Biashara ya mtandaoni imeibuka kuwa eneo la fursa mpya nchini Kenya

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
Biashara ya mtandaoni imeibuka kuwa eneo la fursa mpya nchini Kenya

Na Kelvin Isenye Ogome

11111.jpg


Kutokana na ongezeko la matumizi ya simu tamba na za kisasa pamoja na kuimarishwa kwa mtandao, imekuwa rahisi kwa idadi kubwa ya Waafrika kutumia mtandao katika maisha yao ya kila siku, kama vile kupata habari za aina mbalimbali, kujiburudisha, hata kuuza na kununua bidhaa mtandaoni.

Takwimu inaonyesha kuwa, hivi sasa watumiaji wa mtandao nchini Kenya imezidi milioni 43, na biashara ya mtandaoni imeibuka kuwa eneo la fursa mpya za ajira, na kuwavutia wawekezaji wa kigeni nchini Kenya. Kwa sasa majukwaa ya biashara ya mitandaoni yanayojulikana nchin Kenya ni pamoja na jumia , kilimall, jiji, na amambo.

6758657865.jpg
grehryjtykuy.jpg


Joseph Odhiambo, baba ya watoto wawili na mwendeshaji pikipiki za uchukuzi amefika kila pembe ya jiji la Nairobi. Kazi yake ya kuwafishia bidhaa walizoagiza mitandaoni imelazimu kifika kila pembe ya jiji hili na kumkutanisha na watu wa matabaka tofauti.

Kuwepo kwa simu za kisasa na huduma za intaneti kumemuwezesha Bwana Odhiambo na wenzake kujiunga na msururu huu mrefu wa biashara ya kisasa.

Kuwepo kwa fursa za biashara na uwezo wa kununua kumewavutia wawekezaji wa kigeni kuanzisha biashara ya mtandaoni jijini Nairobi na Kenya kwa jumla. Angela Lei ametokea nchini China ambako biashara ya kuuza na kununua bidhaa mtandaoni imepiga hatua kubwa. Lei alianza biashara ya kuuza bidhaa hasa za elektroniki mtandaoni mwaka 2016. “Biashara ya

3333333.jpg

(Angela Lei na Timu yake)

mtandaoni ni tasnia inayoendelea kuongezeka, tangu janga la corona kubisha ulimwenguni, watu wengi zaidi wananunua bidhaa mitandaoni, biashara yetu imenoga, hivi sasa napata zaidi ya wateja 3,000 kwa siku. ” anasema Bi. Angela Lei.

Ikilinganishwa na maduka ya kawaida, kuendesha biashara mtandaoni ni jambo rahisi sana. Mfanyabiashara hahitaji hela nyingi kuanzisha na kuendesha aina hii ya biashara.

Susan wangare, mwanafunzi wa chou Kikuu cha Kenyatta ni miongoni mwa Wakenya ambao wamekumbatia ununuzi wa bidhaa mitandaoni. Kupitia kwa simu yake ya mkononi, Susan anaagiza saa na chakula kutoka duka la Annov. “Leo nimenunua saa na rinda, ni rahisi kununua bidhaa mitandaoni kuliko kusumbuka mjini ukitafuta maduka ya kuuza bidhaa. ”

Biashara hii imeongeza nafasi za ajira nchini kufuatia ukuaji wake wa kasi. Ripoti ya halmashauri ya mawasiliano nchini Kenya CA inaeleza kuwa biashara hii hukua kwa kasi ya 40% kila mwaka. Joseph Odhiambo anakiri kuwa ni kutokana na biashara hii ndipo amefanikiwa kuwapeleka wanawe shule na kukidhi mahitaji yake ya kimsingi “Siwezi lalamika sasa, maisha yangu yamebadilika kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita kutokana na kazi hii. Ona watoto wangu wanaenda shule, siwezi lala njaa kama kitambo”

Kenya, Nigeria na Afrika kusini zinaongoza kwa kufanya biashara ya mitandaoni barani Afrika huku bidhaa nyingi zikiagizwa kupitia kwa simu za mkononi. Nguo,saa, viatu na simu zikiwa baadhi ya bidhaa ambazo huagizwa kwa wingi hapa nchini kutoka maduka kama vile Amazon, Alibaba, AliExpress na Jumia.
 
Tanzania wanakwambia “tunaongeza bundle” “lipa $1000 kabla ya kuupload vide YouTube”.

Alafu unataka tuseme Tanzania kuna watu sio mazombie?

Tanzania imejaa wapumbavu kuliko hata North Korea, magepu yapo makubwa soon hata Uganda itatuacha mbali. Tutabaki na slogan The shithole of East Africa
 
Kuna ripoti niliona mahali kuwa tanzania inaongoza Afrika kwa kutumia simu kwa ku chat na kua galia movie tu
 
Back
Top Bottom