Balile: DPP, IGP, DCI lifutieni taifa aibu kesi ya Mbowe

Nafasi za ajira jeshi la polisi;
Sifa za kujiunga:
Awe na division 4 ya point 29, mpaka 34.

Asante
Hoja za div 4 au PhD nihoja za kipumbafu kabisa kuongoza nimoyo Wa huruma na kutambua wajibu wako kila muda wakati wote chamuhim kabisa kuzingatia haq wenye ma PhD ndio waliotuingiza katika mikataba mibovu na wizi wakutisha unafanywa nawao katika Mali zauma tuache kuamini madaftari na vyeti tuangalie kusoma nakuandika kikubwa kabisa katika hili uadilifu ndio msaada kwa nchi sio phd
 
Na Deodatus Balile

Imenichukua muda kuandika makala hii. Ninafahamu kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, anashitakiwa kwa tuhuma za kufadhili ugaidi kwa Sh 600,000. Anashitakiwa pia kwa tuhuma za kupanga njama za kulipua vituo vya mafuta katika miji ya Arusha, Mwanza na Dar es Salaam mwaka 2020.

Kubwa zaidi, anatajwa kuwa alitaka kumdhuru Lengai ole Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mwaka jana. Sabaya yuko mahakamani anashitakiwa kwa wizi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka.

Sitanii, ninafahamu kuna kundi halijakata tamaa. Kila nikiandika ukweli, husambaza taarifa kuwa mimi ni mwanaharakati. Ninadhani katika eneo hili kuna kutojitambua. Kuna tofauti kati ya harakati na uandishi wa habari.

Mwandishi wa habari anasimamia ukweli, ukweli mtupu. Hafanyi kampeni katika jambo analoliandika, bali yeye anaeleza ukweli wa kinachoendelea na kuuonyesha umma ni wapi kuna tundu lizibwe.

Ninafahamu kesi ikiwa mahakamani kifungu cha 114(1)(d) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kinazuia kuijadili, kwa kueleza nani anashinda na nani anashindwa.

Hilo ni jukumu la mahakama, nami sitaingia huko. Ni kwa msingi huo, hata washitakiwa wengine anaoshitakiwa nao Mbowe wala siwataji. Mimi ninalo jambo moja la kitaifa. Sura ya nchi yetu kimataifa.

Ninaomba kwa unyenyekevu mkubwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, Sylvester A. Mwakitalu, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro na Mkurugenzi wa Upelelezi, DCI Kamishna Camillius Wambura mnisikilize kidogo. Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, anaandaa filamu yenye lengo la kuitangaza Tanzania nje ya nchi.

Sitanii, uamuzi wa Rais Samia kuandaa filamu ni wa msingi na wa kuungwa mkono. Yapo mataifa ambayo kamwe hayaifahamu Tanzania. Sisi tuliopata fursa ya kusafiri nje ya nchi, unakuwa kama Washington, ukimwambia Mzungu unatoka Tanzania, anakuuliza: “Tasmania?” Tasmania ni kisiwa cha nchini Australia chenye ukubwa wa kilomita za mraba 90,758. Kina wakaazi 541,000 na kimezungukwa na visiswa vidogo 1,000. Kisiwa hiki ni cha 26 kwa ukubwa duniani. Kinavutia watalii wengi.

Ni nadra sana kukutana na mtu nje ya nchi, tena wakati mwingine wasomi waliobobea wakiifahamu Tanzania.

Uamuzi wa Rais Samia kuitangaza nchi yetu kupitia utalii ni wa kwanza kufanywa na Rais binafsi, bila kutegemea wasaidizi au wageni maarufu kutoka nje ya nchi ndio watangaze utalii wetu. Utalii unakadiriwa kuingiza dola bilioni mbili hapa nchini.

Nchi ya Misri yenye vivutio vichache ukilinganisha na sisi wanaingiza dola bilioni 12 kwa mwaka. Kwa uhalisia, bajeti ya Tanzania ni dola bilioni 14.

Tukiitangaza nchi yetu vizuri, tuna uwezekano wa kupata dola bilioni 15 kama mchezo kutoka kwenye utalii. Ni bahati mbaya, ninasema ni bahati mbaya juhudi hizi anazofanya Rais Samia zinavutwa miguu na uamuzi usio sahihi wa baadhi ya watendaji katika vyombo vya dola.

Sitanii, nimeomba kwa unyenyekevu mkubwa DPP, IGP na DCI mniazime masikio. Kuna makosa tunayafanya, sina uhakika kama ni kwa bahati mbaya au makusudi.

Hili neno ugaidi ni neno baya na la hatari sana katika masikio ya watalii, jumuiya ya wafanyabiashara na wasafiri wa kawaida. Yaliyotokea Septemba 11, 2001 nchini Marekani, bila kusahau ya Agosti 7, 1998 kwa Tanzania na Kenya ni somo kuu la ubaya wa neno gaidi.

