Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Man u mechi nzima walikuwa na touches kwenye box la Arsenal 12 tu

Saka pekee alikuwa na touches 13

️ Player of the Match, @Arsenal’s Bukayo Saka


70 touches
13 touches in opposition box (most this season)
37/47 passes completed
4 chances created
5 shots, 2 on target
7th PL goal this season,


3rd Arsenal player to score in 3 successive PL apps v Man Utd
IMG-20230123-WA0019.jpg
 
Acha tu waniite mamluki ila me naongea ukweli, points 8 Kwa pep ni ndogo sana labda kama aendelee kusua sua kama mwanzo

Mfano game ya leo tungesuruhu zilikuwa zibaki point 3 na mchezo mmoja mkononi, tufanye huo mchezo tungeshinda zimekuwa points 6

Sasa unamzidi points 6 pep ambaye bado una game nae home and away, na wote tunajua ukweli ni kwamba city uwezo wa kutupiga anao, kwahiyo kama akishinda hizo game 2 ingekuwa tuna level points

Kama shabiki wa Arsenal nataka sana kubeba hii ndoo ila haitokuwa rahisi hivi kama ambavyo tunataka kujifariji, pep kama kocha mzoefu kuliko wetu na wachezaji wake Wazoefu kuliko wetu

Kuanzia game ya tote city ni kama vile wameamka Fulani hivi na ikitokea waka maintain consistency kuanzia hapa hadi mwisho sio ajabu wao wanaweza, swali je nasie tunaweza?

Tunaweza kucheza under pressure kila game bila kupoteza focus yetu? Tunaweza kumantain hii form hadi mwisho? Tunaweza kuendelea kuwa na focus ata kama ikitokea tukapoteza game kadhaa?

Ukweli ni kwamba haiwezi kuwa rahisi ila kwakuwa hatujafika hapa kwa bahati mbaya basi batuna budi kukomaa tu hadi game ya mwisho, ila ukweli utabaki kuwa sio rahisi kama ambavyo tunataka kuaminishana
Umesema ukweli ila tu nikwambie kwamba asilimia 60 ya michezo migumu arsenal imeshacheza na imepoteza mmoja tu.
Tumu zote ni ngumu ila huwezi kuwa bingwa uingereza bila kuwachakaza vigogo jambo ambalo arsenal wamefaulu kwa 60 % hivyo sina wasiwasi gemu na mancity tutapata ushindi pia mbele ya Pep.
 
Cesc:


“I was lucky enough to be at the training ground recently and it was like I had never been there before. Everything had changed so much. The manager of the training ground said it was 95% Mikel who had changed the whole thing. He’s changed everything…”
The perception of the club in the last few years, a lot of positive messages around the training ground, much bigger facilities, better equipment, the pitches. Everything. You name it. At the entrance they have a symbol of an empty Premier League [trophy cabinet]…
He wants to show the message. It’s an inspiration every day to go there and prove yourself that you really want to put the Premier League [trophy] in there. I think it’s changed the mentality of the club since Arsène left. It is fantastic what he has done.”
All the ACL injuries we used to get. One or two every season. It wreaked havoc with our league performance. Is it luck we haven’t had one for at least a couple of years? The state of that training ground under Wenger. It needed sorting, no question. Mikel knows.
 
Aliyoyaongea yote Pundit wetu Mzee Ambigile Mwasapile ni sahihi kabisa ila alichokosea ni hapa:

"ATAKAYEMALIZA JUU YA ARSENAL NI BINGWA "

Nina uhakika kuna timu zaidi ya 2 zitakazo maliza juu ya Arsenal, je Epl ya msimu huu kutakua na mabingwa zaidi ya wawili?
Vipi bado unaona kuna timu za kumaliza hapo juu?
 
Umesema ukweli ila tu nikwambie kwamba asilimia 60 ya michezo migumu arsenal imeshacheza na imepoteza mmoja tu.
Tumu zote ni ngumu ila huwezi kuwa bingwa uingereza bila kuwachakaza vigogo jambo ambalo arsenal wamefaulu kwa 60 % hivyo sina wasiwasi gemu na mancity tutapata ushindi pia mbele ya Pep.
Pamoja mkuu
 
UCHAMBUZI BAADA YA MECHI 19 KUTAMATIKA

JE TUNACHEZAJE?


