Askofu Ruwaichi: Wajumbe wa Tume ya Uchaguzi kuteuliwa na Rais wanakosa Uhuru

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Akiwasilisha maoni mbele ya Kamati ya Bunge kuhusu na Miswada ya Sheria za Uchaguzi iliyowasilishwa na Serikali Bungeni, Askofu Mkuu wa Jimbo la Kanisa Katoliki Dar es Salaam, Askofu Jude Thaddaeus Ruwai'chi amesema Uhuru wa Wajumbe hao unapaswa kutiliwa maanani kwasababu Uteuzi wao unatoka kwa Rais.

Ameongeza kuwa Tume hiyo inapaswa kuwa na muundo wa Kijaji ikiwa na Watendaji ambao ni Majaji kama Tume iliyoundwa kuchunguza Majaji wanaochunguza Ukiukwaji wa Maadili ili iweze kutoa maamuzi yanayokubalika na kuheshimika.

Aidha, amependekeza Wajumbe wa Kamati ya Usaili inapaswa kuanzishwa kwa Mujibu wa Katiba ya Tanzania na wasitokane na uteuzi wa Rais huku akitolea mfano wa Kenya ambako Wajumbe Kamati hiyo Huteuliwa na Tume ya Utumishi ya Bunge, Chama cha Sheria, Baraza la Viongozi wa Dini na baadaye Rais hupewa majina kwaajili ya kutangaza Uteuzi wao.

==========

"Hata Wajumbe wa Kamati hiyo wote kwa sehemu kubwa ni wateule wa Rais na hivyo uhuru wao ni wa kutia maanani, ni vyema kabisa kuwa Kamati hii iwe ya Majaji kama ile iliyoundwa kuchunguza mambo yanayohusu Majaji wanapochunguzwa dhidi ya ukiukwaji wa maadili ili iweze ikatoa maamuzi yanayoheshimika na kukubalika" -Askofu Ruwai'chi

"Kifungu cha 5(2) kinasema kuwa Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe watashika nafasi zao baada ya kuapishwa na Rais, kwa mujibu wa kifungu cha 8(1) muda wa Utumishi wa Wajumbe umetajwa kuwa ni miaka Mitano (5) sawa na Ibara ya 74, Kifungu cha Nne (4) cha Katiba inavyosema, aidha kifungu hicho cha 8(2) kinatoa sababu ya ukomo wa Utumishi wa Mjumbe kuwa ni pamoja na kumalizika kwa muda wa miaka Mitano (5) tangu alipoteuliwa, ikiwa amefariki, ikiwa amejiuzuru au kujitokeza jambo lolote ambapo tangu alipoteuliwa ikiwa asingekuwa Mjumbe asingeweza kuteuliwa au ameondolewa na Rais kutokana na sababu mbalimbali kama uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa sababu ya maradhi au kwa sababu nyingine yoyote au pia kwa sababu ya tabia mbaya, kupoteza sifa ya kuteuliwa kuwa Mjumbe, kigezo cha kutokea kwa jambo lolote ambapo kama asingekuwa Mjumbe asingeweza kuteuliwa ni Kigeni na hakipo kwenye Katiba, mandhari Katiba imetoa vigezo, sababu zinzoweza kusababisha mtu kuondolewa basi hizo ndizo kigezo halali na cha kuzingatia" -Askofu Ruwai'chi

"Kamati ya Usaili inaundwa na Kifungu cha 9(1) na kujumuishwa Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, Jaji Mkuu wa Zanzibar ambaye atakuwa Makamu Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Mjumbe mwingine mmoja atakayeteuliwa na Rais kwa kuzingatia Jinsia, isitoshe kusema kuwa hiki ni kitu kipya na kama tulivyosema hiki ni kitu ambacho hakimo katika Katiba, ili Kamati hii iweze kuwa na nguvu na iaminike ni lazima ianzishwe na Katiba na vile vile Wajumbe wake wawe ni tofauti na hawa ambao wanaonekana ni wateule wa Rais" -Askofu Ruwai'chi

"Kwa pale Nchini Kenya kwa mfano Wajumbe wa Kamati ya usaili wanateuliwa na Vyombo vya Kisheria ikiwemo Tume ya Utumishi wa Bunge, Chama cha Sheria cha Kenya, Baraza la pamoja la Viongozi wa Dini na Rais yeye hupelekewa majina ili atangaze uteuzi na sio kuwateua" -Askofu Ruwai'chi

"Kifungu cha 10(1) kinaonyesha kuwa Mwenyekiti na Makamu wake wataeuliwa na Rais moja kwa moja na wao hawahusiki na mchakato wa usaili, hili ni sawa kwani Katiba haidai hivyo lakini kosa la sheria ni kule kuwafanya Mwenyekiti na Makamu wake wasiwe Wajumbe wakati tayari Katiba inawaita ni Wajumbe, hivyo vyote ambavyo vinapendekezwa na Sheria juu ya Kamati ya usaili ni Batili" -Askofu Ruwai'chi
 
100% yupo sawa. Kama kweli CCM wanataka uchaguzi huru, wenye haki na uwazi.

