Ni kwa sababu niliipima akili yake na kujua anachokitaka, na nisingeweza kumkimbia mapema kwa sababu angewasingizia mambo mengi sana wenzake.
Mpaka sasa baadhi ya viongozi wa chama wananichukia sana mimi, wanamchukia mwampamba na wengine, lakini hii ni kwa sababu ya uwongo waliokuwa wakilishwa na SAA NANE, yeye alikuwa anatuita tupumzike ama tupige story, halafu anakibadilisha kinakuwa kikao cha mikakati ya PM7 halafu anaanzisha maada za kujadili kisha anawarekodi na kupeleka kwa hao baadhin ya viongozi, masikini ya mungu viongozi wetu wanaamini na kuanza kuwaona wenzao waongo nakadharika.
Hii ni aina mbaya sana ya kufanya strugle, sisi hapa adui yetu ni CCM tu, tunavyopoteza muda kurekodiana wenyewe kwa wenyewe haisaidii kitu.
Muda alioutumia SAA NANE kuturekodi ili akauze habari angeutumia kufanya maswala ya msingi kwa chama hakika tungezidi kuwa mbali.
Lakini ndio hivyo tena njia ya mwongo fupi, na kila kitu sasa kipo hadharani.....NAENDELEA KU-COMPILE MANENO YAKE NILIYOMREKODI AKISISITIZA UANZISHWAJI WA PM7 NITAYAWEKA HUMU KILA MTU AMUELEWE SAA NANE NI NANI
Binafsi naona unanipa maswali mengi zaidi ya majibu, tafadali nisaidie ufafanuzi kidogo hapa mkuu
Hapo pa zambarau, naona umejibu kwa hoja dhaifu sana, kwa hiyo ulihudhuria ili uwatetee wenzio wasisingiziwe sio?! mbona umesubiri hadi yamekuja haya ndio ukajitokeza? unadhani huku ni kutetea watu ama kujitetea? Uzuri Ben kakiri kabisa kuhusu usaliti wake, wewe unasema eti ulimsoma akili yake ndio maana 'ukashirikiana nae' ila sijui kwanini yeye ndo kawa wa kwanza kuja kuwalipua humu maana kwa tafsiri ya maneno yako ulipaswa kuwa wa kwanza kufuchua mipango yake!?
Hapo pekundu, mtu akianzisha topic ambayo kwa ufahamu wako unaona ni usaliti na unafiki kwa viongozi na chama chako kwa ujumla, mchango wako katika hiyo mada unakuaje? Unapinga? au unaonesha jinsi ya kuufanikisha? maana naona unavyosisitiza juu ya kurekodiwa inaonekana unaelewa extent ya content ya usaliti wenu.
Hapo pa bluu, inaonekana maongezi ya vikao vyenu yalikuwa na uchangiaji ambao una'content iliyo na 'bei' nzuri, na ndio maana ukaweza kuwasilishwa kwa huyo mtu (aliyemtuma labda, kama yupo), ila pia inaonekana kila mmoja wenu ana hofu na kiasi gani kitatolewa kwenye forums kama ushahidi wa uhusika wenu, ndio maana mnakuja nusu nusu.
Binafsi naona kwa kuwa hamkuweza kupinga tokea wakati mnaanza vikao, mkaunda umoja na kupeana majina, mkahudhuria vikao na kupanga mipango kwa siri kuhujumu chama chenu wenyewe na chetu sote wapenda mabadiliko, huu ni usaliti mkubwa sana, na najua mlipaswa kulijua hili toka mwanzo.
Roho inaniuma sana, wananchi wapenda mabadiliko wanachanga shilingi mia tano, elfu,sio kwa kuwa wanazo nyingi, hapana, ila wanajitolea kuleta mabadiliko hasa baada ya kuchoshwa na hali waliyolazimishwa kuwa nayo kwa miaka mingi, leo hii tunagundua kuwa kati ya wale tuliowaamini kuwa wako mstari wa mbele wanashirikiana na adui kutuuza!!
Dhambi hii haitawaacha salama, Muda utaongea.