Tanzania inapaswa kuwa ya mwisho kumfungulia mtu kesi ya ugaidi au kumtaja mtu kuwa ni gaidi. DCI ameiambia dunia Hamza Mohamed aliyeua askari watatu na mlinzi wa kampuni binafsi alikuwa gaidi. Inawezekana alikuwa mgonjwa wa akili tu. Neno kama hili halipaswi kutamkwa kamwe kutoka vinywani mwa vyombo vya dola. Mbowe anashitakiwa kwa kufadhili ugaidi, tena kwa Sh 600,000!!! Ugaidi kwa Sh 600,000? Let us be serious.

Sitanii, wanaotafuta nafasi ya kulichafua taifa letu mbele ya jamii ya kimataifa wanakusanya hizi kauli na kueleza kuwa Tanzania kuna ugaidi. Nilisema nitaizungumzia kesi ya Mbowe kwa picha pana. Kila Mbowe anapopelekwa mahakamani, vyombo vya habari vya kimataifa vinaimulika Tanzania na kuhakikisha neno ‘ugaidi’ linatajwa.

Sisi tunaweza kuwa na malalamiko yetu dhidi ya Mbowe. Tena wengine nikizungumza nao wanasema Mbowe alitaka kumshinikiza Rais Samia kwa matamko juu ya Katiba mpya, na milele Rais hashinikizwi. Tunaweza kujikuta katika ‘kujimwambafai’ tunalichafua taifa letu kwa kiwango cha kutisha. Ninashawishika kusema hapa tulipofika tufunge breki.

Tufunge breki tuchague mkondo wa mazungumzo badala ya mabavu. Rwanda na Burundi walipigana kwa mtutu, ila mwisho wa siku walikuja AICC Arusha wakafanya mazungumzo na wakaafikiana.

Ninaomba kusema si kila tatizo la kisiasa tutalitatua kwa kukamata watu na kuwafikisha mahakamani. Kwa kufanya hivyo, tutajikuta tunamchafua Rais aliyeko madarakani na nchi kwa ujumla.

Sitanii, kwa hatua iliyofikiwa DPP nikuombe utumie busara ya Mfalme Suleiman katika kubaini mtoto ni wa nani.

Mama mmoja alisema mtoto auawe, akatwe vipande viwili kila anayedai ni wake apewe kipande akazike. Aliyekuwa mama wa kweli akasema ni bora mama wa kusingizia amchukue huyo mtoto angalau atakuwa anamwona, anampungia mkono akiwa hai. Mfalme Suleiman kwa kauli hizo mbili akabaini mama halisi wa mtoto.

DPP wakati umefika utumie Kifungu cha 91 cha Sheria ya Mwenendo wa Mashitaka (CPA) kuondoa kesi ya Mbowe mahakamani. IGP na DCI niwaombe sana neno ugaidi msilitumie tena, linachafua sura ya Tanzania. Mbowe ni Mtanzania. Zungumzeni naye, mwelezeni umuhimu wa uzalendo kwa taifa letu.

Lakini pia msikilize na kesi zake za kuvunjiwa ukumbi wa Bilcanas. Msumeno ukate pande zote. Ninarudia, si kila kesi ya kisiasa tutaimaliza kwa kuifikisha mahakamani. Tuvuke huu msitari unaoleta sura ya ubabe. Mungu ibariki Tanzania.
Miongoni mwa wachache wenye uwezo wa kutumia kalamu vxr je wanaufahamu?

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Kama Mbowe ni gaidi, Gaidi ni gaidi tu, tutumie jina gani lingine? Nyoko nn, Balile aache uchadema wake kuandika kuhusu Mbowe. Balile ni Chadema inajulikana. Acha Mbowe afunzwe adabu.
 
Kuna watu wanajua kufikiri sawa sawa.Nadhani wakati umefikia katiba mpya wakatazama namna ya kuunda chombo kitakacho tazama utendaji wa Police.
... kabisa; kuna watu wako vizuri upstairs. Chombo huru cha ku-oversee utendaji wa polisi ni muhimu mno kwa sasa kuliko wakati mwingine wowote na mamlaka ya ukamataji mapolisi watakoonekana kukiuka sheria na taratibu wanaweza kukabidhiwa JWTZ, kitengo maalumu cha kudili na mapolisi. Kuwaacha polisi hao hao wajikamate wenyewe ni kulindana kama ilivyo sasa.
 
Na Deodatus Balile

Imenichukua muda kuandika makala hii. Ninafahamu kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, anashitakiwa kwa tuhuma za kufadhili ugaidi kwa Sh 600,000. Anashitakiwa pia kwa tuhuma za kupanga njama za kulipua vituo vya mafuta katika miji ya Arusha, Mwanza na Dar es Salaam mwaka 2020.

Kubwa zaidi, anatajwa kuwa alitaka kumdhuru Lengai ole Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mwaka jana. Sabaya yuko mahakamani anashitakiwa kwa wizi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka.

Sitanii, ninafahamu kuna kundi halijakata tamaa. Kila nikiandika ukweli, husambaza taarifa kuwa mimi ni mwanaharakati. Ninadhani katika eneo hili kuna kutojitambua. Kuna tofauti kati ya harakati na uandishi wa habari.

Mwandishi wa habari anasimamia ukweli, ukweli mtupu. Hafanyi kampeni katika jambo analoliandika, bali yeye anaeleza ukweli wa kinachoendelea na kuuonyesha umma ni wapi kuna tundu lizibwe.

