UCHAMBUZI BAADA YA MECHI 19 KUTAMATIKA
JE TUNACHEZAJE?
4-3-3 YA ARTETA
Arsenal kwenye karatasi anaingia na 4-3-3 kama kawaida Toka msimu uanze lakini Huwa haiko hivyo mechi ikianza na hapa ndo pamekuwa na taabu kwa timu pinzani kupata matokeo mbele ya Arsenal, Arsenal akiwa na mpira anatumia mabeki watatu wanne anakuwa kiungo(Zincheko), Arsenal akifanya build up inaanza kwa kipa na anatumia mabeki wawili wa Kati (Saliba & Gabriel) mbele ya Ramsdale kwa namna hii timu nyingi zinashindwa kuikaba Arsenal katikati kwasababu zinaamini ni ngumu mpira kuanzia pale,ndo maana team karibia zote EPL ukowatoa city waliobaki wote Build up inafanywa na mabeki wa pembeni na sio Kati.
Arsenal akiwa na mpira anakuwa na namba 6 wawili (Zincheko & Partey) hawa ni wachezaji wenye uwezo mkubwa upande wa kupiga pasi za kila Aina,kudrible na kuamua timu icheze vipi...timu nyingi zinakuja kutia pressure kwenye mpira na zinaacha maeneo ya wazi mengi ambayo Huwa yanashambuliwa na namba 8 wawili wa Arsenal (Xhaka & Odegaard) wakati huo Saka na Martinelli wakiwa wamwutanua uwanja kila mtu upande wake mshambuliaji wa Arsenal Huwa anabaki peke ake juu ya Xhaka na Odegaard kitu ambacho kinaitawanya timu pinzani na kuifanya wachezaji wake wawe mbali mbali na hii imekuwa ikiwasaidia Arsenal katika vitu vingi ..
1: Arsenal wakipoteza mpira ,wanawahi kuupata haraka kwasababu kila eneo linakuwa na namba kubwa kuzidi mpinzani.
2: Arsenal akifanikiwa kufika Hilo eneo ni ngumu kumzuia kwasababu anatengeneza Overload (Idadi kubwa ya wachezaji) inaongezeka kwasababu mabeki wa pembeni Tayari wanakuwa wanatembea kila zone ya uwanja (Kukaba, kucheza na kushambulia) hii ndo inafanya mipira mingi inayopita kushoto utamuona Zincheko akipita zone zote kama ilivyo kwa kulia Ben White utamkuta kwenye Beki,zone ya katikati ya uwanja pembeni,na zone ya mwisho ushambuliaji akiwa anaenda sambamba na Saka .
Arsenal ispokuwa na mpira kwenye Ile formation ya 4-3-3 Huwa ni tofauti kabisa,Kuna mechi Arsenal inacheza kawaida sana na haipotezi kwasababu idadi ya wachezaji wanaokaba na wanaozuia ni kubwa kuliko Idadi ya wachezaji wanaocheza na kushambulia kutoka timu pinzani.
3: Arsenal kwa hizi mechi 19 amekuwa Mfalme kwenye (Rest defense).Rest defense ni kile kitendo Cha mabeki kukaa kwenye mfumo wao wa ulinzi muda timu yao anashambulia.Hakuna timu EPL kwasasa inayoweza kufanya hiki kitu kwa usahii kama Arsenal, Arsenal akiwa na mpira ukiwa mguuni mwa beki yoyote ,beki wengine wanakuwa kwenye shape Yao ya ulinzi vilevile,ukishatoka eneo la mabeki kwenda kwa Viungo bado mabeki wanapanda kwenye msitari usiopishana hili kuzuia counter attacks na hii ndo imefanya wawe wagumu kupoteza mechi zao.
Arsenal akiupoteza mpira mara nyingi Huwa anafanya haya mawili
1:Wale wanne wanarudi haraka eneo lao na Xhaka anarudi chini eneo sawa na Partey huku Saka/Martinelli/Ode wakiweka presha kwa mtu mwenye mpira Nketiah/Jesus Huwa anasogea chini eneo la Odegaard hili kuwazuia mabeki wawili wa Kati wasiende mbali kuishambulia ngome ya Arsenal .hii njia ya overload ambayo Arsenal anaitumia ni ngumu kutoka salama kwa kila shambulio unalofanya au unalofanyiwa kwasababu kila mpira na kila eneo unakuta wachezaji wa Arsenal ni 3vs2 4vs2 na hii ndo system iliyoifanya Arsenal ifike hapa Leo.
2:Kuweka presha mbele ya mpira na kwa mchezaji mwenye mpira unazuia njia ya upigaji wa pasi za mbele zenye madhara,na kama itapigwa ikiuvuka msitari mmoja inakutana na mtihani kama ule ule uliotoka kuufanya.
By the way, Arsenal imefungwa goli Zaidi ya 60% ni Makosa binafsi na sio ubora wa wapinzani kimbinu na kimfumo.
Points 50
Mechi 19
It's unbelievable
