Ajali ya basi la Isamilo na Libanika, alfajiri ya leo

Ajali ya basi la Isamilo na Libanika, alfajiri ya leo

dronedrake

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2013
Posts
24,809
Reaction score
61,673
Ajali mbaya za basi la Isamilo linalofanya safari zake Mwanza-Dar kugongana uso kwa uso na basi la Libanika (Dar-Mwanza) iliyotokea alfajiri ya leo, kijiji cha Msembeta, kata ya Nala, wilaya ya Dodoma, mkoa wa Dodoma.

Kumekuwa na ripoti za vifo kadhaa na majeruhi wengi

Chanzo cha ajali ikiwa ni mwendokasi wa basi la Isamilo (linatoka Mwanza kwenda Dar) , ku overtake lori kwenye mlima na likiwa kwenye kona kali, kulivamia basi la Libanika lililokuwa linatoka Dar kwenda Mwanza

Updates 1
=========================
Wamefariki watu 9 ikiwemo dereva, makondakta na abiria
Jumla ya majeruhi ni 66 na 9 kati yao wameripotiwa kuwa katika hali mbaya na wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma
==========================

Updates 2
=========================
Dereva nambari 2 wa basi la Isamilo akamatwa na anashikiliwa na jeshi la polisi Dodoma
Ikumbukwe huyu dereva ndiye "aliyesababisha" ajali kisha kukimbia akiwa na majeraha
=========================


cc2.jpg
bb1.jpg


aa2.jpg
 
RIP marehemu na pole nying kwa majeruhi.
Hii week kumetokea ajali nying za mabus ya abiria.

NB: mm Huwa nakaa siti ya katikati .
Upande wa Dereva.
abadan sikaagi siti za mbele.

Hao Abiria wa mbele sijuo kama wametoka salama.
 
Ajali mbaya za basi la Isamilo linalofanya safari zake Mwanza-Dar kugongana uso kwa uso na basi la Libanika (Dar-Mwanza) iliyotokea alfajiri ya leo, eneo la Msembeta, Dodoma

Kumekuwa na ripoti za vifo kadhaa na majeruhi wengi

Chanzo cha ajali ikiwa na mwendokasi wa basi la Isamilo (linatoka Mwanza kwenda Dar) , ku overtake kwenye mlima na likiwa kwenye kona kali, kulivamia basi la Libanika lililokuwa linatoka Dar kwenda Mwanza

View attachment 3641874View attachment 3641875View attachment 3641876
Mungu wangu🥱
 
Hawa wapumbavu wa mabasi wamezoea kuovateki wanapojisikia, wakitukuta sisi waendesha bebi woka tunawapisha njia,wakikutana wemyewe au na Lori haya ndio matokeo yake. Na wakifanya upumbavu wao kuna abiria wanachekelea tu kama mazuzu.
 
Back
Top Bottom