Ninafahamu kesi ikiwa mahakamani kifungu cha 114(1)(d) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kinazuia kuijadili, kwa kueleza nani anashinda na nani anashindwa.

Hilo ni jukumu la mahakama, nami sitaingia huko. Ni kwa msingi huo, hata washitakiwa wengine anaoshitakiwa nao Mbowe wala siwataji. Mimi ninalo jambo moja la kitaifa. Sura ya nchi yetu kimataifa.

Ninaomba kwa unyenyekevu mkubwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, Sylvester A. Mwakitalu, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro na Mkurugenzi wa Upelelezi, DCI Kamishna Camillius Wambura mnisikilize kidogo. Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, anaandaa filamu yenye lengo la kuitangaza Tanzania nje ya nchi.

Sitanii, uamuzi wa Rais Samia kuandaa filamu ni wa msingi na wa kuungwa mkono. Yapo mataifa ambayo kamwe hayaifahamu Tanzania. Sisi tuliopata fursa ya kusafiri nje ya nchi, unakuwa kama Washington, ukimwambia Mzungu unatoka Tanzania, anakuuliza: “Tasmania?” Tasmania ni kisiwa cha nchini Australia chenye ukubwa wa kilomita za mraba 90,758. Kina wakaazi 541,000 na kimezungukwa na visiswa vidogo 1,000. Kisiwa hiki ni cha 26 kwa ukubwa duniani. Kinavutia watalii wengi.

Ni nadra sana kukutana na mtu nje ya nchi, tena wakati mwingine wasomi waliobobea wakiifahamu Tanzania.

Uamuzi wa Rais Samia kuitangaza nchi yetu kupitia utalii ni wa kwanza kufanywa na Rais binafsi, bila kutegemea wasaidizi au wageni maarufu kutoka nje ya nchi ndio watangaze utalii wetu. Utalii unakadiriwa kuingiza dola bilioni mbili hapa nchini.

Nchi ya Misri yenye vivutio vichache ukilinganisha na sisi wanaingiza dola bilioni 12 kwa mwaka. Kwa uhalisia, bajeti ya Tanzania ni dola bilioni 14.

Tukiitangaza nchi yetu vizuri, tuna uwezekano wa kupata dola bilioni 15 kama mchezo kutoka kwenye utalii. Ni bahati mbaya, ninasema ni bahati mbaya juhudi hizi anazofanya Rais Samia zinavutwa miguu na uamuzi usio sahihi wa baadhi ya watendaji katika vyombo vya dola.

Sitanii, nimeomba kwa unyenyekevu mkubwa DPP, IGP na DCI mniazime masikio. Kuna makosa tunayafanya, sina uhakika kama ni kwa bahati mbaya au makusudi.

Hili neno ugaidi ni neno baya na la hatari sana katika masikio ya watalii, jumuiya ya wafanyabiashara na wasafiri wa kawaida. Yaliyotokea Septemba 11, 2001 nchini Marekani, bila kusahau ya Agosti 7, 1998 kwa Tanzania na Kenya ni somo kuu la ubaya wa neno gaidi.

Tanzania inapaswa kuwa ya mwisho kumfungulia mtu kesi ya ugaidi au kumtaja mtu kuwa ni gaidi. DCI ameiambia dunia Hamza Mohamed aliyeua askari watatu na mlinzi wa kampuni binafsi alikuwa gaidi. Inawezekana alikuwa mgonjwa wa akili tu. Neno kama hili halipaswi kutamkwa kamwe kutoka vinywani mwa vyombo vya dola. Mbowe anashitakiwa kwa kufadhili ugaidi, tena kwa Sh 600,000!!! Ugaidi kwa Sh 600,000? Let us be serious.

Sitanii, wanaotafuta nafasi ya kulichafua taifa letu mbele ya jamii ya kimataifa wanakusanya hizi kauli na kueleza kuwa Tanzania kuna ugaidi. Nilisema nitaizungumzia kesi ya Mbowe kwa picha pana. Kila Mbowe anapopelekwa mahakamani, vyombo vya habari vya kimataifa vinaimulika Tanzania na kuhakikisha neno ‘ugaidi’ linatajwa.

Sisi tunaweza kuwa na malalamiko yetu dhidi ya Mbowe. Tena wengine nikizungumza nao wanasema Mbowe alitaka kumshinikiza Rais Samia kwa matamko juu ya Katiba mpya, na milele Rais hashinikizwi. Tunaweza kujikuta katika ‘kujimwambafai’ tunalichafua taifa letu kwa kiwango cha kutisha. Ninashawishika kusema hapa tulipofika tufunge breki.

Tufunge breki tuchague mkondo wa mazungumzo badala ya mabavu. Rwanda na Burundi walipigana kwa mtutu, ila mwisho wa siku walikuja AICC Arusha wakafanya mazungumzo na wakaafikiana.

Ninaomba kusema si kila tatizo la kisiasa tutalitatua kwa kukamata watu na kuwafikisha mahakamani. Kwa kufanya hivyo, tutajikuta tunamchafua Rais aliyeko madarakani na nchi kwa ujumla.

