Umuofia kwenu!!
Kama mada ilivyo, nimempeleka kwanza kwao kwa muda usiopungua miezi miwili.....akajifunze kitu (kama ni mwenye kujifunza). Siku moja tu baada ya kutoka kwake;
1. Leo kwa mara ya kwanza, katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu, nimefanikiwa kutulia nyumbani saa mbili usiku na kuangalia taarifa ya habari mwanzo mwisho. Kabla, ilikuwa sikai maana nikibadilisha channel tu na kuweka kituo changu pendwa cha Star TV kuangalia taarifa basi manung'uniko yenye kukera huanza kukimbizana kutoka nje ya kinywa chake.
"Tutaacha vp kubadilishiwa channel wakati TV sio yetu na hata bei yake hatuijui..."
"Hata kuzima we zima tu, nini kubalisha channel" Dah
2. Nimepumzika kushuhudia mabega na makwapa ya mke wangu yakionwa na watoto muda wote awapo nyumbani. Jitihada za kumrekebisha ili aendane na desturi yangu, daima huenda sambamba na ugomvi.
3. Nimepumzika kuona sura ya kununanuna pale ninapotoa maelekezo.
4. Udokozi wa vielfu tano tano vyangu katika tigopesa yangu utakoma kwa muda.
5. Nitapumzika kusikia matusi kama 'nyoko we' n.k yanayotolewa kwa watoto kila siku.
6. Nitafurahia vichenji vinavyobaki katika matumizi madogomadogo na kuziweka mezani. Kwa kawaida hivi hutoweka dakika moja tu baaada ya kuviweka, hata kama akiwa amelala basi huamka ghafla na kuvichukua kisha kulala tena.
Mbona nina furaha sana sasa?!!! Atarudi kweli? Arudi ili nije kupata stress tena?
Ndoa..........mh!
Kama mada ilivyo, nimempeleka kwanza kwao kwa muda usiopungua miezi miwili.....akajifunze kitu (kama ni mwenye kujifunza). Siku moja tu baada ya kutoka kwake;
1. Leo kwa mara ya kwanza, katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu, nimefanikiwa kutulia nyumbani saa mbili usiku na kuangalia taarifa ya habari mwanzo mwisho. Kabla, ilikuwa sikai maana nikibadilisha channel tu na kuweka kituo changu pendwa cha Star TV kuangalia taarifa basi manung'uniko yenye kukera huanza kukimbizana kutoka nje ya kinywa chake.
"Tutaacha vp kubadilishiwa channel wakati TV sio yetu na hata bei yake hatuijui..."
"Hata kuzima we zima tu, nini kubalisha channel" Dah
2. Nimepumzika kushuhudia mabega na makwapa ya mke wangu yakionwa na watoto muda wote awapo nyumbani. Jitihada za kumrekebisha ili aendane na desturi yangu, daima huenda sambamba na ugomvi.
3. Nimepumzika kuona sura ya kununanuna pale ninapotoa maelekezo.
4. Udokozi wa vielfu tano tano vyangu katika tigopesa yangu utakoma kwa muda.
5. Nitapumzika kusikia matusi kama 'nyoko we' n.k yanayotolewa kwa watoto kila siku.
6. Nitafurahia vichenji vinavyobaki katika matumizi madogomadogo na kuziweka mezani. Kwa kawaida hivi hutoweka dakika moja tu baaada ya kuviweka, hata kama akiwa amelala basi huamka ghafla na kuvichukua kisha kulala tena.
Mbona nina furaha sana sasa?!!! Atarudi kweli? Arudi ili nije kupata stress tena?
Ndoa..........mh!