Kati ya Uwekezaji nilikuwa nausubiri kwa hamu ni ujenzi wa hotel ya kisasa eneo hilo, lile eneo linaenda kuwa very strategic na hakuna kabisa hotel, TANTRADE walitaka kujenga hotel nzuri pale Sabasaba na kuboresha exhibition grounds ziwe na international standard ili kuvutia international exhibition lakini nilishangaa sana JPM aliwakatalia plan yao na walikuwa wameishapata na funding kabisa.
Niliwahi kuwa na wateja wamekuja kwenye maonesho walishangaa sana eneo hilo kukosa hotel nzuri ya kulala, walisema Bongo bado hatujui kuexplore the potentials we have, maonesho yetu ni moja ya maonesho makubwa sana Afrika haiwezi kuwa shaghalabaghala namna hiyo, so finally pale tunapata hotel, hope TANTRADE nao watakuja kivingine na exhibition grounds zao, miundombinu ya BRT mizuri kabisa, pale sasa pageuzwe Centre ya maana ya sports and functions.