Bila upendo na umoja ni ngumu sana kuuondoa umaskini kwenye familia

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,223
22,299
"Bora mtu baki kuliko ndugu"

Hii ni kauli maarufu sana nyakati hizi kwasbabu ya upendo wa wanafamilia wengi kupungua baina yao. Wanafamilia wamekuwa hawapendani na kupelekea umaskini kuzidi kushamiri. Kwanza tujue kuwa bila familia imara hakuwezi kuwa na taifa imara. Mafanikio ya taifa yanaanza na familia. Familia ndo zinatoa wataalamu, wanasiasa, wanamichezo, wasanii hata viongozi wa dini. Lakini kwa upande mwingine familia ndo zinatoa mafisadi, majambazi na wahalifu wa kila aina. Kwahiyo familia sio kitu cha mchezo mchezo.

Tukija kwenye hoja kuhusu uhusiano wa umaskini na familia ndo tunajikuta tunajiuliza swali kuu "tunauondoa vipi umaskini kwenye familia?". Kimsingi kazi hii sio ndogo.. ni shughuli pevu kwelikweli yenye mchakato mrefu. Hakuna kanuni sahihi jinsi gani umaskini utatokomezwa lakini kuna mambo ya kuzingatia bila kujali mbinu gani inayotumika na wanafamilia kupambana na umaskini. Kuna familia nyingi zilizojiondoa kwenye umaskini kwa kupitia elimu. Mbinu ya elimu ni ya uhakika sana. Lakini kuna zingine kupitia vipaji vya wanafamilia wakajikuta pia wamefanikiwa. Kina Filbert Bayi, Diamond Platinumz, Christiano Ronaldo, Harmonize, Shilole, Kajala, Steve Nyerere na wengine ni mifano ya watu walioweza kuushinda umaskini kupitia vipaji vyao.

Lakini ili umaskini kutokomezwa lazima familia nzima iwe kitu kimoja na wapendane. Yaani asitokee mtu kujiona bora kuliko wenzake au kuleta ubinafsi na wivu. Mara nyingi huwa anatokea mwanafamilia mmoja ambaye nadhani Mungu humtumia kuondoa umaskini wa familia. Kwa mfano anaweza kutokea mtoto mmoja mwenye akili za ajabu akaja kupata kazi ya mshahara mnono na marupurupu akawainua wenzake. Au mwingine akaanza biashara na kufanikiwa kisha kuibeba familia yake.

Diamond Platinumz ni mfano hai mrahisi wa mwanafamilia mmoja kufanikiwa na kuiinua familia yake nzima. Lakini hiyo huwa inawezekana endapo wanafamilia wanaheshimiana na kupendana. Tukiangalia Diamond ni mdogo kwao lakini iko wazi familia yake inamheshimu na kumpenda hivyo wakajikuta na wao wananufaika. Lakini pia Diamond angeweza kuwa mbinafsi na kufakamia hela zake peke yake na vidosho ila kutokana na upendo ndo tunaona pia ndugu zake wanaofahamika na wao wako vizuri.

Je, huu umoja na upendo inawezekanaje? Jibu ni kupitia wazazi. Baba na mama lazima wawajibike kuwajengea watoto roho za kupendana na kusaidiana kuanzia utotoni. Mimi baba yangu toka utotoni lazima awepo kwenye chakula cha usiku na familia nzima. Hata baada ya kula lazima awapigie stori mbalimbali na kujikuta familia nzima mnafurahi. Wale kina baba wanaotumia muda wa jioni kuwa bar na kurudi watoto wamelala mnafanya upumbavu. Hata kina mama pia lazima wawe wakali sana kwa watoto wenye tabia za ubinafsi ili asije akawa na tabia hiyo. Wazazi wanapoachana huwa ni huzuni duniani mpaka mbinguni, lakini hata ikifikia point lazima muachane basi hakikisheni mnapambania watoto wenu wakue vizuri.

Single mama pia hakuna jinsi, lazima mpambanie watoto wenu wakue vizuri wakiwa na maadili mazuri. Mama Diamond ni mfano mzuri wa mama aliyehakikisha mwanae anafanikiwa na kuwa na maadili. Yule kijana ana nidhamu. Lakini ile nidhamu yake ni kazi ya Bi Sandra.
 
