Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Watanzania,
Ukubali ama ukatae, uchukie ama ukasirike.utukane ama usonye.ulaani ama ubariki ukweli ni kuwa CCM na Serikali yake ndio bima ya matatizo,kero na changamoto za watanzania.ndio maana mtu akipatwa na matatizo au kuonewa au kunyanyaswa anaangalia wapi kuliko na ofisi ya CCM ama wapi wanapatikana viongozi wa CCM ama amkimbilie Kiongozi yupi wa CCM kupata suluhu ya matatizo yake.
Ndio maana kwa sasa ni kawaida kuona watu kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wakitafuta kwa kila njia namba za viongozi wa CCM ili kufikisha vilio vyao,kwa kuwa wanajuwa viongozi wa CCM Ni wasikivu,wenye huruma,upendo,ukarimu, unyenyekevu,utu,uungwana,utayari na wenye maamuzi ya haraka katika kuwasaidia wanyonge na wenye kuelemewa na mizigo ya shida mbalimbali zinazowasibu.
Lakini pia wanawatafuta na kuwakimbilia CCM kwa kuwa wanajuwa ndio wenye serikali,ndio wenye majibu,ndio wenye suluhisho ,ndio wenye sauti,ndio wenye ufunguo wa kila mlango,ndio wenye amri ya mwisho,ndio watoa maamuzi ndio walio pewa dhamana ya kuongoza Taifa hili na wanajuwa kuwa ukifika na kufikisha kero yako CCM lazima upate tumaini,faraja na tabasamu katika moyo wako.
Ndio maana vijana mbalimbali kutoka maeneo mbalimbali nchini wanaojitolea kwa muda mrefu katika ofisi na maeneo tofauti tofauti wanaikimbili CCM pale wanapoona wameonewa au hawajatendewa haki au kumefanyika upendeleo wa waziwazi wa kuwapatia ajira watu wengine ambao hawakustahili kupata ajira serikalini na kuwaacha wao wakiwa na sifa stahiki.
ambao kwa moyo wa upendo na uzalendo wamekuwa wakifanya kazi bure kwa kujitolea pasipo malipo lakini mwisho wa siku wanaachwa na kuchukuliwa wengine kwa kuwa tu kuna viongozi wa juu katika halmashauri husika wanaoamua kupachika ndugu zao au wale waliotoa fedha kama rushwa na kuwaacha watoto wa maskini wakibubujikwa na machozi kwa huzuni na maumivu makubwa kwa kutotendewa haki na wahusika.
Hii ndio maana unaona Watanzania wengi sana wakiwepo wale wa kutoka vyama vya upinzani wakiwa karibu sana kufutilia kila kinachokuwa kinaendelea na kujiri ndani ya CCM.kwa kuwa kila mtu anafahamu kuwa CCM Ndio Kila kitu katika Taifa letu na kwamba ikipiga chafya tu lazima kila mtu apate mafua na kuugua .ndio maana afya njema ya CCM Ndio afya na uhai wa Taifa letu kwa kuwa ni CCM Pekee iliyo na uwezo wa kuliongoza Taifa letu.
Tofauti na mavyama ya upinzani ambayo yanashindwa kuwa na mbadala hata wa mwenyekiti tu wala kuwa na uwezo wa kuandaa ilani yake au kuwa na maono ya urefu wa pua zao tu.zaidi utakachokikuta upinzani kama CHADEMA ni juu ya Usaka Tonge na kung'ang'ania kupata fursa ya kuteuliwa kugombea udiwani au ubunge.
ndio maana ni kawaida kuona vyama kama CHADEMA vikiazima mgombea Urais kutoka CCM ili akapeperushe bendera yake kwa muda tu. jambo ambalo kamwe na katu huwezi ukaliona wala kulisikia wala kuja kuliona likitokea ndani ya CCM Kuchukua mgombea Urais kutoka upinzani ndani ya wiki moja na kumpa nafasi ya kugombea urais wa nchi yetu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Ukubali ama ukatae, uchukie ama ukasirike.utukane ama usonye.ulaani ama ubariki ukweli ni kuwa CCM na Serikali yake ndio bima ya matatizo,kero na changamoto za watanzania.ndio maana mtu akipatwa na matatizo au kuonewa au kunyanyaswa anaangalia wapi kuliko na ofisi ya CCM ama wapi wanapatikana viongozi wa CCM ama amkimbilie Kiongozi yupi wa CCM kupata suluhu ya matatizo yake.