Kitu kidogo sana kukifanya lakini watatoa sababu zisizo na maana yoyote kukwamisha tume huru.
 
Rais akiamua kutumia madaraka yake vibaya, hata kama hao wajumbe wakipatikana kwa kupigiwa kura na wananchi hawatoweza kuwa huru!

Mimi nitaendelea kuamini kwamba, suala la uhuru linaanzia kwa mtu anayeteuliwa, yeye mwenyewe ndani yake yupo huru? Anafahamu haki na kiapo chake kinamtaka afanye nini?

Hatuwezi kamwe kuwa na taasisi huru kwenye nchi hii kama hatutopata watu huru na wanaojitambua, watu wasio na tamaa za mali wala vyeo!
 
CCM na Samia wanafanya maigizo, hawako tayari kuona unafanyika uchaguzi huru kwa sababu ya uchu wa madaraka walionao. Samia anajua uchaguzi ukisimamiwa na tume huru hawezi kurudi ikulu labda kuja kuaga tu.
 
CCM na Samia wanafanya maigizo, hawako tayari kuona unafanyika uchaguzi huru kwa sababu ya uchu wa madaraka walionao. Samia anajua uchaguzi ukisimamiwa na tume huru hawezi kurudi ikulu labda kuja kuaga tu.
Wewe unawaza kama mimi. Hawa wanatuchezea tu akili. Maana hiyo jeuri ya kuruhusu uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi, hawana. Ni kama tu wanavyopiga chenga mchakato wa Katiba Mpya.
 
Rais akiamua kutumia madaraka yake vibaya, hata kama hao wajumbe wakipatikana kwa kupigiwa kura na wananchi hawatoweza kuwa huru!

Mimi nitaendelea kuamini kwamba, suala la uhuru linaanzia kwa mtu anayeteuliwa, yeye mwenyewe ndani yake yupo huru? Anafahamu haki na kiapo chake kinamtaka afanye nini?

Hatuwezi kamwe kuwa na taasisi huru kwenye nchi hii kama hatutopata watu huru na wanaojitambua, watu wasio na tamaa za mali wala vyeo!
Kwa nini isiwekwe sheria yaani kuwepo na katiba ambayo ni huru kisheria na basi kama ikatokea wamepatikana wajumbe wa kamati ambao nia zao siyo nzuri basi wabanwe na sheria ili waje kwenye mstari.
 
Kwa nini isiwekwe sheria yaani kuwepo na katiba ambayo ni huru kisheria na basi kama ikatokea wamepatikana wajumbe wa kamati ambao nia zao siyo nzuri basi wabanwe na sheria ili waje kwenye mstari.
Sheria zipo na zinasema wazi kabisa kuhusu uhuru wa Tume ya uchaguzi. Je ni kweli wapo huru?
Matatizo ya hii nchi ni makubwa sana na hayawezi kumalizwa na sheria.
 
Binafsi naona mchakato unaweza kufanyika, lakini bado naamini hatutakuwa na tume huru.
Mchakato wa kuwapata hao watumishi wa tume huru nao utakuwa na kasoro zitakazo pelekea kupita mapandikizi ya wenye mamlaka..
Mpaka sasa naamini kuna watu ambao si wanasiasa wazi wazi ndio watakaopita ili kuaminishwa kuwa hawakuwa wanachama wa chama chochote.
Tungejikita kubadili katiba yote, haya mengine pia yangepatikana kwa urahisi.
 
CCM na Serikali yao wana kazi sana... haya yote wayachuje na wayachakachue? Hivi hawachoki?
 
Nilimfuatilia Mhashamu Baba Askofu Mkuu wa Dar es salaam akitoa sababu za TEC mbele ya Kamati ya Bunge kuhusu kuboresha Muswada wa Sheria ya uchaguzi kwa kweli nimewakubali. Wametoa zaidi ya sababu 27 kuboresha Sheria hii na ninaiomba Serikali izingatie kwa asilimia 90 sababu walizotoa ili uchaguzi ujao uwe huru na wa haki. Kwa kweli nimewakubali TEC ina wasomi na wana uelewa mpana sana.
 
Sababu za kitoto 🤣🤣hata wanafunzi wanaweza kutoa...Tunataka kuona msimamo wao juu ya Papa acheni kuzunguka sana.


Hao jamaa zako hata Nondo yule wa ACT wazalendo hawamfikiii kwa uelewa wa mambo ya siasa...
 
Sababu za kitoto 🤣🤣hata wanafunzi wanaweza kutoa...Tunataka kuona msimamo wao juu ya Papa acheni kuzunguka sana.


Hao jamaa zako hata Nondo yule wa ACT wazalendo hawamfikiii kwa uelewa wa mambo ya siasa...
We mjinga
 
Back
Top Bottom