Angalieni hii ramani ya nyumba alafu mnishauri kitu

Angalieni hii ramani ya nyumba alafu mnishauri kitu

Eneo la 150m² ni kusema 10m×15m kwa wastani.

Kuchomoa nyumba ya vyumba vitatu, sebule, jiko na vyoo humo then parking inahitaji kazi ya ziada.
 
Tatizo unapita katikati ya jiko ukitaka kupita mlango wa nyuma. Jikoni ni sehemu nyeti.
Ondoa hiyo dining ongeza ukubwa sebule kidogo weka open kitchen.
Kama ni Ushauri wa faragha

Anapaswa chumba kilicho karibu na masta akihamishe apeleke upande wa kitchen na mbadala wake

Ili akitumia mlango wa nyuma mgeni asione

Sema choo cha public itabidi kihame pia kutosheleza nafasi na chemba zitaongezeka

Halafu hii collection ya typing inayojitokeza jf siipendi imekuwa sijui sehemu sahihi ya kutoa malalamiko

Sidhani kama keypad yangu inasuggest mineno ya hovyo wakati naandika

Jf kama wana ziada kwenye app yao watambue inaletaError
 
Ndugu

Je hii ramani inaenea kwenye eneo la aquare mita 150 na kubakiza sehemu ya kupaki kagari na kuanika nguo.... Naombeni mawazo yenu ikibidi sana naombeni na vipimo

Mimi nilikuwa na waza icheze kwenye square mita 72 au 81 square meter...

Naombeni mawazo yenu na vipimo vizuri kadiri muwezavyoView attachment 3564803
Ramani ya kipuuzi! Kwanni vyumba vya watoto hakuna vyoo vya ndani? Mimi Banda langu vyumba vya watoto nimewawekea masta bedroom.... public toilet ni kwajili ya wageni au Incase of anything
 
Bila vipimo ni ngumu kukadiria

Tuseme kwa mchoro jinsi ulivyo tukadirie kila chumba kina m3×m3, sebule m5×m3, dining m4×m2.5, vyoo kila kimoja m2×m2.5, kitchen, kibaraza cha jikoni na store m5×m2.5

  • Hapo unapata usable space jumla ya msq 73.5

(Hiyo ni usable space haijajumuisha corridor, upana wa kuta na veranda)

Tuje kwenye makadirio ya upana na urefu wa hiyo nyumba

  • Hapo upana wa nyumba ni kama m10 na urefu ni m11 (m10×m11) = msq 121

(Kiwanja cha msq 72-81 hakitatosha kujenga hiyo nyumba ya ndoto yako)

Hautapata hata sehemu ya kupark gari, kabustani kakishikaji, watoto pa kucheza au pa kukaa watu siku ukifa
Siku akifa? Mkuu mbona unamtisha mwenzio
 
Shukrani sana mkuu.. vipi kwenye square meter 150 unaonaje kutakua na sehemu hata ya jumuia kusali?
Makadirio yetu upana na urefu wa nyumba ni sqm 121

Ukisema una kiwanja kina sqm 150 (sqm 150-sqm 121) zinabaki sqm 29 tu

Hapo kwenye hizo sqm 29 utoe vinjia vinavyozunguka nyumba yako unapopakana na majirani zako

Tuseme umetoa m 1.5 za vinjia pande zote nne za nyumba
  • Upana wa nyumba + vinjia=m10+(2×m1.5)= m13
  • Urefu wa nyumba + vinjia =m11+(2×m1.5)= m14

Kwa hiyo upana na urefu wa eneo la nyumba + vinjia kuzunguka nyumba itakuwa m13×m14=sqm 182
Kwa kiwanja cha sqm 150 utakuwa unadaiwa eneo la sqm 32

Hapo haujachimba shimo la choo
 
Makadirio yetu upana na urefu wa nyumba ni sqm 121

Ukisema una kiwanja kina sqm 150 (sqm 150-sqm 121) zinabaki sqm 29 tu

Hapo kwenye hizo sqm 29 utoe vinjia vinavyozunguka nyumba yako unapopakana na majirani zako

Tuseme umetoa m 1.5 za vinjia pande zote nne za nyumba
  • Upana wa nyumba + vinjia=m10+(2×m1.5)= m13
  • Urefu wa nyumba + vinjia =m11+(2×m1.5)= m14

Kwa hiyo upana na urefu wa eneo la nyumba + vinjia kuzunguka nyumba itakuwa m13×m14=sqm 182
Kwa kiwanja cha sqm 150 utakuwa unadaiwa eneo la sqm 32

Hapo haujachimba shimo la choo
Shukran hapo nshakupata mkuu
 
Kuna wakati sqm 450 ilikuwa ndio minimum. Na hapo ni kujenga choo cha shimo tu. Ukitaka ma septic imekula kwako.

