Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Timerlane nakubaliana na wewe. Kinachoigharimu Arsenal kwa sasa ni hofu ya kisakolojia ya kushinda makombe, ubora wa Arsenal ndani ya hii misimu 3 ni mkubwa mno. Mshambuliaji wa kati pekee hatoshi kubadili psychological fear.

Confidence huja hata kwa kubeba vikombe vidogo vidogo kama FA na Carabao ila ukikaa muda mrefu bila kikombe hata uwe na ubora mkubwa kiufundi wachezaji wanakuwa hawana ile mentality ya kushinda makombe.
 
Arteta ni mwanafunzi wa Pep kwa asilimia kubwa, hili halina ubishi. Amechukua mbinu nyingi toka kwa Pep akiwa City iliyokuwa na Gundogan, Silva, Bernado, KdB, Aguero, Mahrez, Sane, n.k. Na pengine ameangalia mbinu za Pep akiwa Barca iliyokuwa na Xavi, Messi, Busquet na Iniesta. Kwa lundo la talents kama hizi Pep alikuwa hatumii nguvu kubwa kufikisha ujumbe wake kwa wachezaji na matokeo yanapatikana. Ndio maana jamaa hakuwa anawekeza sana kwenye CF kwenye timu zake.
Ila sasa Arteta anataka kucheza bila CF (eti Merino/Kai) halafu support ya attacking brains inatoka kwa Odegaard, Martinelli, Saka na Rice.

Mngechukua kombe ilikuwa dhihaka kubwa sana kwa ulimwengu wa mpira. Kila siku humu tunawaambia tatizo ni Arteta, ninyi mnawalaumu Kroenke.
Rice sio mchezaji wa 105miliions, hana tofauti na Henderson wa Liverpool ambaye media za uingerezz zilitaka apewe Ballon d Or
Kina Masingeli wenyewe wanakwambia Tetea ndie mwalimu wa Pep
Project ya Mikel Arteta ndani ya Arsenyo inafikirisha sana, sidhani kama inaweza kukumbukwa na kupewa heshima na mashabiki wa soka kwa kila msimu kumaliza mikono mitupu.
Tetea anapaswa kulaumiwa sana na mashabiki wa Arsenalia kwa timu kutokubeba makombe.
Kila mwisho wa msimu mashabiki wanakua na matarajio makubwa ya msimu ujao bila ya kuwaza msimu unaofata wapinzani nao wanajipanga ili warejee wakiwa washindani wa kweli.
Kuna timu 2 kati ya Chelsea, Manchester na Spurs zina nafasi kubwa ya kubeba ndoo msimu huu, hivyo watakuwa na msimu Bora kuliko Arsenyau na Tetea wake.
1746696164752.jpg
 
Jamaa kaongea ukwel mtupu

Shida sio wachezaji wa Arsenal shida ni Mashabiki wanaamini mno kuwa team yao ni team bora😃😃kumbe ni version ya Tottenham iliyochangamka
Arse8 na Makolokolo ni mapacha kabisa, wote ni kamdomo wala huwa hawana hata sekunde ya kuheshimu wapinzani wataokutana nao kimchezo.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Mna nini Cha kutuambia baada ya kupoteza mchezo?
verifaidi yuza wewe ni wa kukimbia jukwaa?😃
mkorea ungeingilia kati na karate uwavhape PSG maana ndugu zenu arse8 walianza kukabia hadi mikono
Castr nilikuambia ni rahisi ngamia kupenya tundu la sindano kuliko aseno kuchukua UEFA
Do you see?
Nikakuahidi Aseno akichukua UEFA mwaka huu najitoa jf 😂
HENRY14 njoo tu angalau usafishe nyota ya kupiga picha na PL yetu maana dah
Kikombe mnachoweza nyie ni Cha kahawa tu
Tuache kidogo 😂🙌🏾
 
Ukitaka kujua hawa watu kuna mahali kuna shida. subiri wiki ipite,warudi kudanganyana tena. yaani kama watoto vile.

Watakwambia mafanikio yao wamejitahid wamefika nusu fainali na kumfunga madrid, utawasikia wakikwambia EPL hawajaweza kuchukua kisa marefa wa EPL wanawaonea, ukiwauliza vipi mashindano mengine ambayo hamuonewi mbona hamjachukua?

Ukiwaambia pia Arteta ni tapeli watakukatalia.
 
Mimi ni United, shida ya Arsenal si kwamba ni timu mbaya hapana ni timu Bora sana, lakini wanachokosa Arsenal ni ile Personality na Maturity, unajua kwenye mpira kuna ile mentality Fulani ya kubeba majukumu as if una share ya umiliki kwenye timu, kama utakuwa unaangalia vizuri na unaujua mpira bila mapenzi utaona timu zote zinazochukua makombe zina hizo sifa, unaweza kuona timu hii mbona haichezi vizuri lakini inachukua makombe ni kwasababu ya burning desire iliyo kwenye mioyo ya wachezaji.

Vipaji na mifumo haitoshi, Inahitaji uwe na wachezaji wa aina hiyo ambao wao Kila nafasi ama dakika ina maana kwao, Juzi Inter Milan na Barca Kila timu ilikuwa inajua muda wowote tunaweza kufunga goli, Kila mara ni keep pushing, Sasa Arsenal wao wanafuata tu njia za kocha na kucheza vipaji vyao lakini wamesahau kuwekeza kwenye akili, pindi tu Arsenal players wakiwa na ile akili ya kibingwa watavunja gundu lao na kufika mbali sana.

Arsenal wameziacha mbali timu nyingi hasa kiuchezaji, Inahitaji uwe na timu kuifunga Arsenal. Vipaji na mbinu havitoshi , good personality ndiyo iliwafanya Madrid wachukue UEFA back to back na si kwamba Zidane alikuwa ni kocha Bora sana hapana bali wale jamaa Kina Toni kroos, Modric, Cristiano, Casemiro, Ramos, Marcelo walikuwa wanajua tunaenda kufanya Nini kiasi ambacho hata bila kocha wanacheza.
Comment bora kabisaa hii. 👏👏👏👏
 
Back
Top Bottom