Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hapa duniani timu ninayoipenda kuliko zote ni Arsenal FC ikifuatiwa na Simba SC na national teams za Tanzania na France.

Lakini niseme wazi kwamba kwa jinsi Arsenal inavyocheza mpira slow basi hatutakuja kamwe kubeba makombe makubwa.

Aina ya mpira wetu ungeweza kuwa hatari sana kama tungecheza kwa kasi. Kucheza taratibu hivi kunataka uwepo wa wachezaji exceptional ili kuweza kubeba makombe.

Barcelona iliweza kubeba makombe kwasababu walikuwa na Messi, Xavi na Iniesta, pia Puyol, Alves, Bosquet, Pique, Villa etc. Mara kadhaa walicheza kwa kasi na kupiga counter lakini mostly walitegemea hao wachezaji hatari.

Sasa hapa kwetu Arsenal kuna wachezaji sita ambao angalau wana winning mentality ni Rice, Saliba, Martinelli, Trossard, Partey na Saka. Na hawa wote ukiondoa Saliba na Rice ni normal players, sio exceptional.

Wachezaji ambao nawaona ni squad players na watakupa output ya kueleweka mostly kwenye mechi ndogo ni Odegaard, Magalhaes, White, Zinchenko, Tomiyasu na Gabriel Jesus. Nawapa muda Kiwior na Raya.

Wachezaji mizigo ni Elneny, Nelson, Havertz, Vieira, Nketiah, Rowe, Ramsdale na Soares. Hawa waondolewe haraka maana hawana faida yoyote. Akina Lokonga na Marquinhos waliopo mkopo wasirudi.

Kwahiyo katika hali hii nategemea Arsenal tutatolewa UCL kwenye robo fainali na tutaingia top 4 ya EPL kwa tabu sana. Tutatolewa FA siku chache zijazo.

Mwezi huu wa December tunaweza kupata point chache sana maana tumeshapoteza kwa aston villa na hapo bado broghton, liverpool, westham na fulham.

January apatikane beki wa kati, winga wa kulia na mshambuliaji hatari ili angalau kuokoa jahazi lisizame kuanzia February 2024.

Arteta na Edu waache kuleta wachezaji laini na waache huu mpira slow slow.
Niliandika hapa watu wakatukana. Tumeishia kupata point 4 mwezi december baada ya michezo mitano.

Kuanzia kwa Arteta mpaka timu yenyewe hakuna quality na spirit ya kuweza kubeba kombe kubwa.

Apatikane kocha ambaye ni tactical na sio huyu anapiga pasi zisizokuwa na umuhimu na mpira wake predictable.
 
Niliandika hapa watu wakatukana. Tumeishia kupata point 4 mwezi december baada ya michezo mitano.

Kuanzia kwa Arteta mpaka timu yenyewe hakuna quality na spirit ya kuweza kubeba kombe kubwa.

Apatikane kocha ambaye ni tactical na sio huyu anapiga pasi zisizokuwa na umuhimu na mpira wake predictable.

Sure, tunacheza mpira wa taratibu no quick passing of the ball. Tunahitaji mabadiliko
 
N
Kuna mdau humu alituambia Real Madrid and Manchester City pekee ndio washindani wa Arsenal kwenye Champions league au alikuwa anatania ?
Nafikiri yalikuwa maoni yake binafsi kulingana anavyoilewa asenali,ila binafsi asenali sijawahi kumtarajia awe bora sana kama wanavyoiona baadhi ya mashabiki.

Mfano kuna wengine walifurahia kuona Christmas asenali yupo juu wakajua ndio itadumu😂,asenali ni mtego 😂😂😂
 
1698828249198.jpg
 
Maoni yangu ni haya na hayatendelea kubadilika kama die hard fans mnaamini Arsenal atabeba EPL or champions league trophy under Arteta na kina Saka basi kutakuwa na tatizo la akili somewhere HAPPY NEW YEAR GUYS!
Sasa ni wakati rasmi muanze mbio za kuiskaka top four. Habari za ubingwa waachieni wenye pumzi zao za kufukuzia ubingwa.
 
Niliandika hapa watu wakatukana. Tumeishia kupata point 4 mwezi december baada ya michezo mitano.

Kuanzia kwa Arteta mpaka timu yenyewe hakuna quality na spirit ya kuweza kubeba kombe kubwa.

Apatikane kocha ambaye ni tactical na sio huyu anapiga pasi zisizokuwa na umuhimu na mpira wake predictable.
Kocha mbwa kabisa umbwa mkubwa.
 
Back
Top Bottom