Yaan Kenya nyie uchumi huo mliokuwa nao ni ule ule mliochukua kutoka kwa Mkoloni, hakuna mlichofanya zaidi kuendelea nao tena mkaupoza na spidi. Kitu kilichofanya muda wote huu mtusumbue Africa mashariki tulikosa uongozi bora.
Maana kama mngekuwa na uchumi bora isingewezekana JPM aje apindue Meza kwa miaka 5, yaan haiwezekani ina maana muna uchumi mbovu siku nyingi sema mlipata advantage kupitia uongozi mbaya tuliokuwa nao lakini sasa mumeanza kuona moto.
Yaani Miaka 5 tu, Maendeleo ya TZ yamewafyekelea mbali, je ikifika 10yrs or 15 yrs or 20yrs itakuwaje...na kwa mwendo huo wa uchumi wenu na uongozi wenu wa ovyo uliojaa Ufisadi na Ukabila yaan jiandae Uganda kuwakimbiza na mkikaa vibaya hadi Burundi.
Kama mumemsikia leo JPM anakwambia anataka kutengeneza Meli kwenda Kaliuwa ili mizigo ya Congo iende moja kwa moja Congo bila kupitia nchi nyingine na akamaliza akasema upande huo wa Congo ambako anataka kujenga Meli kuna Migodi ya Madini ya Congo na walikuwa wanakosa usafirishaji wa Meli ili yawe yanasafirishwa kuja bandari ya Dar.