Biashara mtandaoni tunakwama wapi

Jitambuwe

Senior Member
Sep 25, 2011
166
130
Habari ndugu zangu, pole na uchovu wa siku nzima.

Leo nimeona niwasilishe haya mawazo kwa ufupi, ili tuweze kujadili na kuweza kujua nini cha kufanya ili tuweze kuvuka hatua moja kwenda nyingine.

Twende kwenye mada husika

Kwa kipindi kilefu nimejaribu kupitia na chunguza biashara za mtandaoni, nimeona upende wetu hatujaweza kufanya vizuri.
Kuna baadhi ya kampuni zilijaribu lakini hazikufanikiwa. Mfano Jumia Tanzania alifanya biashara hii kama miaka 2hivi nadhani hapa Tanzania lakini akaamua kufunga biashara yake.

Mwingine ni Michongo kutoka Dudumizi hosting nadhani kama sijakosea. Lakini na yeye biashara bado inajivuta flani hivi.

Biashara hii ya mtandaoni maarufu kama eCommerce imeshindwa kuleta ushawishi mkubwa hapa nchini, na kufanya watu wengi kuagiza mizigo yao kwenye tovuti (website) za nje ambapo wanalipia gharama kubwa, kuliko tungekuwa na tovuti zetu ambapo tungeweza kuingizia serikali yetu mapato zaidi.

Kama Tanzania hapa tungeweza kubuni tovuti kama eBay, Amazon au hata kikuu basi. Watu wakaagiza mzigo kutoka China, USA na nchi nyinginezo. Au watu wakafanya manunuzi ya bidhaa za ndani na kulipia kwa TSH kama vile Jumia anavyo fanya. Nadhani tungeongeza thamani furani katika Nchi yetu.

Maana ndani ya nchi yetu hatuna tovuti za kibiashara, kifedha, nanyinginezo. Tovuti nyingi tunazo tumia ni za Nchi nyingine tena malipo kwa card za benki, inaumiza sana.

Njia za malipo tunazo, tena mitandao ya simu imelahisisha.

Je wewe mwenzangu unaona nini kiweze kufanyika ili tuweza kuleta heshima kwenye Nchi yetu?
 
Habari ndugu zangu, pole na uchovu wa siku nzima.

Leo nimeona niwasilishe haya mawazo kwa ufupi, ili tuweze kujadili na kuweza kujua nini cha kufanya ili tuweze kuvuka hatua moja kwenda nyingine.

Twende kwenye mada husika

Kwa kipindi kilefu nimejaribu kupitia na chunguza biashara za mtandaoni, nimeona upende wetu hatujaweza kufanya vizuri.
Kuna baadhi ya kampuni zilijaribu lakini hazikufanikiwa. Mfano Jumia Tanzania alifanya biashara hii kama miaka 2hivi nadhani hapa Tanzania lakini akaamua kufunga biashara yake.

Mwingine ni Michongo kutoka Dudumizi hosting nadhani kama sijakosea. Lakini na yeye biashara bado inajivuta flani hivi.

Biashara hii ya mtandaoni maarufu kama eCommerce imeshindwa kuleta ushawishi mkubwa hapa nchini, na kufanya watu wengi kuagiza mizigo yao kwenye tovuti (website) za nje ambapo wanalipia gharama kubwa, kuliko tungekuwa na tovuti zetu ambapo tungeweza kuingizia serikali yetu mapato zaidi.

Kama Tanzania hapa tungeweza kubuni tovuti kama eBay, Amazon au hata kikuu basi. Watu wakaagiza mzigo kutoka China, USA na nchi nyinginezo. Au watu wakafanya manunuzi ya bidhaa za ndani na kulipia kwa TSH kama vile Jumia anavyo fanya. Nadhani tungeongeza thamani furani katika Nchi yetu.

Maana ndani ya nchi yetu hatuna tovuti za kibiashara, kifedha, nanyinginezo. Tovuti nyingi tunazo tumia ni za Nchi nyingine tena malipo kwa card za benki, inaumiza sana.