Ndio maana kwa sasa ni kawaida kuona watu kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wakitafuta kwa kila njia namba za viongozi wa CCM ili kufikisha vilio vyao,kwa kuwa wanajuwa viongozi wa CCM Ni wasikivu,wenye huruma,upendo,ukarimu, unyenyekevu,utu,uungwana,utayari na wenye maamuzi ya haraka katika kuwasaidia wanyonge na wenye kuelemewa na mizigo ya shida mbalimbali zinazowasibu.
Lakini pia wanawatafuta na kuwakimbilia CCM kwa kuwa wanajuwa ndio wenye serikali,ndio wenye majibu,ndio wenye suluhisho ,ndio wenye sauti,ndio wenye ufunguo wa kila mlango,ndio wenye amri ya mwisho,ndio watoa maamuzi ndio walio pewa dhamana ya kuongoza Taifa hili na wanajuwa kuwa ukifika na kufikisha kero yako CCM lazima upate tumaini,faraja na tabasamu katika moyo wako.
Ndio maana vijana mbalimbali kutoka maeneo mbalimbali nchini wanaojitolea kwa muda mrefu katika ofisi na maeneo tofauti tofauti wanaikimbili CCM pale wanapoona wameonewa au hawajatendewa haki au kumefanyika upendeleo wa waziwazi wa kuwapatia ajira watu wengine ambao hawakustahili kupata ajira serikalini na kuwaacha wao wakiwa na sifa stahiki.
ambao kwa moyo wa upendo na uzalendo wamekuwa wakifanya kazi bure kwa kujitolea pasipo malipo lakini mwisho wa siku wanaachwa na kuchukuliwa wengine kwa kuwa tu kuna viongozi wa juu katika halmashauri husika wanaoamua kupachika ndugu zao au wale waliotoa fedha kama rushwa na kuwaacha watoto wa maskini wakibubujikwa na machozi kwa huzuni na maumivu makubwa kwa kutotendewa haki na wahusika.
Hii ndio maana unaona Watanzania wengi sana wakiwepo wale wa kutoka vyama vya upinzani wakiwa karibu sana kufutilia kila kinachokuwa kinaendelea na kujiri ndani ya CCM.kwa kuwa kila mtu anafahamu kuwa CCM Ndio Kila kitu katika Taifa letu na kwamba ikipiga chafya tu lazima kila mtu apate mafua na kuugua .ndio maana afya njema ya CCM Ndio afya na uhai wa Taifa letu kwa kuwa ni CCM Pekee iliyo na uwezo wa kuliongoza Taifa letu.
Tofauti na mavyama ya upinzani ambayo yanashindwa kuwa na mbadala hata wa mwenyekiti tu wala kuwa na uwezo wa kuandaa ilani yake au kuwa na maono ya urefu wa pua zao tu.zaidi utakachokikuta upinzani kama CHADEMA ni juu ya Usaka Tonge na kung'ang'ania kupata fursa ya kuteuliwa kugombea udiwani au ubunge.
ndio maana ni kawaida kuona vyama kama CHADEMA vikiazima mgombea Urais kutoka CCM ili akapeperushe bendera yake kwa muda tu. jambo ambalo kamwe na katu huwezi ukaliona wala kulisikia wala kuja kuliona likitokea ndani ya CCM Kuchukua mgombea Urais kutoka upinzani ndani ya wiki moja na kumpa nafasi ya kugombea urais wa nchi yetu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.