Geza Ulole
Wizara ya Uchukuzi Miradi ya Ujenzi wa Viwanja vya ndege na Ukarabati
1. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mwanza
katika mwaka wa fedha 2026/27, mradi huu umetengewa Shilingi bilioni 6.0
2. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Arusha
Mradi huu umetengewa Shilingi bilioni 3.08 fedha za ndani katika mwaka wa fedha 2026/27.
3. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mtwara
Mradi huu umetengewa kiasi cha Shilingi bilioni 3.48fedha za ndani katika mwaka wa fedha 2026/27
4. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Serengeti
Mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi milioni 100.0fedha za ndani kwa ajili ya kuratibu maandalizi ya utekelezaji wa Mradi.
5. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Mkoa wa Kagera
Katika mwaka wa fedha 2026/27,Mradi huu umetengewa Shilingi bilioni 1.9fedha za ndani
6. Mradi wa Ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro – KIA
Ukarabati wa kiwanja hiki umetengewa Shilingi bilioni 32.0fedha za ndani katika mwaka wa fedha 2026/27
7. Mradi wa Uboreshaji na Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA)
Katika mwaka wa fedha 2026/27, Serikali imetenga jumla ya Shilingibilioni 26.75 fedha za ndani
8. Mradi wa Uendelezaji wa Viwanja vya Ndege vya Mikoa
Katika mwaka wa fedha 2026/27, Mradi huu umetengewa jumla ya Shilingi bilioni 14.38 fedha za ndani
Ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Lindi;
Ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Moshi;
Ujenzi wa jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Musoma;
Ukarabati na uboreshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Singida;
Ufungaji wa mfumo wa taa za kuongozea ndege katika Kiwanja cha Ndege cha Mafia;
Ununuzi wa magari mawili ya zimamoto kwa ajili ya viwanja vya ndege vya Shinyanga na Sumbawanga;
Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Njombe kutokana na uwepo wa mazao ya mbogamboga, matunda na maua.