Njia za malipo tunazo, tena mitandao ya simu imelahisisha.

Je wewe mwenzangu unaona nini kiweze kufanyika ili tuweza kuleta heshima kwenye Nchi yetu?
Nadhani upo kwenye zoezi la awali kumiliki website yako utoe huduma ya e-commerce. Soko la mtandao kwa nchii hii ni pasua kichwa. Sina mengi sana, atajazia Masokotz mana yeye mara ya mwisho alivimba na kusema timu yake Iko mezani 😆
 
Biashara za mtandaoni tunakwama hapa:-

1. UTAPELI
Biashara nying za mtandaoni zinaendeshwa kitapeli tapeli.
Anajitokeza mtu anatengeneza website kama ya jamii forum, kumbe sio.
anatangaza bidhaa zake unazikubali ,mnaingia makubaliano mpaka pesa unamtumia.Kam advance, Mwisho wa biashara unaambilia hamna.

Web nyingi znazojinasibisha na biashara mtandaoni nying zinamilikiwa na wezi tu na wapo online kukusubir ww kukupa Huduma.

Wanapost bidhaa nzur zikuvutie, ukiingia ktk 18 zao umekwisha.

2.GHARAMA
Biashara za mtandaoni, zina gharama sana, kuanzia kuiendesha kwake biashara na mteja kuipata bidhaa.

KUBWA ZAIDI NIUTAPELI.
 
Wale Jumia waliiweza sana iyo biashara mi nahisi walitofautiana na magufuli kwene ishu za kodi ila walikuwa poa sana. unapata kitu ulichoagiza na wanakuletea kwa wakati popote ulipowaambia wewe. kuondoka kwa wale jamaa kulikuwa anguko kubwa sana kwa biashara ya mtandao maana hata ajira walitoa sana kwa vijana wa mauzo, waendesha kirikuu ...

mtu mweusi hlf awe mzawa hawezi hio biashara maana janjajanja nyingi na uaminifu ni sifuri
 
Nadhani upo kwenye zoezi la awali kumiliki website yako utoe huduma ya e-commerce. Soko la mtandao kwa nchii hii ni pasua kichwa. Sina mengi sana, atajazia Masokotz mana yeye mara ya mwisho alivimba na kusema timu yake Iko mezani 😆
Kumbe Nilivimba??Any way nitarudi hapa na minofu kadhaa muda sio mrefu...
 
Ndugu yangu,
Kwanza niweke wazi kwamba IKO Project ya e commerce ambayo ni Local na ya Kitanzania ambayo ni matumaini yangu kwamba itakuwa ya kipekee ingawa bado ni mapema kuanza kuiweka sokoni.

Biashara ya Mtandaoni inafanyika sana Tanzania.Hata hivyo ufanyikaji wa biashara hiyo bado unafanyika offline na zaidi kwa kutumia TRUST network.Ndio maana inakuwa ni rahisi sana mtu kutapeliwa kwa kuonyeshwa vitu vya BEI rahisi hali inayopelekea mtu kufikiri amepata kumbe amapatikana.

Changamoto za kuanzisha Ecommerce kwa Tanzania ni nyingi ikiwamo
  1. Mfumo wa kikodi
  2. Mfumo wa kijamii na kiuchumi
  3. Suala a elimu na uelewa.
  4. BIMA ya kudhamini Biashara ya Mtandaoni IPO?
  5. Je Mfumo wa kusimamia Malipo ambao ni nafuu na
  6. Pia ni suala zima la mfumo wa logistics na
  7. Huduma kwa wateja.
  8. Uzalishaji wa Bidhaa
  9. Ubora wa Bidhaa

Biashara nyingi za mtandaoni bado hazijaweza kusimama vizuri kwa upande wa Tanzania kwa sababu bado masuala hayo hapo juu hayajaweza kusimama ipasavyo kwa sababu hayo maeneo hapo juu yanahitaji kushughulikiwa.Ili kuweza kushughulikiwa yanahitaji mifumo imara ya Tehama ambayo inahitaji uwekeza katika fedha na rasilimali watu ili kutengenezwa.

