kadoda11
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 21,453
- 20,755
kwanza zanzibar jana niliwasikiza wachezaji kadhaa wakizungumza ,kiswahili chao ni kama cha mombasa kabisa,...Kadoda mbona mnazungumza tofauti na waunguja + wapemba
seronga kajibu vizuri sana...ukweli ni kwamba kila eneo la tz lina lahaja yake ya kiswahili kutokana mchanganyiko wa lugha za kienyeji za eneo husika.
pwani karibia yote ya tz ikiwemo visiwa vya zanzibar ina lahaja yake ya kiswahili.
kwa namna fulani,waswahili wa pwani ya tz wanazungumza kiswahili kinachoshabihiana na kiswahili cha wakenya wa mombasa.
kiswahili cha kinzibar pia kinatofautina.mfano kiswahili anacho zungumza mpemba kinatoutiana kidogo na kiswahili cha waunguja.