Sitanii, kwa hatua iliyofikiwa DPP nikuombe utumie busara ya Mfalme Suleiman katika kubaini mtoto ni wa nani.

Mama mmoja alisema mtoto auawe, akatwe vipande viwili kila anayedai ni wake apewe kipande akazike. Aliyekuwa mama wa kweli akasema ni bora mama wa kusingizia amchukue huyo mtoto angalau atakuwa anamwona, anampungia mkono akiwa hai. Mfalme Suleiman kwa kauli hizo mbili akabaini mama halisi wa mtoto.

DPP wakati umefika utumie Kifungu cha 91 cha Sheria ya Mwenendo wa Mashitaka (CPA) kuondoa kesi ya Mbowe mahakamani. IGP na DCI niwaombe sana neno ugaidi msilitumie tena, linachafua sura ya Tanzania. Mbowe ni Mtanzania. Zungumzeni naye, mwelezeni umuhimu wa uzalendo kwa taifa letu.

Lakini pia msikilize na kesi zake za kuvunjiwa ukumbi wa Bilcanas. Msumeno ukate pande zote. Ninarudia, si kila kesi ya kisiasa tutaimaliza kwa kuifikisha mahakamani. Tuvuke huu msitari unaoleta sura ya ubabe. Mungu ibariki Tanzania.
Umeongea ukweli, lakini kwa kuwa Rais Samia bado anashinikizwa na kundi moja ndani ya serikali yake au chama, hatafanya ila anaishi kwa kisasi. Ninyi Jamiiforums, tafadhali mkubali ukweli acheni kujipendekeza kufungia fungia watu wanaosema ukweli.
 
Hoja za div 4 au PhD nihoja za kipumbafu kabisa kuongoza nimoyo Wa huruma na kutambua wajibu wako kila muda wakati wote chamuhim kabisa kuzingatia haq wenye ma PhD ndio waliotuingiza katika mikataba mibovu na wizi wakutisha unafanywa nawao katika Mali zauma tuache kuamini madaftari na vyeti tuangalie kusoma nakuandika kikubwa kabisa katika hili uadilifu ndio msaada kwa nchi sio phd
Sasa tuambie kwanini wanakimbilia madaraja ya mwisho ya ufaulu wakati ya kwanza yapo?tena wanaweka na sharti kabisa kwamba aanzie division 4 ilhali kuna vijana waliofaulu vizuri wapo mtaani lakini vigezo vya polisi haviwaruhusu?
 
Kuna member mmoja kwenye ile thread ya kesi ya Mbowe kaandika point ya maana sana; kwamba Jeshi la Polisi ni chombo kinachohusika na haki za wananchi moja kwa moja; is there any oversight body to oversee Police Force? Hakipo!

Yaani wao Polisi wamekabidhiwa mamlaka yote kuhusu haki za wananchi na hakuna chombo huru kinacho-monitor matendo yao? Wanaweza kujifanyia wapendavyo na kuripoti UONGO? Hii haikubaliki; kama taasisi kama TRA, PPRA, LATRA, n.k. ambazo zina oversight bodies kuhakikisha haki inatendeka sembuse polisi wanaohusika na MAISHA ya wananchi? Tena polisi wenyewe ndio hawa wanaoweza kutumika na wanasiasa! Hii ni hatari sana! Katiba Mpya isisahau hili.
Mzee mmoja amedai SSH haijui hii nchi! Nadhani madai hayo yanaweza kuwa na ukweli kiasi. SSH angekuwa anaifahamu vizuri hii nchi angejua kuwa jeshi la polisi siyo chombo cha kukiamini sana. Angekuwa anaifahamu nchi ikiwa ni pamoja na undani wa jeshi la polisi asingemeza jumla jumla taarifa kuwa ushahidi wa kutosha upo kuwa Mbowe ni gaidi! Matokeo ya SSH kutolifamu jeshi lake la polisi pamoja na vyombo vingine kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe sasa imeanza kugeukwa mwiba kwa nchi yetu. Kesi imeanza kuibua mambo mazito kuhusu jeshi la polisi ambayo lazima yaje kufanyiwa kazi bila kujali Mbowe amepatikana na hatia au la. Lakini pia inaelekea huu ni mpango wa Mungu kuwa pamoja na madhara yanayotokana na kesi hii yatokee mambo ya kunufaisha jamii yetu. Sote sasa tunajua kuwa udhaifu uliopo katika jeshi la polisi hauvumiliki!
 