4-3-3 YA ARTETA

Arsenal kwenye karatasi anaingia na 4-3-3 kama kawaida Toka msimu uanze lakini Huwa haiko hivyo mechi ikianza na hapa ndo pamekuwa na taabu kwa timu pinzani kupata matokeo mbele ya Arsenal, Arsenal akiwa na mpira anatumia mabeki watatu wanne anakuwa kiungo(Zincheko), Arsenal akifanya build up inaanza kwa kipa na anatumia mabeki wawili wa Kati (Saliba & Gabriel) mbele ya Ramsdale kwa namna hii timu nyingi zinashindwa kuikaba Arsenal katikati kwasababu zinaamini ni ngumu mpira kuanzia pale,ndo maana team karibia zote EPL ukowatoa city waliobaki wote Build up inafanywa na mabeki wa pembeni na sio Kati.
Arsenal akiwa na mpira anakuwa na namba 6 wawili (Zincheko & Partey) hawa ni wachezaji wenye uwezo mkubwa upande wa kupiga pasi za kila Aina,kudrible na kuamua timu icheze vipi...timu nyingi zinakuja kutia pressure kwenye mpira na zinaacha maeneo ya wazi mengi ambayo Huwa yanashambuliwa na namba 8 wawili wa Arsenal (Xhaka & Odegaard) wakati huo Saka na Martinelli wakiwa wamwutanua uwanja kila mtu upande wake mshambuliaji wa Arsenal Huwa anabaki peke ake juu ya Xhaka na Odegaard kitu ambacho kinaitawanya timu pinzani na kuifanya wachezaji wake wawe mbali mbali na hii imekuwa ikiwasaidia Arsenal katika vitu vingi ..
1: Arsenal wakipoteza mpira ,wanawahi kuupata haraka kwasababu kila eneo linakuwa na namba kubwa kuzidi mpinzani.

2: Arsenal akifanikiwa kufika Hilo eneo ni ngumu kumzuia kwasababu anatengeneza Overload (Idadi kubwa ya wachezaji) inaongezeka kwasababu mabeki wa pembeni Tayari wanakuwa wanatembea kila zone ya uwanja (Kukaba, kucheza na kushambulia) hii ndo inafanya mipira mingi inayopita kushoto utamuona Zincheko akipita zone zote kama ilivyo kwa kulia Ben White utamkuta kwenye Beki,zone ya katikati ya uwanja pembeni,na zone ya mwisho ushambuliaji akiwa anaenda sambamba na Saka .
Arsenal ispokuwa na mpira kwenye Ile formation ya 4-3-3 Huwa ni tofauti kabisa,Kuna mechi Arsenal inacheza kawaida sana na haipotezi kwasababu idadi ya wachezaji wanaokaba na wanaozuia ni kubwa kuliko Idadi ya wachezaji wanaocheza na kushambulia kutoka timu pinzani.

3: Arsenal kwa hizi mechi 19 amekuwa Mfalme kwenye (Rest defense).Rest defense ni kile kitendo Cha mabeki kukaa kwenye mfumo wao wa ulinzi muda timu yao anashambulia.Hakuna timu EPL kwasasa inayoweza kufanya hiki kitu kwa usahii kama Arsenal, Arsenal akiwa na mpira ukiwa mguuni mwa beki yoyote ,beki wengine wanakuwa kwenye shape Yao ya ulinzi vilevile,ukishatoka eneo la mabeki kwenda kwa Viungo bado mabeki wanapanda kwenye msitari usiopishana hili kuzuia counter attacks na hii ndo imefanya wawe wagumu kupoteza mechi zao.

Arsenal akiupoteza mpira mara nyingi Huwa anafanya haya mawili
1:Wale wanne wanarudi haraka eneo lao na Xhaka anarudi chini eneo sawa na Partey huku Saka/Martinelli/Ode wakiweka presha kwa mtu mwenye mpira Nketiah/Jesus Huwa anasogea chini eneo la Odegaard hili kuwazuia mabeki wawili wa Kati wasiende mbali kuishambulia ngome ya Arsenal .hii njia ya overload ambayo Arsenal anaitumia ni ngumu kutoka salama kwa kila shambulio unalofanya au unalofanyiwa kwasababu kila mpira na kila eneo unakuta wachezaji wa Arsenal ni 3vs2 4vs2 na hii ndo system iliyoifanya Arsenal ifike hapa Leo.

