Faiza, nakupa hongera za dhati kabisa, nimejaribu sana kukupigia simu sijakupata, kwa bahati nzuri "Gozi" lako likanipigia alfajiri ya leo na kunieleza kuwa kakunyang'anya simu yako na kaizima. I wonder why.
Nikikupa pongezi peke yako itakuwa simtendei haki "shemeji" yangu, Gozi lako, nampa pongezi sana kwa kuidumisha ndoa hii kwa miaka hii yote. Najua kakustahamilia sana, au niseme mmestahamiliana? Nawapa pongezi za dhati.
Jamani wana JF, wakati FF ananiita mimi "Anko" huwa anakosea, mimi si "Anko" wake bali ni "cousin" wake kwa mama, yaani ni mtoto wa mama mkubwa na mdogo, ingawa nimemzidi kidogo tu kwa umri (tumecheza pamoja utotoni) lakini amezoea kuniita anko baada ya kuwa tu watu wazima na nephews wamekuwa wengi kiasi cha kusahaulika jina langu na kuwa ni ama "anko" au mjomba kwa wengi wanaonifahamu, inanshangaza kuwa hata "bi mdogo" (mke wangu wa pili) huniita anko.
Nimeongea hayo, kwa kutaka tu kuwafahamisha kuwa FF namjuwa, sana sana tena sana.
FF, kwa anaemjuwa, ni easy going, fun loving, with a big smile always. Anaependa sana ndugu zake na marafiki zake, yupo tayari kuwatetea awajuao hata kama wana makosa, she will never betray you! Ni mwanamke straight forward hatafuni maneno na siku zote husema, "nichukie kwa ukweli wangu, usinipende kwa uongo wangu".
Katika kukua kwetu jijini Dar. FaizaFoxy, mitaa ya kariakoo (ya late 60's na early 70's) ni maarufu sana kiasi anatisha kufatana nae. Umaarufu wake una kuja mara mbili, kwanza kazaliwa, kasoma na kukulia hapo Kariakoo, pili kaolewa na mtu maarufu sana pale Kariakoo na Dar au Tanzania kwa ujumla, kutokana na shughuli zake, ni mtoto wa Kariakoo tuliye kuwa nae pia.
Kwa miaka mingi tulipoteana na FF baada ya yeye kuolewa na kwenda kuishi nje ya Tanzania kwa muda mrefu sana, ukimuuliza mwenyewe kwanini mliamua kukaa nje miaka yote hiyo? mwenyewe hujibu "tulimkimbia" Nyerere na siasa zake za kukandamizana. Lakini najua ni stihizai zake tu, kama kuna mtu alikuwa akimpenda Nyerere tulivyokuwa tunakua basi sijamuona zaidi ya FF. Sijui kwa nini baada ya kurudi Tanzania akawa hapatani na Nyerere.
FF ni mkimya sana na huwa haongei mengi, mimi nashangaa hapa JF kawa ni mmoja wa "wapayukaji" na saa zingine huwa ananikera, lakini naweza kukisia ni kwa nini. Ntamuachia mwenyewe.
Nna mengi ya kuongelea kuhusu FF lakini itakuwa si vyema nikamsemea, pengine mwenyewe hatopenda kusemewa yake.
Hongera Faiza, Hongera G.
Psss. Hiyo nick ya Foxy, alipewa na kakaetu mkubwa (mungu amrehem), toka utotoni na imeshika mpaka leo, ingawa sana ilikuwa kwa kifamilia tu tunayoijua, nashangaa kukuta anaitumia humu JF, muulizeni mwenyewe ina maanisha nini.