wakukurupuka1
JF-Expert Member
- Feb 17, 2023
- 525
- 1,186
Wakati ajali hiyo inatokea ndani ya mwezi huu itakuwa ajali ya 3 kwa kampuni hiyo baada ya last week kupata pia ajali maeneo ya Morogoro.
Chanzo ni mwendo wa mashindano.
======
Kamanda wa Polisi, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP John Makuri amethibitisha tukio la ajali mbaya iliyotokea katika Eneo la Igando Wilaya ya Waging'ombe ikihusisha basi la NewForce lililokuwa linatoka Dar kwenda Sumbawanga.
Kwa mujibu wa Kamanda Makuri, bado idadi kamili ya Vifo na Majeruhi haijajulikana na kwa sasa bado wapo eneo la tukio huku Majeruhi wakipelekwa Hospitali ya Kanisa ya Ilembula
======
Watu watano wamefariki huku wengine wakijeruhiwa, baada ya basi la kampuni ya New Force, lenye namba za usajili T 173 DZU, kuanguka wakati likijaribu kulipita lori, kisha kupoteza uelekeo na kugonga daraja katika eneo la Kijiji cha Igando kilichopo wilayani Wanging'ombe mkoani wa Njombe.