Watu wengi sana wanauza bidhaa na huduma kwenye mitandao ila bado kunahitajika platform ambazo zitakuwa innovative ili kuongeza imani ya wanunuzi na ubora wa huduma.

Kuna mengi yakuelezea ambayo Ndio tunajaribu kuyashughulikia katika mfumo ambao tunautengeneza,hata hivyo changamoto zipo na ndizo zinafanya tuzidiki kufurahi tunachokifanya.

Tuendelee na mjadali.Natumaini kwamba Kalaga baho na Jitambuwe mtakuwa mmepata kitu fulani.Bado sijapata MVP ila huenda PILOT Stage ikaingia Sokoni kwenye Robo ya kwanza Mwaka huu wa 2024.
 
Ndugu yangu,
Kwanza niweke wazi kwamba IKO Project ya e commerce ambayo ni Local na ya Kitanzania ambayo ni matumaini yangu kwamba itakuwa ya kipekee ingawa bado ni mapema kuanza kuiweka sokoni.

Biashara ya Mtandaoni inafanyika sana Tanzania.Hata hivyo ufanyikaji wa biashara hiyo bado unafanyika offline na zaidi kwa kutumia TRUST network.Ndio maana inakuwa ni rahisi sana mtu kutapeliwa kwa kuonyeshwa vitu vya BEI rahisi hali inayopelekea mtu kufikiri amepata kumbe amapatikana.

Changamoto za kuanzisha Ecommerce kwa Tanzania ni nyingi ikiwamo
  1. Mfumo wa kikodi
  2. Mfumo wa kijamii na kiuchumi
  3. Suala a elimu na uelewa.
  4. BIMA ya kudhamini Biashara ya Mtandaoni IPO?
  5. Je Mfumo wa kusimamia Malipo ambao ni nafuu na
  6. Pia ni suala zima la mfumo wa logistics na
  7. Huduma kwa wateja.
  8. Uzalishaji wa Bidhaa
  9. Ubora wa Bidhaa

Biashara nyingi za mtandaoni bado hazijaweza kusimama vizuri kwa upande wa Tanzania kwa sababu bado masuala hayo hapo juu hayajaweza kusimama ipasavyo kwa sababu hayo maeneo hapo juu yanahitaji kushughulikiwa.Ili kuweza kushughulikiwa yanahitaji mifumo imara ya Tehama ambayo inahitaji uwekeza katika fedha na rasilimali watu ili kutengenezwa.

Watu wengi sana wanauza bidhaa na huduma kwenye mitandao ila bado kunahitajika platform ambazo zitakuwa innovative ili kuongeza imani ya wanunuzi na ubora wa huduma.

Kuna mengi yakuelezea ambayo Ndio tunajaribu kuyashughulikia katika mfumo ambao tunautengeneza,hata hivyo changamoto zipo na ndizo zinafanya tuzidiki kufurahi tunachokifanya.

Tuendelee na mjadali.Natumaini kwamba Kalaga baho na Jitambuwe mtakuwa mmepata kitu fulani.Bado sijapata MVP ila huenda PILOT Stage ikaingia Sokoni kwenye Robo ya kwanza Mwaka huu wa 2024.
One of the bigger mistake watu wanafanya hapa ni kuanza kufikiria uwepo wa App kwanza. Uliwahi kuwa winga?
Mana experience ya uwinga ni kuuuza huduma hii, kutangaza bidhaa za mtu kupitia mtandao. Kuna jamaa sinza wamekatiza kariakoo kufanya model ya kuuza machimbo ya bidhaa. It can not be genuine good kama itaanza na kuuza kila kitu
 
Back
Top Bottom