Ambangile
Arsenal v Newcastle
.Hii imekutanisha timu mbili ambazo zipo imara haswa kiufundi, kimbinu , utimamu wa kimwili , matamanio ya kupambana uwanjani ... leo kasoro kitu kimoja tu , Arsenal walitaka kucheza boli , kuacha mpira utembee wakati Newcastle waliona njie nyingine ya kupata chochote ni kupoteza muda
.Vitu ambavyo nilivyoviona kwa mara kwa mara
1: Almiron & Joelinton umakini wa kurudi nyuma kusaidia ulinzi kutoruhusu mabeki wao wawili wa pembeni wawe 1 Vs 1 dhidi ya ( Saka na Martinelli )
2: Xhaka na Zinchenko wanavyobadilishana nafasi ya namba 8 wa kushoto mmoja akipanda mwingine anashuka waki offer vertical pass kutoka kwa Partey na beki Gabriel ( yani wanakuwa eneo ambalo inaruhusu ipigwe pasi ya mbele nyuma ya kiungo cha Newcastle )
3: Newcastle mstari wao wa ulinzi haupo chini sana wala haupo juu sana , kwanini ? kuepuka runs nyuma yao dhidi ya utatu wa Arsenal , na pia juu hawa press sana wanawaacha Saliba na Gabriel kuwa na mpira huku wakifunga kwenye midfield
4: Idadi ya wachezaji Arsenal wanaotumia kushambulia hasa kwenye line ya mwisho ya ulinzi ya Newcastle haipungui watu 6 ... ujasiri wa hali ya juu.!
.Eddie Howe alikuwa ameanza kupress kwa 4-3-3 lakini Arsenal kuna nyakati walikuwa wanaishinda hiyo press na ndio maana akaamua kubadilisha kukabia katikati sio juu sana wala chini kwa shape ya 4-5-1 na kumuacha Wilison pekee mbele, ilikuwa ngumu kwa Arsenal kuwafungua Newcastle walizuia vizuri sana
NOTE
1: Nyie hawa Arsenal wapo fit ukifanya masihara wanakutoa damu , muda wote wako busy tu uwanjani
2: Newcastle mechi ya 6 mfululizo hii bila kuruhusu wavu wao kuguswa ( clean sheets 6 mfululizo )
3: Namuelewa Arteta kuchukia dhidi ya mbinu ya Newcastle kupoteza muda hata mimi ningemaindi lakini pia ningekuwa Eddie Howe fresh tu kwasababu nataka kujitetea
4: ATAKAYEMALIZA JUU YA ARSENAL NI BINGWA
FT : Arsenal 0-0 Newcastle