Ben Saanane anavyoteseka na kivuli cha unafiki...

Ben Saanane anavyoteseka na kivuli cha unafiki...

Adha ya vijana kutumika kuchafua watu ndio hii?
Umewahi msikia Ben saanane kwenye mkutano wowote?au M4C yoyote ya kichama?
Unamisikiaga hapa kwenye usaliti,mara TISS n.k hii ndio kazi ya Ben saanane pale chadema.......

Kazi uliyopewa ni ngumu sana.
 
Naomba msaada yeyote aniwekee ule uzi uliomuibua Ben saanane na usaliti wake kule india kwa watanzania wenzetu na kukimbia na hela........

Kaka leo umekamatika utahangaika sana ila tushakujua mapemaaa kua we mbeba tunguri za Zitto.
 
Mkuu changia mada. Mimi sio CCM ila nina kadi niliyoitunza kwa kumbu kumbu kama anavyofanya slaa........

Ishu ya kadi sio ya msingi hapa,wanaoijadili ni wapuuzi tu...CHADEMA inahitaji commitment sio karatsi ya karatasi...Endeleeni kuwapa vichwa hao vilaza...

Mi nimempa ushauri tu wa kujitafakari hasa pale watetezi wake wanapokuwa wewe,Ritz ,Rejao,Upiu na Chama......Tunachoshukuru sisi sasa Mungu amewaumbua wasaliti hawa akiwemo Ben,Zitto,Juliana,Mchange,Mwampamba na wengine.Ukweli huushinda uongo daima.
 
Hivi huko CHADEMA hakuna mtu uwezo wa kuwakanya hawa "vijana" waache haya malumbano kwenye hii mitandao?.......

Nyani Ngabu: Waliotakiwa kuwakanya wamewagawa katika makundi, kuna vijana wanaothaminiwa michango yao na vijana wengine hawana thamani yeyote mbele ya watu hao.

Kama Dr. Mkumbo aliingilia kati yakashindikana unategemea nini. Mimi nadhani watu kama nyinyi( wewe, Mzee mwanakijiji etc) wasio na upande labda mkiitwa mnaweza mkatatua mgogoro huu.
 
Lakini ninyi hapa mna mu attack Ben kwa kusema tu kwamba amesema uongo? Hamjajibu hoja zake.Mwenzenu yuko tayari kwenda kwenye vikao vya chama.Ninyi mnakimbia kivuli chake na leo mmetumwa na Zitto kuja huku kwa kasi kumtetea.Ben has evidence,nilitegemea kama una busara kama makamu m/kiti BAVICHA.Ungeenda kupeleka suala hili kwenye Chama.Swali,Kwa nini ulikua kwenye kikundi hicho,na mission yenu ilikuwa nini?........

Kama Ben ana evidence(ujumbe wa kurekodi aliotumwa aufanye) si apeleke mbele ya chama.

Hapo ndipo utakapo sikia nani ni mnafiki.Jana nasikia makamu Mwenyekiti Taifa ametupa kadi ya chama chini.Anatajka kuidhuru,chadema kipo tena????
 
Muulize Ben saanane walionana wapi na zitto(eneo) waliongelea nini??
Mamuya amesewa walipo onana na zitto,Je ben walionana wapi?
Akikujibu hili swla njoo hapa nikupe zwadi.Ben ni mnafiki na mwongo wa kimataifa

kwanini Zitto alimpigia simu Kitila ili Ben aje akanushe yaliyoandikwa na Mamuya???

kwanini hamjakanusha shutuma zilizotolewa na Mamuya na Ben badala yake mnajikita katika kumshambulia Ben???

unaonekana umejitolea kufa na kupona kuwatetea(kujitetea)
 
Nyani Ngabu: Waliotakiwa kuwakanya wamewagawa katika makundi, kuna vijana wanaothaminiwa michango yao na vijana wengine hawana thamani yeyote mbele ya watu hao. Kama Dr. Mkumbo aliingilia kati yakashindikana unategemea nini. Mimi nadhani watu kama nyinyi( wewe, Mzee mwanakijiji etc) wasio na upande labda mkiitwa mnaweza mkatatua mgogoro huu.

Viongozi wa juu wanasuka hizi dili za kuchafuana mitandaoni na alipo yanafanyika kihalali kabisa pale makao makuu.Unategemea nini?
Lakini vita hii ya kusi na kasi itafika mwisho
 
I don' t know why
I keep believing
That one day, they' ll bring us together
When they' ve shown
In more ways than one
That all they care about is the TSHS.
KWAHERI CHADEMA CHAMA KINA WENYEWE HIKI.
those who tried to bring us together also brought this poverty and corruption we witness today, may be these have different vision of splitting us into 'manageable groups' hence see if we can move forward. For sure Africa has got a lot to do!
 
hizo ni akili za abunuasi, kwani kipindi mnaanzisha kile kikundi chenu cha MP7 zitto alikuwa tayari ameshatangaza nia ya urais?
Jibuni hoja za kijana Ben acheni uingiza watu wasiohusika kwani mliyafanya gizani sasa mchana kweupe yamewekwa.

