Miji mingi kwa sasa imebadilika hapa Tz, japo utamaduni wetu wa kutojali mazingira unatuangusha. Yani barabara mpyaaaa, lakini, uzuri utabaki kwenye hiyo barabara tu, makazi na shughuli zingine bado zinachukiza miji yetu. Hakuna bustani za kutosha, pia unakuta barabara zina sehemu ya maua ama nyasi au miti, si watumiaji wala mamlaka husika wanaojali. Hapo usisahau mabanda ya maduka yasiyopangwa, mama ntilie n.k, duka linaanzia ndani ,vitu vinapangwa hadi barabarani. Yani unaingia mjini utasema pamepigwa mabomu.