Angalieni hii ramani ya nyumba alafu mnishauri kitu

Angalieni hii ramani ya nyumba alafu mnishauri kitu

Loading failed

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2023
Posts
2,964
Reaction score
8,242
Ndugu

Je hii ramani inaenea kwenye eneo la aquare mita 150 na kubakiza sehemu ya kupaki kagari na kuanika nguo.... Naombeni mawazo yenu ikibidi sana naombeni na vipimo

Mimi nilikuwa na waza icheze kwenye square mita 72 au 81 square meter...

Naombeni mawazo yenu na vipimo vizuri kadiri muwezavyo
Screenshot_20260328-144528.jpg
 
Bila vipimo ni ngumu kukadiria

Tuseme kwa mchoro jinsi ulivyo tukadirie kila chumba kina m3×m3, sebule m5×m3, dining m4×m2.5, vyoo kila kimoja m2×m2.5, kitchen, kibaraza cha jikoni na store m5×m2.5

  • Hapo unapata usable space jumla ya sqm 73.5

(Hiyo ni usable space haijajumuisha corridor, upana wa kuta na veranda)

Tuje kwenye makadirio ya upana na urefu wa hiyo nyumba

  • Hapo upana wa nyumba ni kama m10 na urefu ni m11 (m10×m11) = sqm 121

(Kiwanja cha sqm 72-81 hakitatosha kujenga hiyo nyumba ya ndoto yako)

Hautapata hata sehemu ya kupark gari, kabustani kakishikaji, watoto pa kucheza au pa kukaa watu siku ukifa
 
Bila vipimo ni ngumu kukadiria

Tuseme tukadirie kila chumba kina m3×3, sebule na dining m4×5, vyoo m2×2, kitchen, kibaraza na store m3.5×2.5

Hapo unapata jumla ya msq 41.75

Itatosha utapata na sehemu ya kupark gari, kabustani kakishikaji, watoto pa kucheza na pa kukaa watu siku ukifa
Pa kukaa watu siku akifa 😅
 
Bila vipimo ni ngumu kukadiria

Tuseme kwa mchoro jinsi ulivyo tukadirie kila chumba kina m3×m3, sebule m5×m3, dining m4×m2.5, vyoo kila kimoja m2×m2.5, kitchen, kibaraza cha jikoni na store m5×m2.5

  • Hapo unapata usable space jumla ya msq 73.5

(Hiyo ni usable space haijajumuisha corridor, upana wa kuta na veranda)

Tuje kwenye makadirio ya upana na urefu wa hiyo nyumba

  • Hapo upana wa nyumba ni kama m10 na urefu ni m11 (m10×m11) = msq 121

(Kiwanja cha msq 72-81 hakitatosha kujenga hiyo nyumba ya ndoto yako)

Hautapata hata sehemu ya kupark gari, kabustani kakishikaji, watoto pa kucheza au pa kukaa watu siku ukifa
sahihi kbsa
 
Ndugu

Je hii ramani inaenea kwenye eneo la aquare mita 150 na kubakiza sehemu ya kupaki kagari na kuanika nguo.... Naombeni mawazo yenu ikibidi sana naombeni na vipimo

Mimi nilikuwa na waza icheze kwenye square mita 72 au 81 square meter...

Naombeni mawazo yenu na vipimo vizuri kadiri muwezavyoView attachment 3564803
wengine hatujasoma mkuu hio square meter ndo nini hiko..
 
Bila vipimo ni ngumu kukadiria

Tuseme kwa mchoro jinsi ulivyo tukadirie kila chumba kina m3×m3, sebule m5×m3, dining m4×m2.5, vyoo kila kimoja m2×m2.5, kitchen, kibaraza cha jikoni na store m5×m2.5

  • Hapo unapata usable space jumla ya msq 73.5

(Hiyo ni usable space haijajumuisha corridor, upana wa kuta na veranda)

Tuje kwenye makadirio ya upana na urefu wa hiyo nyumba

  • Hapo upana wa nyumba ni kama m10 na urefu ni m11 (m10×m11) = msq 121

(Kiwanja cha msq 72-81 hakitatosha kujenga hiyo nyumba ya ndoto yako)

Hautapata hata sehemu ya kupark gari, kabustani kakishikaji, watoto pa kucheza au pa kukaa watu siku ukifa
Shukrani sana mkuu.. vipi kwenye square meter 150 unaonaje kutakua na sehemu hata ya jumuia kusali?
Mi hayo ma square meters hata sijui,najuaga 40*20, 40"40 tu
hayo unayo jua sasa unazidisha ndo unapata square meter mkuu
 
Ndugu

Je hii ramani inaenea kwenye eneo la aquare mita 150 na kubakiza sehemu ya kupaki kagari na kuanika nguo.... Naombeni mawazo yenu ikibidi sana naombeni na vipimo

Mimi nilikuwa na waza icheze kwenye square mita 72 au 81 square meter...

Naombeni mawazo yenu na vipimo vizuri kadiri muwezavyoView attachment 3564803
Weka nguzo halafu hii iwe ghorofa ya kwanza. Chini yake utapata nafasi ya parking, kuanika nguo n.k.

Amandla....
 
Ndugu

Je hii ramani inaenea kwenye eneo la aquare mita 150 na kubakiza sehemu ya kupaki kagari na kuanika nguo.... Naombeni mawazo yenu ikibidi sana naombeni na vipimo

Mimi nilikuwa na waza icheze kwenye square mita 72 au 81 square meter...

Naombeni mawazo yenu na vipimo vizuri kadiri muwezavyoView attachment 3564803
Ondoa mlango wa kuingia jikoni kutoka kwenye terrace ili upate nafasi ya kutosha ya kaunta na makabati ya kutosha jikoni. Mlango uhamishiwe kwenye pantry, mtu atoke kwenye terrace aingie kwenye pantry ndio aingie jikoni. Badala ya mlango wa jikoni weka dirisha ili mtu akiwa jikoni aone kinachoendelea kwenye terrace na jiko liwe na mwanga na upepo wa kutosha. Na wasiwasi kama bafu la watoto litatosha kuwa na choo, beseni la kunawia na sehemu ya kuogea. Aidha, hauna stoo.

Amandla...
 
Ondoa mlango wa kuingia jikoni kutoka kwenye terrace ili upate nafasi ya kutosha ya kaunta na makabati ya kutosha jikoni. Mlango uhamishiwe kwenye pantry, mtu atoke kwenye terrace aingie kwenye pantry ndio aingie jikoni. Badala ya mlango wa jikoni weka dirisha ili mtu akiwa jikoni aone kinachoendelea kwenye terrace na jiko liwe na mwanga na upepo wa kutosha. Na wasiwasi kama bafu la watoto litatosha kuwa na choo, beseni la kunawia na sehemu ya kuogea. Aidha, hauna stoo.

Amandla...
Asante mkuu na vipi kwa square meter hizo 72 yaani mita 8*9 au 9*9 nyumba itakua atleast njema mkuu ?
 
Asante mkuu na vipi kwa square meter hizo 72 yaani mita 8*9 au 9*9 nyumba itakua atleast njema mkuu ?
Haienei. Kwenye maeneo yaliyopimwa unatakiwa kubakiza nafasi ya angalau mita 1 na nusu pande tatu na mita 3 mbele. Hivyo sana sana utakuwa na nafasi ya kujenga ya mita 6.9 ambazo zinatosha kupanga vyumba viwili tu. Bado hujafikiria septic tank na soak pit. Ukipandisha utaweza kujibanabana. Kwa nyumba hii, tafuta kiwanja kingine.

Amandla...
 
Back
Top Bottom