Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,018
- 20,489
Mbona mnakuwa wajinga na wazushi hivi? Kusoma hujui ndugu?
we mwehu nini? mimi nimeuliza swali na nimeona kwenye ukurasa wa Yericko Nyerere kule facebook, so nimeuliza kupata uhakika, wewe unaniambia niache uzushi.
Mwehu ni ww ubateleta habari ya jana ambayo mbaya zaidi in uzushi bila tone la aibu wala tone la utafiti umekimbilia ku post uporo!
Hii habari ni ya jana na kwamba waliofariki ni watu wawili kutokana na ajali hiyo lkn si ben saanane kama ulivyokurupuka.
Pole rudi usingizini.
Mbona mnakuwa wajinga na wazushi hivi? Kusoma hujui ndugu?
Asante kwa taarifa ndugu, nimekuta kwenye ukurasa wa Yericko Nyerere anasema wote wamefariki.
[h=5]Yericko Nyerere
[/h]23 hrs · Edited ·
Habari tulizopata muda huu ni kuwa Ben Saanane amepata ajali mbaya eneo la Maili moja Kibaha wakielekea Rombo Kilimanjaro kwa ajili ya kampeni pamoja na Marafiki zake wawili .
Gari inayomilikiwa na Allan Meshili aina ya Prado T377ACG iligongwa na gari nyingine na kupoteza mwelekeo kisha ikavaana uso kwa uso na gari ya aina ya scania ya mafuta.
Kuna watu wapo eneo la tukio watatutumia taarifa zaidi
UPDATES:
Taarifa yakusikitisha nikuwa wale walipata ajali sambamba na Ben wamefariki dunia mda huu
Na hapo chini ni maneno ya Bob Chacha Wangwe
Bob Chacha Wangwe Ben Wa Saanane
Ni muda mchache uliopita nilikua nanyi,tukicheka
,Kutaniana na kupeana moyo katika ndoto zetu
Allan Patrick Meshili ,Umetangulia.Umeniacha rafiki
yako uliyeniahidi utakua nami hadi tone la Mwisho.
Umeniachia msiba mkubwa Moyoni.Sijawahi kuwa
na Rafiki wa Kweli kushinda kipimo chako
Allan.Umetimiza Ahadi yako hadi Pumzi yako ya
Mwisho
Faith Makundi,Nilihama siti ya mbele nikahamia
kiti cha nyuma ili nisome kitabu ulichoniletea kama
zawadi "Banker to the Poor"-Profesa Muhammad
Yunus .Uliniahidi kutumia likizo yako kuhakikisha
kipindi hiki tunapanga na kutekeleza yote
tuliyokubaliana hasa proposal yangu ya kutumia
vikoba phasewise na kuanza mchakato wa
kutengeneza network kwa ajili ya kuanzisha Benki
ya Maendeleo ya Watu wa Rombo.Ulinishawishi
nichukue likizo pia kipindi hiki kama wewe na Allan
kabla hujarudi Afrika Kusini .Tulienda Rombo kwa
ajili ya kampeni lakini pia kupata practical
experience ya hali ya Rombo
Sasa mmetangulia,bado nichukue Likizo kwa ajili
ya nini sasa?
Washirika wangu,watu muhimu katika safari yangu
nimewapoteza kwa mkupuo mbele ya Macho
yangu.
Sitamkufuru Mwenyezi Mungu,Ana mipango yake.
Ni machozi ya uchungu,Sina wa Kumlilia zaidi
yako wewe Mwenyezi Mungu uwalaze pema peponi
Allan na Faith
Familia zinahuzunika na kuwalilia.Ni msiba
mkubwa kwetu sote
Nahisi Moyo wangu unazimia kwa huzuni.Ni
uchungu mkali Moyoni.
Asanteni Makamanda mlioahirisha safari zenu na
kuungana nami hadi Muhimbili.Mlinitambua kwa
Tshirt ya M4C mkaungana nasi hadi muda huu
tunapotoka Muhimbili.Wapo marafiki zangu wa
kwenye mitandao # Gabriel na Mkewe # Joyce
Mungure.Asanteni sana
Namshukuru Mungu kwa kuniponya katika ajali
hii....!Ni wewe pekee Unayejua kwanini
umeniponyakatika ajali hii ya tatu katika maisha
yangu .Sitakuhoji...!
Kwa leo sina mengi ya kusema.
Mungu awabariki wote mlioungana nasi Muhimbili
na marafiki wote mlioko Mbali
Jina la Bwana lihimidiwe !
Mbona mnakuwa wajinga na wazushi hivi? Kusoma hujui ndugu?
Waliopata ajali na Ben ndio wamefariki. ....
Duhh mungu ailaze roho yake mahali pema peponi kma ni kweli lakin.
Kaka lawama zote naziweka kwako, unajua umetumia ksiwahili kigumu kwenye kupost swala nyeti. Umesema
" Taarifa yakusikitisha nikuwa wale walipata ajali sambamba na Ben wamefariki dunia mda huu" Hilo neno sambamba ndo limenichanganya hapo. Plus maneno ya Bob Chacha wangwe akisema " Ben Wa Saanane
Ni muda mchache uliopita nilikua nanyi,tukicheka,Kutaniana na kupeana moyo katika ndoto zetu ".
Anyway nimekosea, niwieni radhi sana. Moderator, naomba muuondoe uzi huu.
Kumbe na wewe fyatu sikujua nazidi kukujua zaidi kweli nyie ndio ile mizigo ya kutoswa baharini.
Kaka lawama zote naziweka kwako, unajua umetumia ksiwahili kigumu kwenye kupost swala nyeti. Umesema
" Taarifa yakusikitisha nikuwa wale walipata ajali sambamba na Ben wamefariki dunia mda huu" Hilo neno sambamba ndo limenichanganya hapo. Plus maneno ya Bob Chacha wangwe akisema " Ben Wa Saanane
Ni muda mchache uliopita nilikua nanyi,tukicheka,Kutaniana na kupeana moyo katika ndoto zetu ".
Anyway nimekosea, niwieni radhi sana. Moderator, naomba muuondoe uzi huu.
Mkuu FF inanikumbusha kipindi kile baada.ya.jamaa kushindwa kumuwekea sumu prezidaa Zitto na Habib Mchange walipokuwa hotelini Moro kuelekea Iringa jamaa walilegeza stud za tairi la gari wakijaribu kummaliza kwa njia ya ajali.
Mambo ya kulishana sumu yanatoka wapi hapa? Katika kipindi kigumu ni vizuri kuweka propaganda pembeni dada! Kama alitaka kumlisha huyo mshirika wako sumu mbona hukumpeleka mahakamani?