Basi la Kampuni ya New Force lapata ajali na kuua watu watano

Basi la Kampuni ya New Force lapata ajali na kuua watu watano

Golden deer na New force nadhani mmiliki wake ni shemeji ya mkubwa Fulani huko LATRA..
hizi Basi zinaenfeshwa rafu lkn hakuna RTO anayethubutu kuyakemea.
ma RTO Moro, Iringa, Mbeya, songe semeni ukweli, mmiliki hua anawaona Mara kwa Mara!
Kuna siku naenda Mbeya nimepanda V8 jamaa wametupita Nyororo sisi dereva ana 80 inawezekana wao walikuwa na zaidi ya 100 na hatukuwakuta tena. Newforce Mbele Sauli nyuma ni mwendo wa mbio tu na overtaking za hovyo. Yaani Malori na mabasi au magari yanayokuja mbele yao.ndio yanatakiwa yakae pembeni na yawapishe ili wao wapite. Ile halo ilituuzi tukaenda wakuta pale cheki point ya uhamiaji Makambako. Tutasimama na kuwashtaki kwa Polisi pale na kimsingi tulitaka tuwalambe fimbo wale madereva.

Binafsi, naona watu wanaopanda hizo gari za newforce au Sauli ni Wehu. Mtu mzima mwenye akili timamu hawezi risk maisha yake vile. Magari yanakimbizwa hovyo, hayana overtaking zuri. Ulikutana nayo yanashuka kitonga mpaka unashangaa. Hii nchi bwana, inatia uchungu watu wanapoteza maisha na wahusika wapo wanaangalia tu. Very painfull.
 
Siku nimekula NewForce tulipata kipengele Kitonga pale gari ilipasuka kioo cha site mirror tu hamna alieumia. Tukaendelea kibishi ila mwendo wa ni wa hatari sana.
Pole, nilishuhudia hilo tukio. Kwa mtu mwenye akili hawezi panda zile gari.
 
Naona video yake hapa hakika inasikitisha sana yaani.

Nimeona pia wananchi au wadau wa usafiri wanailalamikia @LatraTZ kuwa wanaziandama basi flani za ukanda wa ziwa na kusahau njia nyingine wakidhani ajali ni kwa njia ya Mwanza tu.
Yan jana tu nikasema. Hawa Latra waelekeze macho na njia ya Mbeya. Kumbe tayari kilikuwa kinaumana.
 
Haya magari ya new force yanakimbia jamani, nakumbuka last week nimepanda new force naenda Mbeya na ndo mara yangu ya kwanza kupanda new force.

Aloo gari inaovertake sijapata ona, maeneo yanayo-overtake ni ya hatari sana. Picha linaanza imeovertake gari na mbele kidogo tena kuna gari nyengine inakuja speed ila jamaa hawazi wala nini, kuna muda mpaka nikapiga kelele wenyeji wakawa wananishangaa wakaniambia mbona ni kawaida tu nikasema siangalii mbele.

Kuna muda tulikuwa kitonga nilikuwa naomba dua njia nzima tuvuke walau hapo, maana jamaa anaovertake pale tena yupo na mwendo mkali balaa njia yenyewe ni nyembamba, muda mwingne tupo kwenye kona kali ila jamaa anaovertake na wala haangalii mbele kuna nini, yeye anapiga honi tu anapita daah balaa sana haya magari.



Kampuni za hivi zifungiwe.

Na dereva wa hivyo afutiwe leseni.

Wengine wana magonjwa ya afya ya akili.

Wengine wavuta bangi.

Wengine hawana cha kupoteza.
 
Kwani hiyo haikimbii mwendokasi?

Ina mwendokasi vile vile.

Kwa route za Dodoma Dar mabasi yenye mwendo wa kawaida wa usalama ni Kimbinyiko, nasikia na ABC though sijawahi kuipanda uthibitisha kama ni kweli.
Lakini Kimbinyiko madereva wake wamejaa subira na wako royal.
Kila kampuni ina gari moja au mbili mwendo wa ngiri mkia juu mbio mbio hapo inaleta picha sio kampuni kuna baadhi ya madereva ndio vichaa wa mbio.....
 