Ni jambo jema sana familia kupendana, shida inakuja familia zetu hizi za watoto kila mmoja na mamaake taabu tupu hawa watu daima huwa na upendo wa kinafki sana hasa baba akitoweka duniani
 
"Bora mtu baki kuliko ndugu"

Hii ni kauli maarufu sana nyakati hizi kwasbabu ya upendo wa wanafamilia wengi kupungua baina yao. Wanafamilia wamekuwa hawapendani na kupelekea umaskini kuzidi kushamiri. Kwanza tujue kuwa bila familia imara hakuwezi kuwa na taifa imara. Mafanikio ya taifa yanaanza na familia. Familia ndo zinatoa wataalamu, wanasiasa, wanamichezo, wasanii hata viongozi wa dini. Lakini kwa upande mwingine familia ndo zinatoa mafisadi, majambazi na wahalifu wa kila aina. Kwahiyo familia sio kitu cha mchezo mchezo.

Tukija kwenye hoja kuhusu uhusiano wa umaskini na familia ndo tunajikuta tunajiuliza swali kuu "tunauondoa vipi umaskini kwenye familia?". Kimsingi kazi hii sio ndogo.. ni shughuli pevu kwelikweli yenye mchakato mrefu. Hakuna kanuni sahihi jinsi gani umaskini utatokomezwa lakini kuna mambo ya kuzingatia bila kujali mbinu gani inayotumika na wanafamilia kupambana na umaskini. Kuna familia nyingi zilizojiondoa kwenye umaskini kwa kupitia elimu. Mbinu ya elimu ni ya uhakika sana. Lakini kuna zingine kupitia vipaji vya wanafamilia wakajikuta pia wamefanikiwa. Kina Filbert Bayi, Diamond Platinumz, Christiano Ronaldo, Harmonize, Shilole, Kajala, Steve Nyerere na wengine ni mifano ya watu walioweza kuushinda umaskini kupitia vipaji vyao.

Lakini ili umaskini kutokomezwa lazima familia nzima iwe kitu kimoja na wapendane. Yaani asitokee mtu kujiona bora kuliko wenzake au kuleta ubinafsi na wivu. Mara nyingi huwa anatokea mwanafamilia mmoja ambaye nadhani Mungu humtumia kuondoa umaskini wa familia. Kwa mfano anaweza kutokea mtoto mmoja mwenye akili za ajabu akaja kupata kazi ya mshahara mnono na marupurupu akawainua wenzake. Au mwingine akaanza biashara na kufanikiwa kisha kuibeba familia yake.

Diamond Platinumz ni mfano hai mrahisi wa mwanafamilia mmoja kufanikiwa na kuiinua familia yake nzima. Lakini hiyo huwa inawezekana endapo wanafamilia wanaheshimiana na kupendana. Tukiangalia Diamond ni mdogo kwao lakini iko wazi familia yake inamheshimu na kumpenda hivyo wakajikuta na wao wananufaika. Lakini pia Diamond angeweza kuwa mbinafsi na kufakamia hela zake peke yake na vidosho ila kutokana na upendo ndo tunaona pia ndugu zake wanaofahamika na wao wako vizuri.

Je, huu umoja na upendo inawezekanaje? Jibu ni kupitia wazazi. Baba na mama lazima wawajibike kuwajengea watoto roho za kupendana na kusaidiana kuanzia utotoni. Mimi baba yangu toka utotoni lazima awepo kwenye chakula cha usiku na familia nzima. Hata baada ya kula lazima awapigie stori mbalimbali na kujikuta familia nzima mnafurahi. Wale kina baba wanaotumia muda wa jioni kuwa bar na kurudi watoto wamelala mnafanya upumbavu. Hata kina mama pia lazima wawe wakali sana kwa watoto wenye tabia za ubinafsi ili asije akawa na tabia hiyo. Wazazi wanapoachana huwa ni huzuni duniani mpaka mbinguni, lakini hata ikifikia point lazima muachane basi hakikisheni mnapambania watoto wenu wakue vizuri.

Single mama pia hakuna jinsi, lazima mpambanie watoto wenu wakue vizuri wakiwa na maadili mazuri. Mama Diamond ni mfano mzuri wa mama aliyehakikisha mwanae anafanikiwa na kuwa na maadili. Yule kijana ana nidhamu. Lakini ile nidhamu yake ni kazi ya Bi Sandra.
Moja Kati ya uzi Bora kabisa
 
Kwanza familia unamaanisha nini? Mimi kwangu Familia ni Mama, Baba na Watoto wao, sasa wewe umemaanisha familia ipi?
 
"Bora mtu baki kuliko ndugu"

Hii ni kauli maarufu sana nyakati hizi kwasbabu ya upendo wa wanafamilia wengi kupungua baina yao. Wanafamilia wamekuwa hawapendani na kupelekea umaskini kuzidi kushamiri. Kwanza tujue kuwa bila familia imara hakuwezi kuwa na taifa imara. Mafanikio ya taifa yanaanza na familia. Familia ndo zinatoa wataalamu, wanasiasa, wanamichezo, wasanii hata viongozi wa dini. Lakini kwa upande mwingine familia ndo zinatoa mafisadi, majambazi na wahalifu wa kila aina. Kwahiyo familia sio kitu cha mchezo mchezo.

