Wapendwa, nimeona mjadala juu ya kiti cha Rais na nikaonelea nitoe maelezo kidogo. Kanisa katika protocol zake inatambua na kuwaheshimu viongozi katika hadhi zao mbali mbali.
Hii protocol siyo ya sasa au jana ni ya miaka mingi. Rais ni kiongozi wa nchi hivyo hadhi yake ni hadhi ya nchi siyo yake binafsi.
Kwa sababu ya unyenyekevu wa viongozi wetu, kiti cha Rais kilikuwa kumebanwa kati ya mabenchi amezungukwa na masista na watu wengine. Kikawaida ingebidi sehemu moja ya kanisa benchi ziondolewe na kipangwe kiti chake rasmi na wapambe wake.
Hiyo ndiyo protocol halisi ya Mkuu wa Nchi anayekuja rasmi kwa dhifa ya kitaifa kama Rais wetu alivyokuja kwa kumbukumbu ya kitaifa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Hiyo si heshima kwake bali kwa nchi. Hewala si utumwa, tukikosa heshima kwa viongozi wetu tutakosa heshima hata nyumbani mwetu.
Tunatoa shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wengine wa Taifa kuungana nasi katika ibada ya kumwombea Baba wa Taifa. Ni jambo jema sana.
Hata kanisani tunaheshimu siyo mtu binafsi lakini nafasi yake anayoishika. Kwa mfano Kardinali akiwa yeye haongozi ibada hakai pembeni na maaskofu wengine bali anapewa kiti maalumu kwa heshima yake. Unashukuru wat wa Itifaki ya Ikulu waliotuazima viti walau tukatoa heshima hiyo ndogo kwa mgeni wetu maalumu wa siku hiyo.
Ndugu zangu nimeona nitoe maelezo hayo kwa sababu niliona hoja inakua bila kutazama protocol za kanisa na heshima zake. Vile vile hakuna katazo kiti Fulani kisiingie kanisani ndiyo sababu unaona hata viti vya plastic vinavyotumika sehemu nyingine vinawekwa kanisani watu wakiwa wengi.
Nachukua fursa hii kuwashukuru waamini wa Bukoba Kanisa Kuu na parokia Jirani kwa kuungana nasi kwa wingi kumwombea Baba wa taifa. Mungu awabariki.
Askofu Method Kilaini
Hii protocol siyo ya sasa au jana ni ya miaka mingi. Rais ni kiongozi wa nchi hivyo hadhi yake ni hadhi ya nchi siyo yake binafsi.
Kwa sababu ya unyenyekevu wa viongozi wetu, kiti cha Rais kilikuwa kumebanwa kati ya mabenchi amezungukwa na masista na watu wengine. Kikawaida ingebidi sehemu moja ya kanisa benchi ziondolewe na kipangwe kiti chake rasmi na wapambe wake.
Hiyo ndiyo protocol halisi ya Mkuu wa Nchi anayekuja rasmi kwa dhifa ya kitaifa kama Rais wetu alivyokuja kwa kumbukumbu ya kitaifa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Hiyo si heshima kwake bali kwa nchi. Hewala si utumwa, tukikosa heshima kwa viongozi wetu tutakosa heshima hata nyumbani mwetu.
Tunatoa shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wengine wa Taifa kuungana nasi katika ibada ya kumwombea Baba wa Taifa. Ni jambo jema sana.
Hata kanisani tunaheshimu siyo mtu binafsi lakini nafasi yake anayoishika. Kwa mfano Kardinali akiwa yeye haongozi ibada hakai pembeni na maaskofu wengine bali anapewa kiti maalumu kwa heshima yake. Unashukuru wat wa Itifaki ya Ikulu waliotuazima viti walau tukatoa heshima hiyo ndogo kwa mgeni wetu maalumu wa siku hiyo.
Ndugu zangu nimeona nitoe maelezo hayo kwa sababu niliona hoja inakua bila kutazama protocol za kanisa na heshima zake. Vile vile hakuna katazo kiti Fulani kisiingie kanisani ndiyo sababu unaona hata viti vya plastic vinavyotumika sehemu nyingine vinawekwa kanisani watu wakiwa wengi.
Nachukua fursa hii kuwashukuru waamini wa Bukoba Kanisa Kuu na parokia Jirani kwa kuungana nasi kwa wingi kumwombea Baba wa taifa. Mungu awabariki.
Askofu Method Kilaini