Basi kampuni ya mwekezaji kutoka China, New Force/Golden Deer imepata ajali na kuua watu kadhaa.

Wakati ajali hiyo inatokea ndani ya mwezi huu itakuwa ajali ya 3 kwa kampuni hiyo baada ya last week kupata pia ajali maeneo ya Morogoro.

Chanzo ni mwendo wa mashindano.

======

Kamanda wa Polisi, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP John Makuri amethibitisha tukio la ajali mbaya iliyotokea katika Eneo la Igando Wilaya ya Waging'ombe ikihusisha basi la NewForce lililokuwa linatoka Dar kwenda Sumbawanga.

Kwa mujibu wa Kamanda Makuri, bado idadi kamili ya Vifo na Majeruhi haijajulikana na kwa sasa bado wapo eneo la tukio huku Majeruhi wakipelekwa Hospitali ya Kanisa ya Ilembula

======

Watu watano wamefariki huku wengine wakijeruhiwa, baada ya basi la kampuni ya New Force, lenye namba za usajili T 173 DZU, kuanguka wakati likijaribu kulipita lori, kisha kupoteza uelekeo na kugonga daraja katika eneo la Kijiji cha Igando kilichopo wilayani Wanging'ombe mkoani wa Njombe.
Kiufupi NewForce sio Mabasi ya kupanda hawajali kabisa na matokeo yake ndio haya kusababisha vifo vya watu wasio na hatia..

Lingekufa lidereva peke yake.
 
Rama Tunduma Dar hiyo, jamaa niliwahi mfuata akiwa speed sanaaa, nilipomwambia apunguze speed Kuna jamaa wakawa wanampa kichwa kuwa aendelee kuipa moto, nikamwambia "kaka kuna wakati hizo kelele za wanaokushangilia hautaziona, utawajibika peke yako"

Alijifanya kukaza na kuongea maneno meeengi lakini alipunguza fujo kwa kiasi kikubwa sana!

Wakati fulani abiria wanachangia sana hizi ajali, either kwa kukaa kimya au kwa kushangilia madereva wanapokwenda
Ulifanya jambo la msingi ni heri akushushe na nauli akupe maana akigoma nashuka tutamalizana Polisi ,kukaza ujinga kama huo harafu unakufa kizembe au kuwa kilema ni uendawasimu.
 
Ndio wanabeti kwa kupewa 100,000 kwa dereva anayewahi kufika pale Uyole au Msamvu au Magufuli. Hizi wapo madereva wa SAULI na Newforce. Kwa sisi tunaotumia barabara ya TANZAM, Hayo mabasi yalitakiwa yafungiwe muda na tumelalamika sana kuwa yachukuliwe hatua wenye mamlaka wananyamaza tu. Natamani leo dereva awe amekufa, kuwe na ndugu wa kiongozi yoyote wa nchi au awemo Polisi mmoja amayechukua rushwa ya 1000 kisha kufumbia macho huo upuuzi.

Kuna siku nilikuwa nasafiri na nipo kwenye V8 jamaa wakatupita wanakimbizana na hatukuweza wakutana hadi tumefika pale kwenye cheki point ya uhamiaji Makambako. Jamaa wanakimbiza hovyo, wana overtake hovyo n.k. Siku tulikutana na SAULI anashuka kitonga pale, aiseeeee.
Dawa Yao ni kueneza sumu Kwa watu wastaarabu ambao ni wengi wasipande ,binafsi siwezi panda hayo Mabasi labda Kwa dharula sana..
 
Jeshi la polisi fanyeni kazi yenu kwa weledi. Mabasi yanayovunja sheria za barabarani mnayafahamu vizuri. Ikiwezekana hizo kampuni zifutwe kabisa.
Wajinga tuu hao Polisi Bora hata Latea,Huwa vikipewa buku ten hakuna Cha maana wanafanya.
 
Back
Top Bottom