Bantugbro
JF-Expert Member
- Feb 22, 2009
- 4,473
- 4,254
Wee Edward ni mwalimu wa skuli ya namna gani usiyejua hata historia ya Afrika?Iko Europe!? Dewji (Mo) ni muhindi and he owns Tanzania!!!!
Tanzania ni nchi yenye raia wa rangi mbalimbali, weusi, wazungu, washirazi, wahindi, wasonjo etc.
Huyo MO unaye mzungumzia hajui nchi nyingine zaidi ya Tanzania. Ancestors wake walikuja kabla hata nchi yetu haijaitwa Tanzania, enzi hizo za Tangayika na Zanzibar.
FYI chama tawala Tanzania kilitokana na muungano wa vyama viwili, TANU na Afro-Shirazi Party (ASP).umeshawahi kujiuliza kwanini Ma-Afro na Ma-Shirazi waliamua kukaa pamoja na kuunda chama cha ASP ili kudai uhuru wa nchi toka kwa Mkoloni Mwarabu huko Zanzibar?
Na baadaye wakaungana na TANU ya bara ili kuunda CCM?
Siku nyingine usiropoke tena juu mambo usiyojua vizuri.