Amandla...
 
Tafuta picha za open kitchen utanielewa
Mimi ninavyojua open kitchen iko wazi, hamna ukuta kati ya secure na jiko. Open kitchen ilipata umaarufu kama njia ya kutowatenganisha walio jikoni ( mara nyingi wanawake)na wale waliosebuleni ( mara nyingi wanaume). Wanaopika wanaweza kushiriki katika mazungumzo yanayoendelea sebuleni na wale wa sebuleni wanaweza kushiriki katika mambo ya jikoni.

Kilichofanikisha open kitchen ni kuwa na kitchen hoods zenye nguvu ya kuhakikisha moshi unaotokana na mapishi hauwi kero kwa walio sebuleni.

Kwa tamaduni za wengi wetu open kitchen hazifai kutokana na maeneo kuwa defined kwa jinsia. Jikoni ni kwa wanawake na sebuleni kwa wanaume.

Mgawanyiko huu unawaruhusu wanawake kujikalia wanavyotaka bila kuhofia macho ya wanaume. Na kwa vile nyumba zetu nyingi hazina hoods, harufu yote ya makaangizo pamoja na moshi wake itaishia sebuleni.

Katika migahawa dhana hiyo hiyo imejirudia. Katika migahawa yenye open kitchen design wateja wanaona chakula kinavyopikwa kwa sababu nako hamna ukuta kati ya jiko na sehemu ya kulia. Unaweza kusema mama Ntilie ni mfano wa open kitchen.

Sasa niambie kwa uelewa wako "open kitchen" zikoje. Sio lazima uweke picha. Maelezo tu yatatosha.

Amandla...
 
Open Kitchen
1775072919136.jpeg


Amandla...
 
Bila vipimo ni ngumu kukadiria

Tuseme kwa mchoro jinsi ulivyo tukadirie kila chumba kina m3×m3, sebule m5×m3, dining m4×m2.5, vyoo kila kimoja m2×m2.5, kitchen, kibaraza cha jikoni na store m5×m2.5

  • Hapo unapata usable space jumla ya sqm 73.5

(Hiyo ni usable space haijajumuisha corridor, upana wa kuta na veranda)

Tuje kwenye makadirio ya upana na urefu wa hiyo nyumba

  • Hapo upana wa nyumba ni kama m10 na urefu ni m11 (m10×m11) = sqm 121

(Kiwanja cha sqm 72-81 hakitatosha kujenga hiyo nyumba ya ndoto yako)

Hautapata hata sehemu ya kupark gari, kabustani kakishikaji, watoto pa kucheza au pa kukaa watu siku ukifa
Nimecheka kwa sauti kuu... Hahahahahaha.
 
Mzee m² 150 ni ndogo sana hako kakiwanja ni kadogo mnoo
 
Ndugu

Je hii ramani inaenea kwenye eneo la aquare mita 150 na kubakiza sehemu ya kupaki kagari na kuanika nguo.... Naombeni mawazo yenu ikibidi sana naombeni na vipimo

Mimi nilikuwa na waza icheze kwenye square mita 72 au 81 square meter...

Naombeni mawazo yenu na vipimo vizuri kadiri muwezavyoView attachment 3564803
Mkuu tafuta kiwanja kingine, sq m 150, kwa ramani hiyo kiwanja hakitoshi nyumba itabanana, utakosa hata pa kutemea mate, ramani ni nzuri.

Halafu ukianza ujenzi ramani iongezee kidogo ama jiko ulicancell, maana ninajua hayo majiko ya ndani hayatumiki kupikia ni ya kupashia viporo tu, ili hao wanao nao wawekee vyoo vya self.

Siyo usiku kila mtu kabanwa au asubuhi anataka kuwahi zake mitikasi, waanze kusubiriana, maisha ya hivyo yamepitwa na wakati.

Hicho kilichopo kwenye mchoro kibaki kuwa cha publick.
 
Back
Top Bottom