Bila aibu wala woga, CCM yaitangazia dunia kuwa hakuna Mtanzania mwenye uadilifu!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Baada ya CCM kuitangazia dunia...
  • Kwamba Watanzania hatuna mwenye uwezo wa kusimamia uendeshaji wa chombo kama Bandari kwa uadilifu!
  • Kwamba Watanzania kwa ujumla wetu ni watu wasio na uaminifu katika utendaji wa kazi popote pale tulipo,
  • Kwamba Watanzania kwa tabia sisi ni wadokozi, wala rushwa na wasiowajibika kwa matendo yetu.
  • Kwamba Watazania kwa desturi zetu si binadamu walio na busara wala hekima katika kulinda kilicho chetu.
  • Kwamba Watanzania hatuna ari ya kujiletea maendelo peke yetu bila kusimamiwa na wageni kutoka nje.
  • Kwamba sisi Watanzania ni wavivu wa kufikiri tusio na ubunifu unaoendana na kasi ya mabadiliko duniani,
  • Kwamba peke yetu, sisi Watanzania ni viumbe tofauti kabisa tuliojikuta labda hapa duniani kwa bahati mbaya tu.
  • Kwamba pamoja na kujaaliwa neema lukuki ya mali asili sisi peke yetu hatuna fikra ya kujikwamua kutoka lindi la umasikini.
Inaaminika kuwa ili taifa liendelee vitu vinne vinahitajika; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora, Je Watanzania tunachokosa ni nini?

Kama chama tawala CCM kinakiri na kuitangazia dunia kwamba Tanzania hakuna mwenye uwezo, sifa wala busara, je tutegemee nini?

Sifa zote wanazozitaja kupelekea kuuzwa kwa bandari ndio sifa hizo hizo viongozi wao wengi ndani ya chama na ndani ya serikali wanazo.

Sasa shangaa walivyo mataahira. Baada ya kuitangazia dunia hivyo bado wana uhalali gani wa kuendelea kung'ang'ania madaraka?

Na Watanzania kwa ukondoo wao badala ya kuwawajibisha, wanawachekea tu na kupiga vigelegele huku wanaibiwa mchana kweupe.

Kwa nini kwa mfano tusiwatafute watu nje ya CCM wenye hizo sifa wanazokiri hawana watuongoze? Ya nini CCM kung'ang'ania madaraka?

Tumeanza na bandari na zipo tetesi kwamba yapo mengi yako jikoni yanapikwa na CCM, je tunarudi utumwani? Sasa tulidai uhuru wa nini?

Hivi kati ya Watanzania 60,000,000 wanaCCM ni wangapi? Sijui jamii za Kimataifa zinaiangaliaje hiyo CV mpya tuliyobebeshwa na CCM!
 
Baada ya CCM kuitangazia dunia...
  • Kwamba Watanzania hatuna mwenye uwezo wa kusimamia uendeshaji wa chombo kama Bandari kwa uadilifu!
  • Kwamba Watanzania kwa ujumla wetu ni watu wasio na uaminifu katika utendaji wa kazi popote pale tulipo,
  • Kwamba Watanzania kwa tabia sisi ni wadokozi, wala rushwa na wasiowajibika kwa matendo yetu.
  • Kwamba Watazania kwa desturi zetu si binadamu walio na busara wala hekima katika kulinda kilicho chetu.
  • Kwamba Watanzania hatuna ari ya kujiletea maendelo peke yetu bila kusimamiwa na wageni kutoka nje.
  • Kwamba sisi Watanzania ni wavivu wa kufikiri tusio wala ubunifu unaoendana na kasi ya mabadiliko duniani,
  • Kwamba peke yetu, sisi Watanzania ni viumbe tofauti kabisa tuliojikuta labda hapa duniani kwa bahati mbaya tu.
  • Kwamba pamoja na kujaaliwa kila aina ya mali asili sisi peke yetu hatuna fikra ya kujikwamua kutoka lindi la umasikini.
Inaaminika kuwa ili taifa liendelee vitu vinne vinahitajika; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora, Je Watanzania tunachokosa ni nini?

Kama chama tawala CCM kinakiri na kuitangazia dunia kwamba Tanzania hakuna mwenye uwezo, sifa wala busara, je tutegemee nini?

Kwa nini kwa mfano tusiwatafute watu nje ya CCM wenye hizo sifa wanazokiri hawana watuongoze? Ya nini CCM kung'ang'ania madaraka?
Hizi tabia tunazo kweli. Lakini tunapaswa kuweka mifumo ya kuwadhibiti watu ili walete ufanisi.
 
Ukiona mbwa kakonda ujue shida ipo kwa mfugaji, sio mbwa.

Ukiona mtoto ana tabia zisizokubalika asilimia 99% ni mzazi.