2:Kuweka presha mbele ya mpira na kwa mchezaji mwenye mpira unazuia njia ya upigaji wa pasi za mbele zenye madhara,na kama itapigwa ikiuvuka msitari mmoja inakutana na mtihani kama ule ule uliotoka kuufanya.

By the way, Arsenal imefungwa goli Zaidi ya 60% ni Makosa binafsi na sio ubora wa wapinzani kimbinu na kimfumo.

Points 50
Mechi 19

It's unbelievable
 
Aaahhh wapi, hawa kwa hayo magoli yao ya kubahatisha kuchukua ubingwa bado sana, mechi 4 za mwisho wa ligi watakua wanapambana na Liverpunda kuwania top4 labda kama huzijui hizi Nyani. View attachment 2491898
Fun fact ya hii picha na off topic ..:
Hii picha huyu kima alijipiga selfie Kwa kuchukua camera ya mpiga picha aliyokuwa ameiacha chini, akijikuta amejipiga. Mpiga picha alivyoenda kuchukua camera yake, kima akasepa.
Baadae wakati wa kudevelop picha jamaa akaikuta hii akawaambia wenzake na wengine kwamba 'hii picha huyu kima alijipiga selfie mjue..'
Shida ikaja alipotaka kuiuza. Umma ukamjia juu kuwa hiyo picha siyo Mali yake bali ni Mali ya yule kima hivyo Hana haki ya kuiuza. Nadhani baada ya mivutano sana walimuachia kama Mali yake na akaweza kuiuza.
 
Kuna kitu watu mnajisahau mnapodai City haiwezi kuizuia Arsenal.

City alikua anaongozwa 2 dhidi ya timu inayopenda kupaki basi na ikayabinua matokeo mpaka kua 4 kwa 2. Imepunguza gape la points vizuri tu.

Ina wachezaji wako exposed kwenye hizi pressure for years. Ina options zaidi ya 1 kwa kila nafasi isipokua kipa (sisi tuna hii quality?).

Arsenal tupo FA (tutakutana nao huko), tupo Europa na tuna hii presha ya ligi. Tuna kikosi cha kutuwakilisha kote huko na tukapata same output? Jibu ni hapana.

Tulicheza na Brighton baada ya siku 3 tukacheza na Newcastle na unaona kabisa kwamba kikosi kina fatique. Its allowed to dream but we should not overstep tukasahau angalia vitu vya msingi
 
Acha tu waniite mamluki ila me naongea ukweli, points 8 Kwa pep ni ndogo sana labda kama aendelee kusua sua kama mwanzo

Mfano game ya leo tungesuruhu zilikuwa zibaki point 3 na mchezo mmoja mkononi, tufanye huo mchezo tungeshinda zimekuwa points 6

Sasa unamzidi points 6 pep ambaye bado una game nae home and away, na wote tunajua ukweli ni kwamba city uwezo wa kutupiga anao, kwahiyo kama akishinda hizo game 2 ingekuwa tuna level points

Kama shabiki wa Arsenal nataka sana kubeba hii ndoo ila haitokuwa rahisi hivi kama ambavyo tunataka kujifariji, pep kama kocha mzoefu kuliko wetu na wachezaji wake Wazoefu kuliko wetu

Kuanzia game ya tote city ni kama vile wameamka Fulani hivi na ikitokea waka maintain consistency kuanzia hapa hadi mwisho sio ajabu wao wanaweza, swali je nasie tunaweza?

Tunaweza kucheza under pressure kila game bila kupoteza focus yetu? Tunaweza kumantain hii form hadi mwisho? Tunaweza kuendelea kuwa na focus ata kama ikitokea tukapoteza game kadhaa?

Ukweli ni kwamba haiwezi kuwa rahisi ila kwakuwa hatujafika hapa kwa bahati mbaya basi batuna budi kukomaa tu hadi game ya mwisho, ila ukweli utabaki kuwa sio rahisi kama ambavyo tunataka kuaminishana
Tuko pamoja kimawazo. Nasubiri tufika game 28-30
 
Back
Top Bottom