TULIANZA NA MUNGU NA TUTAMALIZA NA MUNGU.

ukiweka ushabiki pembeni ,hebu jiulize huyo ben pesa ya kuwa PAYMASTER wa kikundi hicho alikua anatoa wapi na waliokuwa wakimpa walimpa kwa malengo gani.
Kumbuka kwa mujibu wa machage kipindi hicho ben akifanya juu chini kumnasa zito ili awe anawafadhili na zito akawa anateleza hakamatiki.
Hapa pia inatakiwa huyo ben atuambie au kuonyesha kama aliwahi kumnasa huyo zito.
 
kama ben anasema amerudi kundini baada yakuwa muasi basi anatumia uwongo ule ule aliokuwa anautumia wakujirekodi yeye mwenyewe mipango na mikakati yake na kisha kuwapelekea wahusika kwamba ni mipango ya masalia kuvuruga chama.that is nonsense

Kuna ubaya gani wa kurekodiwa kama kulikuwa hakuna la siri mlilokuwa kuwa mnaliongelea? Kungekuwa hakuna kitu cha kufanya mrekodiwe, hakika asingeweza kufanya hivyo maana hiyo habari isingeuzika.. Mmekuja na utetezi wenu lakini hauna mashiko.. Nendeni mkajipange upya!
 
tusipokua makini kwenye hii movie stearling atapotea badala ya kufa kama tunavyotegemea tutoe michango yenye staha ili stearling ajitokeze auwawe.
 
Mtiririko wa hizi story nauita Chapters za Kitabu kiitwacho "Kuibuka na Kuzama kwa Upinzani wa ndani ya Chadema"
Najisikia fahari sana kuona kuwa pamoja na upinzani wote huu wa ndani ya chama, Mwenyekiti Mbowe na Katibu Dr Slaa wamesimama kidete bila kutetereka, nastareheshwa na namna waumini makundi haya ya upinzani wa ndani wanavyofunguka wenyewe bila kulazimishwa wala kushurutishwa. Naamini kauli mbiu ya kimapambano inayoongoza harakati za Taasisi ya Chadema "Peoples Power" kuwa ni kauli iliyoasisiwa na Mungu Mwenyewe, maana endapo ingeasisiwa na fikra za kibinadamu hakika isingeweza kukabiliana na upinzani huu.

Kwa mujibu wa historia, jambo lolote jema hupata upinzani wa ndani. Kabla ya TANU palikuwapo vyama vingine kama AA. TAA nk, lakini watu walijitenga navyo na kusonga mbele. Wapinzani wa ndani ya chadema nao wanafuata mkondo ule ule wa historia ili maandiko yatimie kuwa HAKUNA wa kuidanganya historia, wala hakuna wa kujidanganya mwenyewe na katu hakuna wa kumdanganya shetani hata wanafiki wanaotajwa na Quarani.

Chadema_Peoples Power_God's Voice

Long live chadema

Naona unajiliwaza na kujifariji mkuu.
 
Kama Ben anaevidence(ujumbe wa kurekodi aliotumwa aufanye) si apeleke mbele ya chama.Hapo ndipo utakapo sikia nani ni mnafiki.|
Jana nasikia makamu mwenyekiti taifa ametupa kadi ya chama chini.Anatajka kuidhuru,chadema kipo tena????

Amesema atapeleka...anajiamini sana kuliko nyie mnaongea tu hamjulikani mna hoja gani tangible zaidi ya kusema oooh unafiki....Mwenzenu kataja hadi tunguli mlizobeba.Ishu ya Arfi ni ndogo na ya kawaida,yule ni mzee mwenye busara,hana mihemko kama nyie....Nijibu mlichukua hatua gani baana ya kugundua ben ana nia mbaya na chama? na je matusi yenu kule fbuk mlitumwa na Ben?
 
Nyani Ngabu: Waliotakiwa kuwakanya wamewagawa katika makundi, kuna vijana wanaothaminiwa michango yao na vijana wengine hawana thamani yeyote mbele ya watu hao. Kama Dr. Mkumbo aliingilia kati yakashindikana unategemea nini. Mimi nadhani watu kama nyinyi( wewe, Mzee mwanakijiji etc) wasio na upande labda mkiitwa mnaweza mkatatua mgogoro huu.
Siasa za kukimbilia majukwaani na kujitafutia sifa binafsi kwa viongozi vimewafikisha hapa CHADEMA,ombwe la uongozi linahitajika kuokoa jahazi lisizame.
 
Mlikuwa wapi siku zote hizo msiyaseme hayo hadi msubiri Ben aje kuwaumbua hapa? na baada ya siku mbili ndio mnajipanga kuja kumchafua badala ya kujibu hoja zake?

Hivi mnajua hiki mnacho kifanya sasa nia hatari zaidi kwa upande wenu kuliko Ben? Ben ameonekana hapa kuwa smart zaidi yenu na hata hivi viroja mnavyo kuja navyo sasa inathibitisha uwezo wenu mdogo mlionao...

Hivi mbona BEN ajakana hilo?
Amekiri kuwa alikuwa mmoja wa wanakikundi, na kwa sasa amesaliti na wote tunalijua hilo kupitia humu kuwa kulikuw akuna kikundi ila hatukujua ni wakinanani wapo huko na wanafadhiliwa na nani?
na mapka sasa hatujajua labda waje hapa hao PM7 watuambie mfadhili wao ni nani?
ni nani aliye wapa vifaa vya rtekodiana maana inaonekana hili kundi lilikuwa likikutana na wote wanakuwa wapo full nondo kila mtu ni shushu na kifaa chake cha kurekodia wenzie.
 
Back
Top Bottom