Serikali ina kila mifumo ya usimamizi..kuanziaTISS, jeshi na polisi..miaka fulani wakati wa JPM kulikuwa na zoezi la uhakiki mashamba ya korosho..jamaa yangu ni afisa kilimo nikamuambia hiyo ni fursa ya kucheza na wakulima atengeneze pesa..jamaa akasema hawezi fanya kitu kama hicho,lazima watoe taarifa sahihi..maana wao wakimaliza kuhakiki kuna watu wasiojulikana wataenda tena kuhakiki.

Kwa hiyo kupanga ni kuchagua.
 
Watanganyika acheni kulalamika msikubali nchi yenu kuuzwa

Wanaouza nchi wameshapewa mijumba uko kwa wajomba dubei

Wakimalizwa kazi waliotumwa wanaondoka uarabuni
 
Na kwamba hata wao wapo kwenye nafasi zao kwaajili ya matanuzi tu hawana majukumu zaidi ya kuzurura na kkudumbua kodi zetu
Hao ni akina nani? Je jukumu la kuwabana matanuzi unayozungumzia nalo tunawapa Waarabu kwa kuwa tumeshindwa kama Watanzania?
 
Hao ni akina nani? Je jukumu la kuwabana matanuzi unayozungumzia nalo tunawapa Waarabu kwa kuwa tumeshindwa kama Watanzania?
Ni swali la kuwauliza wenye sare wenzao
 
Ukiona mbwa kakonda ujue shida ipo kwa mfugaji, sio mbwa.
Kwa Tanzania yetu mfugaji ni nani na mbwa ni nani? Kumbuka mbwa hana akili, lakini sisi Watanzania kama walivyo binadamu wengine tlijaaliwa akili na Mwenyezi Mungu
Ukiona mtoto ana tabia zisizokubalika asilimia 99% ni mzazi.
Je mzazi wa Watanzania kwa ujumla wao ni nani na mtoto yupi hapa unamuongelea?
 
Baada ya CCM kuitangazia dunia...
  • Kwamba Watanzania hatuna mwenye uwezo wa kusimamia uendeshaji wa chombo kama Bandari kwa uadilifu!
  • Kwamba Watanzania kwa ujumla wetu ni watu wasio na uaminifu katika utendaji wa kazi popote pale tulipo,
  • Kwamba Watanzania kwa tabia sisi ni wadokozi, wala rushwa na wasiowajibika kwa matendo yetu.
  • Kwamba Watazania kwa desturi zetu si binadamu walio na busara wala hekima katika kulinda kilicho chetu.
  • Kwamba Watanzania hatuna ari ya kujiletea maendelo peke yetu bila kusimamiwa na wageni kutoka nje.
  • Kwamba sisi Watanzania ni wavivu wa kufikiri tusio na ubunifu unaoendana na kasi ya mabadiliko duniani,
  • Kwamba peke yetu, sisi Watanzania ni viumbe tofauti kabisa tuliojikuta labda hapa duniani kwa bahati mbaya tu.
  • Kwamba pamoja na kujaaliwa neema lukuki ya mali asili sisi peke yetu hatuna fikra ya kujikwamua kutoka lindi la umasikini.
Inaaminika kuwa ili taifa liendelee vitu vinne vinahitajika; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora, Je Watanzania tunachokosa ni nini?

Kama chama tawala CCM kinakiri na kuitangazia dunia kwamba Tanzania hakuna mwenye uwezo, sifa wala busara, je tutegemee nini?

Kwa nini kwa mfano tusiwatafute watu nje ya CCM wenye hizo sifa wanazokiri hawana watuongoze? Ya nini CCM kung'ang'ania madaraka?

Tumeanza na bandari na zipo tetesi kwamba yapo mengi yako jikoni yanapikwa na CCM, je tunarudi utumwani? Sasa tulidai uhuru wa nini?
CCM ndiyo yenye hizo tabia zote na niwabobezi kwenye hizo tabia
 
Kwa Tanzania yetu mfugaji ni nani na mbwa ni nani? Kumbuka mbwa hana akili, lakini sisi Watanzania kama walivyo binadamu wengine tlijaaliwa akili na Mwenyezi Mungu

Je mzazi wa Watanzania kwa ujumla wao ni nani na mtoto yupi hapa unamuongelea?
Nimefafanua chini..soma maelezo yote mag3.
 
Ni kweli, tumeitangazia dunia kuwa sisi sio lolote katika utendaji. Wanasubiri nini kuleta mawaziri toka mataifa mengine watuongoze..
 
Hizi tabia tunazo kweli. Lakini tunapaswa kuweka mifumo ya kuwadhibiti watu ili walete ufanisi.
Je unaamini kuwa sisi Watanzania ni viumbe tofauti na binadamu wengine? Mifumo hiyo itawekwa na nani? Je kuna mfumo wowote hivi sasa unaoruhusu wizi na ulaji rushwa? Kama ni viongozi ndio wahusika, kwa nini hatuwabani?
 