Mzee mmoja amedai SSH haijui hii nchi! Nadhani madai hayo yanaweza kuwa na ukweli kiasi. SSH angekuwa anaifahamu vizuri hii nchi angejua kuwa jeshi la polisi siyo chombo cha kukiamini sana. Angekuwa anaifahamu nchi ikiwa ni pamoja na undani wa jeshi la polisi asingemeza jumla jumla taarifa kuwa ushahidi wa kutosha upo kuwa Mbowe ni gaidi! Matokeo ya SSH kutolifamu jeshi lake la polisi pamoja na vyombo vingine kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe sasa imeanza kugeukwa mwiba kwa nchi yetu. Kesi imeanza kuibua mambo mazito kuhusu jeshi la polisi ambayo lazima yaje kufanyiwa kazi bila kujali Mbowe amepatikana na hatia au la. Lakini pia inaelekea huu ni mpango wa Mungu kuwa pamoja na madhara yanayotokana na kesi hii yatokee mambo ya kunufaisha jamii yetu. Sote sasa tunajua kuwa udhaifu uliopo katika jeshi la polisi hauvumiliki!
... najaribu kuwaza tu; hivi ikija kugundulika hii kesi ni just fabrication na ushahidi ni wa kutunga then what next? Kuna hatua zozote zinazoweza kuchukuliwa, sio kwa washtakiwa kufungua kesi ya madai, bali mamlaka dhidi ya genge lote la polisi waliohusika kuanzia IGP? Kimsingi hii ni kashfa kubwa sana chombo ambacho kazi yake ya msingi ni kutenda HAKI kinafanya kinyume kabisa!

Kungekuwa na oversight body ya jeshi la polisi hii ndio ilikuwa miongoni mwa majukumu yake ya msingi baada ya kesi kumalizika; kuchunguza kama kulikuwa na ukiukwaji wa haki za washtakiwa wote waliohusika na ukiukwaji huo wawajibishwe. Nchi haiwezi kuendeshwa kihuni na genge fulani lililokabidhiwa madaraka kwa mujibu wa katiba na sheri za nchi wakaamua kizinajisi!
 
IGP anaju
Umeongea vyema kabisa. Ila kuna shida kubwa sana ndani ya kichwa cha Siro. Hata ukiangalia alivyo ongea kwamba polisi hawana sheria inayo wazuia kuingilia mikutano ya vyama vya siasa, utaona uso wake una aibu. Lakini amesha amua ana fanya. Kwa sheria gani? Jilo analijua yeye. Ila kwa kweli polisi imelipaka taifa matope.
IGP anajua mipaka yake kisheria. Anapoingilia vyama vya siasa siyo kwamba hajui balj anatekeleza maelekezo ya watawala. Awali ilidhaniwa vyama husika vitaogopa na kurudi nyuma. Hilo halijatokea; badala yake CHADEMA wamekomaa licha ya kukamatwa na kulala mahabusu. Jeshi la polisi wamejikuta wakimbizana nao kila kukicha. Wakati huo huo polisi hao wanatuhumiwa kuvunja katiba. Hali hii siyo endelevu; lazima ifikie mwisho. Hivyo kinachotafutwa sasa ni huo mwisho; uonekane kana kwamba mazungumzo yamefanyika na maelewano yamepatikana! Ndipo msajili anaingia!
 
Na Deodatus Balile

Imenichukua muda kuandika makala hii. Ninafahamu kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, anashitakiwa kwa tuhuma za kufadhili ugaidi kwa Sh 600,000. Anashitakiwa pia kwa tuhuma za kupanga njama za kulipua vituo vya mafuta katika miji ya Arusha, Mwanza na Dar es Salaam mwaka 2020.

Kubwa zaidi, anatajwa kuwa alitaka kumdhuru Lengai ole Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mwaka jana. Sabaya yuko mahakamani anashitakiwa kwa wizi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka.

Sitanii, ninafahamu kuna kundi halijakata tamaa. Kila nikiandika ukweli, husambaza taarifa kuwa mimi ni mwanaharakati. Ninadhani katika eneo hili kuna kutojitambua. Kuna tofauti kati ya harakati na uandishi wa habari.

Mwandishi wa habari anasimamia ukweli, ukweli mtupu. Hafanyi kampeni katika jambo analoliandika, bali yeye anaeleza ukweli wa kinachoendelea na kuuonyesha umma ni wapi kuna tundu lizibwe.

Ninafahamu kesi ikiwa mahakamani kifungu cha 114(1)(d) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kinazuia kuijadili, kwa kueleza nani anashinda na nani anashindwa.

Hilo ni jukumu la mahakama, nami sitaingia huko. Ni kwa msingi huo, hata washitakiwa wengine anaoshitakiwa nao Mbowe wala siwataji. Mimi ninalo jambo moja la kitaifa. Sura ya nchi yetu kimataifa.

Ninaomba kwa unyenyekevu mkubwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, Sylvester A. Mwakitalu, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro na Mkurugenzi wa Upelelezi, DCI Kamishna Camillius Wambura mnisikilize kidogo. Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, anaandaa filamu yenye lengo la kuitangaza Tanzania nje ya nchi.

Sitanii, uamuzi wa Rais Samia kuandaa filamu ni wa msingi na wa kuungwa mkono. Yapo mataifa ambayo kamwe hayaifahamu Tanzania. Sisi tuliopata fursa ya kusafiri nje ya nchi, unakuwa kama Washington, ukimwambia Mzungu unatoka Tanzania, anakuuliza: “Tasmania?” Tasmania ni kisiwa cha nchini Australia chenye ukubwa wa kilomita za mraba 90,758. Kina wakaazi 541,000 na kimezungukwa na visiswa vidogo 1,000. Kisiwa hiki ni cha 26 kwa ukubwa duniani. Kinavutia watalii wengi.