Tukija kwenye hoja kuhusu uhusiano wa umaskini na familia ndo tunajikuta tunajiuliza swali kuu "tunauondoa vipi umaskini kwenye familia?". Kimsingi kazi hii sio ndogo.. ni shughuli pevu kwelikweli yenye mchakato mrefu. Hakuna kanuni sahihi jinsi gani umaskini utatokomezwa lakini kuna mambo ya kuzingatia bila kujali mbinu gani inayotumika na wanafamilia kupambana na umaskini. Kuna familia nyingi zilizojiondoa kwenye umaskini kwa kupitia elimu. Mbinu ya elimu ni ya uhakika sana. Lakini kuna zingine kupitia vipaji vya wanafamilia wakajikuta pia wamefanikiwa. Kina Filbert Bayi, Diamond Platinumz, Christiano Ronaldo, Harmonize, Shilole, Kajala, Steve Nyerere na wengine ni mifano ya watu walioweza kuushinda umaskini kupitia vipaji vyao.

Lakini ili umaskini kutokomezwa lazima familia nzima iwe kitu kimoja na wapendane. Yaani asitokee mtu kujiona bora kuliko wenzake au kuleta ubinafsi na wivu. Mara nyingi huwa anatokea mwanafamilia mmoja ambaye nadhani Mungu humtumia kuondoa umaskini wa familia. Kwa mfano anaweza kutokea mtoto mmoja mwenye akili za ajabu akaja kupata kazi ya mshahara mnono na marupurupu akawainua wenzake. Au mwingine akaanza biashara na kufanikiwa kisha kuibeba familia yake.

Diamond Platinumz ni mfano hai mrahisi wa mwanafamilia mmoja kufanikiwa na kuiinua familia yake nzima. Lakini hiyo huwa inawezekana endapo wanafamilia wanaheshimiana na kupendana. Tukiangalia Diamond ni mdogo kwao lakini iko wazi familia yake inamheshimu na kumpenda hivyo wakajikuta na wao wananufaika. Lakini pia Diamond angeweza kuwa mbinafsi na kufakamia hela zake peke yake na vidosho ila kutokana na upendo ndo tunaona pia ndugu zake wanaofahamika na wao wako vizuri.

Je, huu umoja na upendo inawezekanaje? Jibu ni kupitia wazazi. Baba na mama lazima wawajibike kuwajengea watoto roho za kupendana na kusaidiana kuanzia utotoni. Mimi baba yangu toka utotoni lazima awepo kwenye chakula cha usiku na familia nzima. Hata baada ya kula lazima awapigie stori mbalimbali na kujikuta familia nzima mnafurahi. Wale kina baba wanaotumia muda wa jioni kuwa bar na kurudi watoto wamelala mnafanya upumbavu. Hata kina mama pia lazima wawe wakali sana kwa watoto wenye tabia za ubinafsi ili asije akawa na tabia hiyo. Wazazi wanapoachana huwa ni huzuni duniani mpaka mbinguni, lakini hata ikifikia point lazima muachane basi hakikisheni mnapambania watoto wenu wakue vizuri.

Single mama pia hakuna jinsi, lazima mpambanie watoto wenu wakue vizuri wakiwa na maadili mazuri. Mama Diamond ni mfano mzuri wa mama aliyehakikisha mwanae anafanikiwa na kuwa na maadili. Yule kijana ana nidhamu. Lakini ile nidhamu yake ni kazi ya Bi Sandra.
Familia nyingi membars wake ni full kurogana na kupigana misumali tu.

Chuki hizi mara nyingi hutokana na malezi ya tangu utotoni jinsi mlivyokuwa treated na wazazi au baadhi ya walezi.


Familia za kiafrika ikitokea mkapendana wote miongini mwenu basi mtakumbana na misumari ya majirani zenu labda muwe mnaishi osterbay ama masaki.
 
Uzi Bora Sana. Katika thread mzur za Mwaka hii imo

Umenisema waziwazi nasema Asante kukaa bar ni kosa kubwa nalifanya.

Hii tabia kwenye wizara mfano Tamisemi... kiongozi anawapa nafasi ndgu zake nayo unaizungumziaje, ndio kuisaidia ndg zako Nako ni njia?? Rushwa Moja ya kipuuz Sana iliyoko kwenye serikali.
 
Back
Top Bottom