urais.
Ujio wa Lowassa ndani ya UKAWA ulibadili kabisa mipango yote iliyokuwa imepangwa na watawala (system) ya kumweka mtu wao Membe ambaye angeendeleza 'status quo'.
Kwa hali hiyo kama Membe angekuwa rais haya madudu yanayoibuliwa leo ya vigogo kukwepa kodi yangefunikwa na wala tusingeyajua.
Mungu ana njia nyingi sana za kumsaidia mtu anayeonewa.
Fikiria kwanza kabla hujapost thread, Lowassa akienda CDM tayari mchakato wa kumpata mgombea CCM tayari ulikuwa umemalizika na yeye alishiriki hadi hatua ya mwisho ya mkutano mkuu na alipiga kura ambayo JPM aliibuka mshindi. Sasa hzo porojo za kuwa kwenda ukawa aliharibu mipango haina mashiko. Ukiwa mwongo usiwe msahaulifu kwani huwa tunaweka akiba ya maneno