.
Yaani wewe huna hata miezi mitano hapa JF unajifanya mjuaji hivyo? Usiwe na akili za mbayuwayu, jaribu hata kuangalia mada za mwazo mwanzo za hii Kenyan forum uone zilianzishwa na nani. Kwa taarifa yako tuu; vagi letu na nyinyi lilianza miaka ya kati hapo hasa 'Gezaulole' alipolianzisha kwasababu ya baadhi yenu kujifanya wajuaji .
Kabla ya hapo habari za kenya zilikuwa zikibandikwa 'international forums' na Watz, baada ya kuchoka kujadili siasa za ndani. Watu walipumzika 'international forums' kujadili mada mbalimbali za nje ya Tz, Wakenya wengi kama wakina 'smatta', 'Ab_Titchaz' na 'nomasana' tulikuwa tukijadiliana kishkaji na utani wa hapa na pale, hakukuwa na majigambo wala matusi (ni kama tunavyojadiliana na mwenzenu 'MK254').
Tatizo ni baadhi yenu watu wa ushagoo mliojifunza kutumia mitandao jizujuzi na kutoa tongotongo ndo mnatokwa na mapovu hapa, sitashangaa kama mmejifunza haya mambo ukubwani na kufikiri dunia yote inaizunguka Nairobi.