Ni nadra sana kukutana na mtu nje ya nchi, tena wakati mwingine wasomi waliobobea wakiifahamu Tanzania.

Uamuzi wa Rais Samia kuitangaza nchi yetu kupitia utalii ni wa kwanza kufanywa na Rais binafsi, bila kutegemea wasaidizi au wageni maarufu kutoka nje ya nchi ndio watangaze utalii wetu. Utalii unakadiriwa kuingiza dola bilioni mbili hapa nchini.

Nchi ya Misri yenye vivutio vichache ukilinganisha na sisi wanaingiza dola bilioni 12 kwa mwaka. Kwa uhalisia, bajeti ya Tanzania ni dola bilioni 14.

Tukiitangaza nchi yetu vizuri, tuna uwezekano wa kupata dola bilioni 15 kama mchezo kutoka kwenye utalii. Ni bahati mbaya, ninasema ni bahati mbaya juhudi hizi anazofanya Rais Samia zinavutwa miguu na uamuzi usio sahihi wa baadhi ya watendaji katika vyombo vya dola.

Sitanii, nimeomba kwa unyenyekevu mkubwa DPP, IGP na DCI mniazime masikio. Kuna makosa tunayafanya, sina uhakika kama ni kwa bahati mbaya au makusudi.

Hili neno ugaidi ni neno baya na la hatari sana katika masikio ya watalii, jumuiya ya wafanyabiashara na wasafiri wa kawaida. Yaliyotokea Septemba 11, 2001 nchini Marekani, bila kusahau ya Agosti 7, 1998 kwa Tanzania na Kenya ni somo kuu la ubaya wa neno gaidi.

Tanzania inapaswa kuwa ya mwisho kumfungulia mtu kesi ya ugaidi au kumtaja mtu kuwa ni gaidi. DCI ameiambia dunia Hamza Mohamed aliyeua askari watatu na mlinzi wa kampuni binafsi alikuwa gaidi. Inawezekana alikuwa mgonjwa wa akili tu. Neno kama hili halipaswi kutamkwa kamwe kutoka vinywani mwa vyombo vya dola. Mbowe anashitakiwa kwa kufadhili ugaidi, tena kwa Sh 600,000!!! Ugaidi kwa Sh 600,000? Let us be serious.

Sitanii, wanaotafuta nafasi ya kulichafua taifa letu mbele ya jamii ya kimataifa wanakusanya hizi kauli na kueleza kuwa Tanzania kuna ugaidi. Nilisema nitaizungumzia kesi ya Mbowe kwa picha pana. Kila Mbowe anapopelekwa mahakamani, vyombo vya habari vya kimataifa vinaimulika Tanzania na kuhakikisha neno ‘ugaidi’ linatajwa.

Sisi tunaweza kuwa na malalamiko yetu dhidi ya Mbowe. Tena wengine nikizungumza nao wanasema Mbowe alitaka kumshinikiza Rais Samia kwa matamko juu ya Katiba mpya, na milele Rais hashinikizwi. Tunaweza kujikuta katika ‘kujimwambafai’ tunalichafua taifa letu kwa kiwango cha kutisha. Ninashawishika kusema hapa tulipofika tufunge breki.

Tufunge breki tuchague mkondo wa mazungumzo badala ya mabavu. Rwanda na Burundi walipigana kwa mtutu, ila mwisho wa siku walikuja AICC Arusha wakafanya mazungumzo na wakaafikiana.

Ninaomba kusema si kila tatizo la kisiasa tutalitatua kwa kukamata watu na kuwafikisha mahakamani. Kwa kufanya hivyo, tutajikuta tunamchafua Rais aliyeko madarakani na nchi kwa ujumla.

Sitanii, kwa hatua iliyofikiwa DPP nikuombe utumie busara ya Mfalme Suleiman katika kubaini mtoto ni wa nani.

Mama mmoja alisema mtoto auawe, akatwe vipande viwili kila anayedai ni wake apewe kipande akazike. Aliyekuwa mama wa kweli akasema ni bora mama wa kusingizia amchukue huyo mtoto angalau atakuwa anamwona, anampungia mkono akiwa hai. Mfalme Suleiman kwa kauli hizo mbili akabaini mama halisi wa mtoto.

DPP wakati umefika utumie Kifungu cha 91 cha Sheria ya Mwenendo wa Mashitaka (CPA) kuondoa kesi ya Mbowe mahakamani. IGP na DCI niwaombe sana neno ugaidi msilitumie tena, linachafua sura ya Tanzania. Mbowe ni Mtanzania. Zungumzeni naye, mwelezeni umuhimu wa uzalendo kwa taifa letu.

Lakini pia msikilize na kesi zake za kuvunjiwa ukumbi wa Bilcanas. Msumeno ukate pande zote. Ninarudia, si kila kesi ya kisiasa tutaimaliza kwa kuifikisha mahakamani. Tuvuke huu msitari unaoleta sura ya ubabe. Mungu ibariki Tanzania.
Bwana Balile, asante kwa Mchango wako ambao umeutoa kwa kutoa mwanga wa muono wako kwa kesi hii ya ugaidi. Kwa muono wangu nakuona Umekua fundi wa uchambuzi populist ambao siku zote huficha ukweli na hautoi matokeo ya uchambuzi chanuo ambao ungetupatia utajiri wa muono na uhalisia wa tukio.