Ni kweli, tumeitangazia dunia kuwa sisi sio lolote katika utendaji. Wanasubiri nini kuleta mawaziri toka mataifa mengine watuongoze..
Mimi nina ubunifu wangu, (intellectual property) kwanini biashara zinakufa na ninikifanyike, namalizia andiko langu cha kushangaza serikali ndiyo inahusika kwe kuua biashara kwakifupi serikali ndiyo itakuwa imeua bandari zetu na nina uhakika tukifanya utafiti litawekwa bayana
 
Ni kweli, tumeitangazia dunia kuwa sisi sio lolote katika utendaji. Wanasubiri nini kuleta mawaziri toka mataifa mengine watuongoze..
Mbona wako Watanzania wengi tu huko nje wanasifika kwa utendaji wao na uwajibikaji? Kwa nini hilo halipo hapa ndani ya nchi, je mchawi wetu ni nani?
 
Hayo maneno yana ukweli kwa asilimia kubwa japokuwa sio watanzania wote wenye hio tabia wapo ambao ni waadilifu na wachapa kazi kama mimi 😊
Je dawa ni kuwaleta wageni au ni kuwachukulia hatua viongozi limbukeni. Tunashindwa wapi?
 
Watanganyika acheni kulalamika msikubali nchi yenu kuuzwa
Nadhani tatizo letu kubwa ni unafiki. Mbolea inayostaawisha unafiki ni woga. Tunamjua adui lakini kwa woga tunasita kumnyoshea kidole.
Wanaouza nchi wameshapewa mijumba uko kwa wajomba dubei
Hao wauza nchi tunaishi nao, tunakula nao, tunalala nao. Kila baada ya miaka mitano tunawachagua waendelee kuuuza nchi.

Nasema hivyo kwa sababu mwenye ychungu na chake hawezi kunyamaza chake kikiibiwa. Ukondoo wetu ndio unawapa ujasiri wa kuendelea kutuibia
Wakimalizwa kazi waliotumwa wanaondoka uarabuni
Na sisi tunawasubiri wamalize kazi waondoke uarabuni...ujinga gani huu?
 
Mbona wako Watanzania wengi tu huko nje wanasifika kwa utendaji wao na uwajibikaji? Kwa nini hilo halipo hapa ndani ya nchi, je mchawi wetu ni nani?
We, ourselves and us.

Umimi, ubinafsi, wizi na kukosa uzalendo.

Manake huwezi kuweka misingi bora, taasisi bora wala mifumo imara ukikosa watu wa namna hii.

Ukienda hukona wizi wako unakutana na mifumo imara sana, huchomoi!
 
Baada ya CCM kuitangazia dunia...
  • Kwamba Watanzania hatuna mwenye uwezo wa kusimamia uendeshaji wa chombo kama Bandari kwa uadilifu!
  • Kwamba Watanzania kwa ujumla wetu ni watu wasio na uaminifu katika utendaji wa kazi popote pale tulipo,
  • Kwamba Watanzania kwa tabia sisi ni wadokozi, wala rushwa na wasiowajibika kwa matendo yetu.
  • Kwamba Watazania kwa desturi zetu si binadamu walio na busara wala hekima katika kulinda kilicho chetu.
  • Kwamba Watanzania hatuna ari ya kujiletea maendelo peke yetu bila kusimamiwa na wageni kutoka nje.
  • Kwamba sisi Watanzania ni wavivu wa kufikiri tusio na ubunifu unaoendana na kasi ya mabadiliko duniani,
  • Kwamba peke yetu, sisi Watanzania ni viumbe tofauti kabisa tuliojikuta labda hapa duniani kwa bahati mbaya tu.
  • Kwamba pamoja na kujaaliwa neema lukuki ya mali asili sisi peke yetu hatuna fikra ya kujikwamua kutoka lindi la umasikini.
Inaaminika kuwa ili taifa liendelee vitu vinne vinahitajika; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora, Je Watanzania tunachokosa ni nini?

Kama chama tawala CCM kinakiri na kuitangazia dunia kwamba Tanzania hakuna mwenye uwezo, sifa wala busara, je tutegemee nini?

Kwa nini kwa mfano tusiwatafute watu nje ya CCM wenye hizo sifa wanazokiri hawana watuongoze? Ya nini CCM kung'ang'ania madaraka?

Tumeanza na bandari na zipo tetesi kwamba yapo mengi yako jikoni yanapikwa na CCM, je tunarudi utumwani? Sasa tulidai uhuru wa nini?
Kwa kifupi CCM imekiri kuwa ni chama cha kifisadi na kimejaa viongozi na wanachama majizi na mafisadi!
 
Mafara yamejianika.
Yanajisema wazi bila kufikiri watu wa naangalia kiongozi ili wapate picha nchi ikoje kwa upande mmoja then waje kwa wanacnhi waliosalia.
 
Back
Top Bottom