Mimi ni United, shida ya Arsenal si kwamba ni timu mbaya hapana ni timu Bora sana, lakini wanachokosa Arsenal ni ile Personality na Maturity, unajua kwenye mpira kuna ile mentality Fulani ya kubeba majukumu as if una share ya umiliki kwenye timu, kama utakuwa unaangalia vizuri na unaujua mpira bila mapenzi utaona timu zote zinazochukua makombe zina hizo sifa, unaweza kuona timu hii mbona haichezi vizuri lakini inachukua makombe ni kwasababu ya burning desire iliyo kwenye mioyo ya wachezaji.
Vipaji na mifumo haitoshi, Inahitaji uwe na wachezaji wa aina hiyo ambao wao Kila nafasi ama dakika ina maana kwao, Juzi Inter Milan na Barca Kila timu ilikuwa inajua muda wowote tunaweza kufunga goli, Kila mara ni keep pushing, Sasa Arsenal wao wanafuata tu njia za kocha na kucheza vipaji vyao lakini wamesahau kuwekeza kwenye akili, pindi tu Arsenal players wakiwa na ile akili ya kibingwa watavunja gundu lao na kufika mbali sana.
Arsenal wameziacha mbali timu nyingi hasa kiuchezaji, Inahitaji uwe na timu kuifunga Arsenal. Vipaji na mbinu havitoshi , good personality ndiyo iliwafanya Madrid wachukue UEFA back to back na si kwamba Zidane alikuwa ni kocha Bora sana hapana bali wale jamaa Kina Toni kroos, Modric, Cristiano, Casemiro, Ramos, Marcelo walikuwa wanajua tunaenda kufanya Nini kiasi ambacho hata bila kocha wanacheza.