Umeshindwa kuanza uchambuzi wako kwa kutueleza Mbowe ni nani, ni nani kisiasa leo, ana nguvu gani au ushawishi wake katika siasa za leo. Tengeneza ushawishi katika uchambuzi wa kisiasa.

Jee umeona kuna fikra mpya zozote katika siasa za Mbowe na za upinzani? au bado ni muendelezo wa siasa za kupayuka tuu bila strategy for?.

Jee unaona kuna ufahari wowote kwa Mbowe kuwa mgeni wa bwana Jela? kuna matokeo ya kustua huko chini kwa wananchi kwa tukio hilo?

Ungeweza kutufahamisha kiwango cha arthari ambazo zilitegemewa.

Charity begins at home.
Injili ambayo anayo ailete huku Kilimanjaro kwani nasi tunaitaka sana. Na sisi kwa umoja wetu tuipeleke maeneo mbali mbali ya nchi yetu.
Kwa msio jua, mvuto wa Mbowe na Upinzani umepoteza sana ushawishi wake huku kwao Mbowe.

Balile kuna uwezekano mkubwa mna wakweza juu viongozi wetu sehemu ambayo hawapaswi kuwapo tena kwa siasa za leo.
 
hapa umelikoroga, does it mean that Mbowe is not patriotic? Not at all!
Unaweza ukawa mzalendo namba Moja.....ila malipo ya uzalendo wako yakawa ni mapigo (maumivu)

Binadamu tumeumbiwa Revenge (kisasi)
Binadamu wachache Sana mfano wa Nelson Mandela ndio pekee walituonesha kwa mifano na vitendo kua hatupaswi kuwafanyia Revenge watesi wetu......

Binadamu tunapishana level of understanding.... ndio maana naungana na jamaa alie sema wakae mezani na mbowe wamalize Hili jambo......

Viva Tanzania.....Viva wazalendo
 
Kwani gaidi anakuwa amevaa shanga usoni ilikujuwa kuwa ni gaidi? nyie vipi!!
uliwahi kusikia ugaidi unadhaminiwa kwa sh 600,000 dola 260? Ikiwa sabaya ni mwema alitaka agaidiwe na mbowe kwa nini mnataka kumfunga.

learn to think in three dimensions
 
Na Deodatus Balile

Imenichukua muda kuandika makala hii. Ninafahamu kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, anashitakiwa kwa tuhuma za kufadhili ugaidi kwa Sh 600,000. Anashitakiwa pia kwa tuhuma za kupanga njama za kulipua vituo vya mafuta katika miji ya Arusha, Mwanza na Dar es Salaam mwaka 2020.

Kubwa zaidi, anatajwa kuwa alitaka kumdhuru Lengai ole Sabaya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mwaka jana. Sabaya yuko mahakamani anashitakiwa kwa wizi wa kutumia silaha na matumizi mabaya ya madaraka.

Sitanii, ninafahamu kuna kundi halijakata tamaa. Kila nikiandika ukweli, husambaza taarifa kuwa mimi ni mwanaharakati. Ninadhani katika eneo hili kuna kutojitambua. Kuna tofauti kati ya harakati na uandishi wa habari.

Mwandishi wa habari anasimamia ukweli, ukweli mtupu. Hafanyi kampeni katika jambo analoliandika, bali yeye anaeleza ukweli wa kinachoendelea na kuuonyesha umma ni wapi kuna tundu lizibwe.

Ninafahamu kesi ikiwa mahakamani kifungu cha 114(1)(d) cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kinazuia kuijadili, kwa kueleza nani anashinda na nani anashindwa.

Hilo ni jukumu la mahakama, nami sitaingia huko. Ni kwa msingi huo, hata washitakiwa wengine anaoshitakiwa nao Mbowe wala siwataji. Mimi ninalo jambo moja la kitaifa. Sura ya nchi yetu kimataifa.

Ninaomba kwa unyenyekevu mkubwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini, Sylvester A. Mwakitalu, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro na Mkurugenzi wa Upelelezi, DCI Kamishna Camillius Wambura mnisikilize kidogo. Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, anaandaa filamu yenye lengo la kuitangaza Tanzania nje ya nchi.

Sitanii, uamuzi wa Rais Samia kuandaa filamu ni wa msingi na wa kuungwa mkono. Yapo mataifa ambayo kamwe hayaifahamu Tanzania. Sisi tuliopata fursa ya kusafiri nje ya nchi, unakuwa kama Washington, ukimwambia Mzungu unatoka Tanzania, anakuuliza: “Tasmania?” Tasmania ni kisiwa cha nchini Australia chenye ukubwa wa kilomita za mraba 90,758. Kina wakaazi 541,000 na kimezungukwa na visiswa vidogo 1,000. Kisiwa hiki ni cha 26 kwa ukubwa duniani. Kinavutia watalii wengi.

Ni nadra sana kukutana na mtu nje ya nchi, tena wakati mwingine wasomi waliobobea wakiifahamu Tanzania.

