Basi la Kampuni ya New Force lapata ajali na kuua watu watano

Abood wana madereva wengine wajinga sana hasa kwenye ku-overtake...wasipojiangalia watakuja kusababisha ajali...
Miaka ya 90 mwishoni na mwanzoni 2000 yalikuwa yakifahamika kama chinja chinja. Watu walikuwa wanaogopa kupanda Abood bus. Kampuni iliyokuwa juu ilikuwa ni Hood na islam mwendo wa kobe ila sasa hivi wamefilisika na kumwacha abood akitamba.
 
Hata sisi abiria kuna mda tunawaendekeza hawa watu na tunabaki kuwalaumu usalama barabarani,gari iko mwendo kasi polisi anaingia anaongea vizuri anauliza hali ya mwendo,karibia abiria wote wanasema mwendo unaridhisha anawakumbusha kuhusu kupiga simu ikiwa kuna uvunjaji wa sheria za barabarani,abiria wao wanawaza kufika
Ikishatokea ajali lawama zinaanza,sasa wale watu mlitaka wafanyeje?

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Golden deer na New force nadhani mmiliki wake ni shemeji ya mkubwa Fulani huko LATRA..
hizi Basi zinaenfeshwa rafu lkn hakuna RTO anayethubutu kuyakemea.
ma RTO Moro, Iringa, Mbeya, songe semeni ukweli, mmiliki hua anawaona Mara kwa Mara!
Hizo chuma za mwekezaji huwa zina maelekezo. DZU zimeongoza kupata ajali katika hiyo kampuni.

Rama na Linyama (Ndugu abia) ndio kina Lewis hamilton wa hayo mabasi. Wanaendesha kama wapo kwenye mashindano ya Formula One.

Ukitaka usafiri wa taratibu panda ABC ila mbeya utaingia saa 3 au saa 4 usiku. Hao kina Golden Deer (New force) na Sauli ukiondoka magufuli saa 9 usiku utaingia mbeya kabla ya saa 10 alasiri na ukiondoka saa 12 alfajiri mbeya unaingia saa 12 kasoro tu.
 
Mbaya sana unaovertake na speed 80-120 halafu mbele unakutana na vicheche .Wiki iliyopita New force iligonga lorry lililokuwa limepaki. Ajali isikieni tu inatisha sana.

Kuna kipindi nilipanda Abood ilikuwa kidogo agonge angle ya kontena, ingeua vibaya sana aisee.

Mungu atunusuru ameen
 
Miaka ya 90 mwishoni na mwanzoni 2000 yalikuwa yakifahamika kama chinja chinja. Watu walikuwa wanaogopa kupanda Abood bus. Kampuni iliyokuwa juu ilikuwa ni Hood na islam mwendo wa kobe ila sasa hivi wamefilisika na kumwacha abood akitamba.
Kafara zilifanya kaz
 
Yan jana tu nikasema. Hawa Latra waelekeze macho na njia ya Mbeya. Kumbe tayari kilikuwa kinaumana.
Binafsi naangalia tatizo la hizi taasisi zetu za kiserikali zinavyoshindwa kusimamia majukumu yao kwa weledi badala yake wanafuatilia issues za ajabu kama ile ya Katarama na Ally's bus kule tweeter.

Wanajisahau kama kuna barabara zaidi ya Dar Mwanza.
 
Naushuhuda mmoja Miaka mi 3 iliyopita
Kuna rafiki yang ni dereva wa bus kampuni X bus za safari ndefu Sasa weekend nilikua naenda nae Bukoba tukifika ushirombo ananiachia niendeshe nilichokua nainjoy ni kukimbizana na bus zingine tulizotoka nazo Arusha nilikua sifikirii kabisa maisha ya watu bahati mbaya hata njia ilikua siijui vizuri.

Tukitoka Bukoka ye anaendesha Hadi singida na tukitoka singida kwenyee saa kumi na mbili jion ananipa mi naenda napeleka chuma had Arusha hapo mi siyo dereva wa hilo bus wala mmiliki hanijui ila ushkaji tu na michezo ya kipuuzi ndo tuliweka mbele Sasa ilikua ni mwendo wa kukimbizana tu, Na kila mkoa tuliokua tunaingia stand Kuna mashabiki wengi ukiwa wa kwanza shangwe ni kubwa balaa
siku moja nikawa nateremka mlima mmoja una kona Kali sana kabla hujaingia babati nikakuta ajali mbaya sana

baada ya kushuhudia ile ajali nilijiona sina tofauti na mtu anaejaribu kucheza na roho za watu niliamua kuacha kabisa ule mchezo niliokuanafanya jamaa akawa ananitafuta weekend nikawa natengengeneza sababu tu ilimradi nisiende.

kwahiyo huku barabarani kuna mambo mengi sana yanaendelea upande wa ma bus kuna ligi ambazo zina mashabiki zaidi ya ligi ya Uefa champions league, watu wanashabikia mwendo kasi wapo tayari wasilale had saa 6 usiku wasubiri bus stand waone Nani kawa wakwanza kufika washangilie

Aina hii ya maisha tuliyoamua kuishi tusipokua makini tutaendelea kushuhudia ajali mbaya sana.
Igunga niliingia na kisbo kutoka Dar Saa kumi na Moja na dkk 7 jioni hapo imetoka ubungo Saa kumi na mbili ...
Kufika igunga gari inamwagiwa juice ,soda na full shangwe km loteee... Wee acha hii nchi
 
Kwani hiyo haikimbii mwendokasi?

Ina mwendokasi vile vile.

Kwa route za Dodoma Dar mabasi yenye mwendo wa kawaida wa usalama ni Kimbinyiko, nasikia na ABC though sijawahi kuipanda uthibitisha kama ni kweli.
Lakini Kimbinyiko madereva wake wamejaa subira na wako royal.
ABC Zaidi ya Kobe wako very sloooow....
 
ABC Zaidi ya Kobe wako very sloooow....



Hao wananifaa mimi,
Ikitokea safari ya Dodoma nitakuja niipande naamini nitafurahia safari yenye utulivu na usalama.

Nimekuwa nikisikia kwa miaka kadhaa hao jamaa hawanaga mwendokasi,

Wanajali sana usalama wa abiria zao.
 
Hizo chuma za mwekezaji huwa zina maelekezo. DZU zimeongoza kupata ajali katika hiyo kampuni.

Rama na Linyama (Ndugu abia) ndio kina Lewis hamilton wa hayo mabasi. Wanaendesha kama wapo kwenye mashindano ya Formula One.

Ukitaka usafiri wa taratibu panda ABC ila mbeya utaingia saa 3 au saa 4 usiku. Hao kina Golden Deer (New force) na Sauli ukiondoka magufuli saa 9 usiku utaingia mbeya kabla ya saa 10 alasiri na ukiondoka saa 12 alfajiri mbeya unaingia saa 12 kasoro tu.
sauli hana safari za saa tisa usiku mkuu, ni kumi na moja ndo huwa anaanza safari zake.
 
Wazungu wana haki kutuita manyani.
Kwa akili hizi ndiyo tutaweza kuendesha bandari? Wacha waarabu wapewe waendeshe kila kitu.
 
Nimegubikwa na simanzi...
😭😭😭
Alafu nataka niwatukane wazembe wote waliosababisha ajali hii... Dereva yuko wapi kmmmkee.,..
Dahh...
Haiwezekanii...
IMG_20230622_223107.jpg

☝🏾Inasemekana na yeye amefariki.
 
Back
Top Bottom