Kuna siku nilikuwa na kaka yangu huko kijijini, kalala usiku ana nguo, aubuhi kaamka hakuna hata moja. Kaamka uchi kabisa.
Kesho yake tumetoka kuwatembelea ndugu (maana ilikuwa likizo), saa mbili kasoro usiku tukapita mti mkubwa sana wa mninga uko barabarani na hapo kuna nyumba za watu wanapika chakula. Chakushangaza hatua kama mbili tulipopita chini ya huo mti moto ukawaka. Tukataka kukimbia lakini tukasita maana niliwahi kusimuliwa ukikuta mauza uza ya namna hiyo usikimbie kwani unaweza kukesha ukikimbia.
Siku ya nne tukarudi zetu mjini. Hatukuwahi kuwaeleza majirani kule kijijini kuhusu tukio hilo.