Uamuzi wa Rais Samia kuitangaza nchi yetu kupitia utalii ni wa kwanza kufanywa na Rais binafsi, bila kutegemea wasaidizi au wageni maarufu kutoka nje ya nchi ndio watangaze utalii wetu. Utalii unakadiriwa kuingiza dola bilioni mbili hapa nchini.

Nchi ya Misri yenye vivutio vichache ukilinganisha na sisi wanaingiza dola bilioni 12 kwa mwaka. Kwa uhalisia, bajeti ya Tanzania ni dola bilioni 14.

Tukiitangaza nchi yetu vizuri, tuna uwezekano wa kupata dola bilioni 15 kama mchezo kutoka kwenye utalii. Ni bahati mbaya, ninasema ni bahati mbaya juhudi hizi anazofanya Rais Samia zinavutwa miguu na uamuzi usio sahihi wa baadhi ya watendaji katika vyombo vya dola.

Sitanii, nimeomba kwa unyenyekevu mkubwa DPP, IGP na DCI mniazime masikio. Kuna makosa tunayafanya, sina uhakika kama ni kwa bahati mbaya au makusudi.

Hili neno ugaidi ni neno baya na la hatari sana katika masikio ya watalii, jumuiya ya wafanyabiashara na wasafiri wa kawaida. Yaliyotokea Septemba 11, 2001 nchini Marekani, bila kusahau ya Agosti 7, 1998 kwa Tanzania na Kenya ni somo kuu la ubaya wa neno gaidi.

Tanzania inapaswa kuwa ya mwisho kumfungulia mtu kesi ya ugaidi au kumtaja mtu kuwa ni gaidi. DCI ameiambia dunia Hamza Mohamed aliyeua askari watatu na mlinzi wa kampuni binafsi alikuwa gaidi. Inawezekana alikuwa mgonjwa wa akili tu. Neno kama hili halipaswi kutamkwa kamwe kutoka vinywani mwa vyombo vya dola. Mbowe anashitakiwa kwa kufadhili ugaidi, tena kwa Sh 600,000!!! Ugaidi kwa Sh 600,000? Let us be serious.

Sitanii, wanaotafuta nafasi ya kulichafua taifa letu mbele ya jamii ya kimataifa wanakusanya hizi kauli na kueleza kuwa Tanzania kuna ugaidi. Nilisema nitaizungumzia kesi ya Mbowe kwa picha pana. Kila Mbowe anapopelekwa mahakamani, vyombo vya habari vya kimataifa vinaimulika Tanzania na kuhakikisha neno ‘ugaidi’ linatajwa.

Sisi tunaweza kuwa na malalamiko yetu dhidi ya Mbowe. Tena wengine nikizungumza nao wanasema Mbowe alitaka kumshinikiza Rais Samia kwa matamko juu ya Katiba mpya, na milele Rais hashinikizwi. Tunaweza kujikuta katika ‘kujimwambafai’ tunalichafua taifa letu kwa kiwango cha kutisha. Ninashawishika kusema hapa tulipofika tufunge breki.

Tufunge breki tuchague mkondo wa mazungumzo badala ya mabavu. Rwanda na Burundi walipigana kwa mtutu, ila mwisho wa siku walikuja AICC Arusha wakafanya mazungumzo na wakaafikiana.

Ninaomba kusema si kila tatizo la kisiasa tutalitatua kwa kukamata watu na kuwafikisha mahakamani. Kwa kufanya hivyo, tutajikuta tunamchafua Rais aliyeko madarakani na nchi kwa ujumla.

Sitanii, kwa hatua iliyofikiwa DPP nikuombe utumie busara ya Mfalme Suleiman katika kubaini mtoto ni wa nani.

Mama mmoja alisema mtoto auawe, akatwe vipande viwili kila anayedai ni wake apewe kipande akazike. Aliyekuwa mama wa kweli akasema ni bora mama wa kusingizia amchukue huyo mtoto angalau atakuwa anamwona, anampungia mkono akiwa hai. Mfalme Suleiman kwa kauli hizo mbili akabaini mama halisi wa mtoto.

DPP wakati umefika utumie Kifungu cha 91 cha Sheria ya Mwenendo wa Mashitaka (CPA) kuondoa kesi ya Mbowe mahakamani. IGP na DCI niwaombe sana neno ugaidi msilitumie tena, linachafua sura ya Tanzania. Mbowe ni Mtanzania. Zungumzeni naye, mwelezeni umuhimu wa uzalendo kwa taifa letu.

Lakini pia msikilize na kesi zake za kuvunjiwa ukumbi wa Bilcanas. Msumeno ukate pande zote. Ninarudia, si kila kesi ya kisiasa tutaimaliza kwa kuifikisha mahakamani. Tuvuke huu msitari unaoleta sura ya ubabe. Mungu ibariki Tanzania.
👍👍
 
uliwahi kusikia ugaidi unadhaminiwa kwa sh 600,000 dola 260? Ikiwa sabaya ni mwema alitaka agaidiwe na mbowe kwa nini mnataka kumfunga.

learn to think in three dimensions
Kwani kesi zote si zipo mahakamani!?
 
Back
Top Bottom